Genesis 33

Genesis 33:1

Esau alipokuwa akija kwa Yakobo, Yakobo aliwaweka wake zake kwa mpangilio upi nyuma yake?

Yakobo aliwaweka watumishi wake wa kike kwanza, kisha Lea na baadae Raheli.

Yakobo alifanya nini alipokuja karibu na kaka yake?

Yakobo aliinama kuelekea ardhini mara saba alipokuja karibu na kaka yake.

Genesis 33:4

Esau alifanya nini alipokuja kwa ndugu yake?

Esau alikimbia kukutana na Yakobo, akamkumbatia, akakumbatia shingo yake, na kumbusu.

Genesis 33:9

Esau alimwambia nini Yakobo kufanya na zawadi alizozituma mapema kwa Esau?

Esau alimwambia Yakobo kubaki nazo mwenyewe, kwa kuwa alikuwa na za kutosha.

Ni sababu gani mbili Yakobo alimpa Esau apokee zawadi zake?

Yakobo alisema ya kwamba kwa sababu Mungu amemtendea mema kwake, na kwa sababu alikuwa na vya kutosha, Esau alipaswa kupokea zawadi zake.

Genesis 33:12

Kwa nini Yakobo alisema anataka Esau aende kabla yake, wakati yeye akisafiri taratibu zaidi?

Yakobo alisema alitaka Esau aende kabla yake kwa sababu wanyama wake wangekufa kama wangepelekeshwa kwa haraka sana.

Yakobo alisema angekwenda kuwaleta familia yake na wanyama wake wapi?

Yakobo alisema alikwenda kuwaleta familia yake na wanyama kwa Esau huko Seiri.

Genesis 33:15

Yakobo alisafiri kwenda wapi, ambapo alijijengea nyumba?

Yakobo alisafiri kwenda Sukothi, ambapo alijijengea nyumba.

Genesis 33:18

Yakobo alisafiri kwenda wapi, ambapo alijinunulia kipande cha ardhi?

Yakobo alisafiri kwenda Shekemu, ambapo alinunua kipande cha ardhi.