Genesis 32

Genesis 32:3

Yakobo alituma ujumbe kwa nani alipokuwa njiani kuelekea Kaanani?

Yakobo alituma ujumbe kwa kaka yake Esau katika njia ya kuelekwa Kaanani.

Kwa sababu ipi Yakobo alituma ujumbe huu

Yakobo alitamani kupata kibali machoni pa Esau.

Genesis 32:6

Mwitikio wa Yakobo aliposikia Esau alikuwa akija na watu mia nne ulikuaje, na alifanya nini?

Yakobo aliogopa, kwa hiyo aligawanyisha watu wake katika makundi mawili ili kwamba kama Esau atashambulia kundi moja, kundi lingine liweze kutoroka.

Genesis 32:11

Ombi la Yakobo kwa Yahwe lilikuwa lipi?

Yakobo alimuuliza Yahwe kumuokoa kutoka mkono wa Esau.

Juu ya ahadi gani Yakobo alimkumbusha Yahwe?

Yakobo alimkumbusha Yahwe ya kuwa aliahidi kumfanikisha Yakobo, na kufanya uzao wake kama mchanga wa bahari.

Genesis 32:19

Yakobo alifikiri angefanikisha nini kwa kutuma zawadi kwa ndugu yake Esau?

Yakobo alifikiri ya kwamba labda angeweza kumtuliza Esau kwa zawadi ambazo alituma kwa Esau ili kwamba baadae, Yakobo atakapomuona, Esau aweze kumpokea.

Genesis 32:22

Yakobo aliishiaje kuwa peke yake usiku huo?

Alichukua wake zake, watumishi wake wa kike, na watoto wake katika kijito cha Yaboki.

Genesis 32:24

Yakobo alifanya nini usiku huo mpaka alfajiri?

Yakobo alishindana na mtu mpaka alfajiri.

mtu alifanya nini alipoona hakuweza kumshinda Yakobo?

Mtu alipiga nyinga ya Yakobo na kuitengua.

Yakobo alidai nini kabla ya kumruhu mtu kuondoka?

Yakobo alidai ya kwamba mtu ambariki.

Genesis 32:27

Mtu alisema jina la Yakobo lingekuwa lipi?

Mtu alisema ya kwamba jina la Yakobo sasa lingekuwa Israeli.

Genesis 32:29

Yakobo alisema amemuona nani uso kwa uso usiku huo?

Yakobo alisema amemuona Mungu uso kwa uso usiku huo.

Genesis 32:31

Yakobo alipata tatizo gani la kimwili baada ya usiku huo?

Yakobo alichechemea kwa sababu ya nyonga yake baada ya usiku huo.