Genesis 18

Genesis 18:1

Abrahamu alipokuwa ameketi mlangoni mwa hema lake, aliona nini alipotazama juu?

Abrahamu aliona wanamume watatu wamesimama mbele yake.

Genesis 18:3

Abrahamu aliwapatia nini wanamume hawa?

Abrahamu aliwapatia wanamume hawa maji ya kunawa, na chakula kidogo.

Genesis 18:9

Sara alikuwa wapi mgeni alipotoa utabiri wake?

Sara alikuwa ndani ya tenti.

Mgeni mmoja alitoa utabiri gani kuhusu Sara?

Mgeni mmoja alisema ya kwamba atakaporudi, Sara angekuwa na mtoto wa kiume.

Genesis 18:11

Sara alichukuliaje utabiri wa mgeni?

Sara alicheka mwenyewe aliposikia utabiri wa mgeni.

Genesis 18:13

Yahwe, mgeni, alisema kitu gani kuhusu mwitikio wa Sara?

Yahwe alimuuliza Sara kwa nini alicheka, kwa kusema, "Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe?"

Genesis 18:16

Wanamume walipoondoka katika nyumba ya Abrahamu, walielekea upande gani?

Wanamume waliondoka nyumbani mwa Abrahamu na kuelekea upande wa Sodoma.

Yahwe aliuliza swali gani walipokuwa wakitembea?

Yahwe alisema, "Je nimfiche Abrahamu kile ninachokusudia kufanya"?

Yahwe alisema Abrahamu anapaswa kufanya nini ili kwamba Yahwe aweze kutimiza ahadi iliyopewa kwa Abrahamu?

Yahwe alisema ya kwamba Abrahamu anapaswa kuwaongoza watoto wake na nyumba yake kutenda utakatifu na haki.

Genesis 18:20

Kwa nini wanamume walikuwa wakielekea upande wa Sodoma?

Wanamume walikuwa wakielekea upande wa Sodoma kwa sababu vilio dhidi ya Sodoma na Gomora vilikuwa vikubwa, na walitaka kuona kama miji ilikuwa na uovu kama vilio vilivyoashiria.

Genesis 18:22

Abrahamu aliposimama na Yahwe, alimuuliza swali gani Yahwe?

Abrahamu aliuliza, "Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?"

Genesis 18:24

Yahwe alisema angefanya nini iwapo kungekuwa na watakatifu hamsini ndani ya mji?

Yahwe alisema angeacha kuangamiza sehemu ile yote kwa niaba yao.

Genesis 18:27

Yahwe alisema angefanya nini iwapo kungekuwa na watakatifu arobaini na tano ndani ya mji?

Yahwe alisema angeacha kuangamiza sehemu ile yote kwa niaba yao.

Genesis 18:29

Yahwe alisema angefanya nini iwapo kungekuwa na watakatifu arobaini ndani ya mji?

Yahwe alisema angeacha kuangamiza sehemu ile yote kwa niaba yao.

Yahwe alisema angefanya nini iwapo kungekuwa na watakatifu thelathini ndani ya mji?

Yahwe alisema angeacha kuangamiza sehemu ile yote kwa niaba yao.

Yahwe alisema angefanya nini iwapo kungekuwa na watakatifu ishirini ndani ya mji?

Yahwe alisema angeacha kuangamiza sehemu ile yote kwa niaba yao.

Genesis 18:32

Yahwe alisema angefanya nini iwapo kungekuwa na watakatifu kumi ndani ya mji?

Yahwe alisema angeacha kuangamiza sehemu ile yote kwa niaba yao.