Genesis 7

Genesis 7:1

Dume na jike saba wa aina gani ya wanyama walipaswa kuingia ndani ya safina?

Dume na jike saba wa kila mnyama safi na ndege walipaswa kuingia ndani ya safina.

Genesis 7:4

Mungu alisema mvua itaendelea juu ya nchi kwa muda gani?

Mungu alisema ya kwamba mvua itaendelea kwa siku arobaini za mchana na siku arobaini za usiku.

Genesis 7:6

Nuhu alikuwa na umri gani gharika lilipokuja juu ya nchi?

Nuhu alikuwa na umri wa miaka mia sita pale ambapo gharika lilikuja juu ya nchi.

Genesis 7:8

Nuhu aliwaletaje wanyama ndani ya safina?

Wanyama walikuja kwa Nuhu na kuingia ndani ya safina.

Genesis 7:11

Maji ya gharika yalitoka katika vyanzo gani viwili?

Maji yalitoka katika chemichemi zote za vilindi , na kutoka angani.

Genesis 7:15

Pale watu na wanyama walipokwisha ingia ndani ya safina, nani aliufunga mlango?

Yahwe aliufunga mlango nyuma yao.

Genesis 7:19

Maji yalipanda kimo gani juu ya nchi?

Maji yalipanda urefu wa dhiraa kumi na tano juu ya vilele vya milima.

Genesis 7:21

Nini kilikufa juu ya nchi kwa sababu ya gharika?

Viumbe wote waliotembea juu ya nchi, na wanadamu wote walikufa.

Genesis 7:23

Watu gani pekee ndio waliosalia juu ya nchi?

Nuhu pekee na wale waliokuwa naye ndani ya safina walibaki hai.