Genesis 6

Genesis 6:1

Binadamu alipoongezeka juu ya nchi, wana wa Mungu walifanya nini?

Wana wa Mungu walijitwalia kwa ajili yao wake katika binti za binadamu.

Mungu alisema nini juu ya urefu wa maisha ya mwanadamu?

Mungu alisema ya kwamba mwanadamu ataishi miaka 120.

Genesis 6:4

Watu hodari wa zamani, watu wenye sifa walikuwa kina nani?

Watu hodari wa zamani walikuwa majitu makubwa waliozaliwa kutokana na ndoa ya wana wa Mungu na binti za watu.

Genesis 6:5

Yahwe aliona kitu gani ndani ya mioyo ya wanadamu katika siku hizo?

Yahwe aliona ya kwamba uovu wa wanadamu ulikuwa mkubwa, na kwamba kila wazo lao lilikuwa ovu.

Genesis 6:7

Yahwe aliamua kufanya nini na mwanadamu?

Yahwe aliamua kuwafutilia wanadamu katika uso wa nchi.

Lakini ni nani aliyepata kibali na Yahwe?

Nuhu alipata kibali na Yahwe.

Genesis 6:9

Nuhu alikuwa mtu wa aina gani?

Nuhu alikuwa mtu mtakatifu, asiye na lawama, na mtu aliyetembea pamoja na Mungu.

Genesis 6:13

Mungu alimwambia nini Nuhu kufanya kabla Mungu hajaangamiza wanadamu?

Mungu alimwambia Nuhu kujenga safina.

Genesis 6:16

Mungu alisema ataangamiza wenye mwili wote wenye pumzi ya uhai ndani mwao kwa jinsi gani?

Mungu alisema ya kwamba alikwenda kuleta gharika la maji juu ya nchi.

Genesis 6:18

Lakini Mungu alithibitisha agano lake na nani?

Mungu alithibitisha agano lake na Nuhu.

Mungu alimwambia Nuhu amlete nani ndani ya safina?

Mungu alimwambia Nuhu kumleta mke wake, wanawe watatu wa kiume, na wake za wanawe.

Ni wanyama gani waliotakiwa kuletwa ndani ya safina kuwekwa hai?

Wawili wa kila aina ya kiumbe hai, wa kiume na kike, walitakiwa kuletwa ndani ya safina.

Genesis 6:20

Nuhu aliitikiaje amri ya Mungu?

Nuhu alifanya yote aliyoamriwa na Mungu.