Genesis 1

Genesis 1:1

Hapo mwanzo Mungu aliumba nini?

Mungu aliziumba mbingu na nchi.

Roho wa Mungu alikuwa akifanya nini hapo mwanzo?

Roho wa Mungu alikuwa akitembea juu ya vilindi juu ya maji.

Genesis 1:3

Mungu aliumbaje nuru?

Mungu alisema, "na kuwe na nuru"

Genesis 1:6

Mungu alitengeneza nini katika siku ya pili?

Mungu alitengeneza anga katikati ya maji yaliyo kuwa chini ya anga na maji ambayo yalikuwa juu ya anga

Genesis 1:9

Mungu aliitaje ardhi kavu na maji yaliyokusanyika?

Mungu aliita ardhi kavu "nchi" na maji yaliyokusanyika "bahari"

Genesis 1:11

Ni viumbe gani hai Mungu aliviumba siku ya tatu?

Mungu aliumba mimea, miti ya matunda, na miche.

Genesis 1:14

Kusudi la mianga angani ni lipi?

Ni kwa ajili ya kutenganisha mchana na usiku, na kama ishara kwa majira, kwa siku na miaka.

Genesis 1:16

Mungu aliumba nini katika siku ya nne?

Mungu aliumba mianga mikuu miwili na nyota.

Genesis 1:20

Mungu aliumba nini katika siku ya tano?

Mungu aliumba viumbe hai vya baharini, na ndege.

Genesis 1:22

Mungu alitoa amri gani kwa viumbe wa baharini na ndege?

Zaeni na muongezeke.

Genesis 1:26

Mungu aliumba nini katika mfano wake?

Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake.

Mtu alipewa mamlaka juu ya vitu gani?

Mungu alimpatia mtu mamlaka juu ya samaki wa baharini, juu ya ndege wa angani, juu ya wanyama wa kufuga, na juu ya kila kitambaacho kinacho tambaa juu ya nchi.

Kitu gani kilikuwa tofauti juu ya jinsi Mungu alivyoumba mtu?

Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake.

Genesis 1:28

Mungu alimpatia mtu amri gani?

Zaeni na kuongezeka, jazeni nchi na muitawale.

Mungu alimpatia mtu ale nini?

Mungu aliwapatia wao kila mmea uzaao mbegu na kila mti wenye tunda.

Genesis 1:30

Mungu alipoona kila kitu alichokiumba, alifikiri nini juu yake?

Mungu alifikiri ya kwamba kilikuwa chema sana.