Genesis 42

Genesis 42:1

Basi Yakobo akafahamu

Neno "basi" inaweka alama ya sehemu mpya ya simulizi.

Kwa nini mnatazamana?

Yakobo anatumia swali kukaripia watoto wake kwa kutofanya kitu chochote kuhusu nafaka. "Msikae hapo tu!"

Shukeni huko ... chini

Ilikuwa kawaida kuzungumza kuhusu kwenda kutoka Kaanani mpaka Misri kama kwenda "chini"

kutoka Misri

Hapa "Misri" ina maana ya watu kuuza nafaka. "kutoka kwa wale wauzao nafaka ndani ya Misri"

Benjamini, ndugu wa Yusufu, Yakobo hakumtuma

Benyamini na Yusufu walikuwa na baba mmoja na mama. Yakobo hakutaka kuthubutu kumtuma mwanawe wa mwisho wa Raheli.

Genesis 42:5

Wana wa Israeli wakaja kununua miongoni mwao waliokuja

Neno "wakaja" inaweza kutafsiriwa kama "kwenda". Pia, maneno "nafaka" na "Misri" inaeleweka. "Wana wa Israeli walikwenda kununua nafaka pamoja na watu wengine waliokwenda Misri"

Basi Yusufu

"Basi" inaweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa maelezo ya nyuma kuhusu Yusufu.

juu ya nchi

Hapa "nchi" ina maana ya Misri. "juu ya Misri"

watu wote wa nchi

Hapa "nchi" inajumlisha Misri na nchi zingine zinayoizunguka. "watu wote wa mataifa yote waliokuja kununua nafaka"

Ndugu zake Yusufu wakaja

Hapa "wakaja" inaweza kutafsiriwa kama "walikwenda"

kumwinamia na nyuso zao hata chini

Hii ni njia ya kuonyesha heshima.

Genesis 42:7

Yusufu akawaona ndugu zake na kuwatambua

"Yusufu alipowaona ndugu zake, aliwatambua"

alijibadili kwao

"alijifanya kana kwamba hakuwa kaka yao" au "hakuwafahamisha ya kwamba alikuwa kaka yao"

Mmetoka wapi?

Hili halikuwa swali la balagha ingawa Yusufu alijua jibu. Ilikuwa sehemu ya maamuzi yake kuficha utambulisho wake kwa ndugu zake.

Genesis 42:9

Ninyi ni wapelelezi

Wapelelezi ni watu ambao kwa siri hujaribu kupata taarifa kuhusu nchi ili kuisaidia nchi nyingine.

Mmekuja kuona sehemu za nchi

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Mmekuja kujua ni wapi hatulindi nchi yetu ili kwamba muweze kutushambulia"

bwana wangu

Hii ni njia ya kuonyesha heshima kwa mtu.

Watumishi wako wamekuja

Ndugu hawa wanajitambulisha kama "watumishi". Hii ni njia maalumu ya kuongea na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. "Sisi, watumishi wako, tumekuja" au "Tumekuja"

Genesis 42:12

Akawambia

"Yusufu akawaambia ndugu zake"

Hapana, mmekuja kuangalia sehemu za nchi

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Hapana, mmekuja kujua ni wapi hatujalinda nchi yetu ili kwamba muweze kutuvamia"

ndugu kumi na wawili

"ndugu 12"

Tazama, mdogo

"Tusikilize, mdogo". Neno "Tazama" linatumika kusisitiza kile walichosema baadae.

mdogo yupo na baba yetu leo hii

"kwa sasa ndugu yetu mdogo yupo na baba yetu"

Genesis 42:14

Ndivyo nilivyowambia; ninyi ni wapelelezi

"kama nilivyotangulia kusema, nyinyi ni wapelelezi"

Mtajaribiwa kwa njia hii

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hivi ndivyo nitakavyowajaribu"

aishivyo Farao

Msemo huu unaashiria kiapo maalumu.

Mtumeni mmoja wenu amlete mdogo wenu

"Chagueni mmoja wenu kumfuata mdogo wenu"

Mtabaki gerezani

"Mliosalia mtabaki gerezani"

hata maneno yenu yatakapothibitishwa, kama kuna ukweli ndani yenu.

Hapa "maneno" ina maana ya kile alichosema. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba niweze kujua kama mnaniambia ukweli"

kifungoni

"gerezani"

Genesis 42:18

Katika siku ya tatu

Neno "tatu" ni mpangilio wa namba."baada ya siku ya pili"

Fanyeni hivi nanyi mtaishi

Taarifa inayotambulika inaweza kuwekwa wazi. "Kama utafanya kile nilichosema, nitakuruhusu uishi"

ninamcha Mungu

Hii ina maana ya kumheshimu Mungu kwa dhati na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii yeye.

mmoja wenu atazuiliwa hapa gerezani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "muache mmoja wa ndugu zako hapa gerezani"

lakini ninyi nendeni

Hapa "ninyi" ni wingi na ina maana ya ndugu wote ambao hawatakaa gerezani. "lakini ninyi mliosalia"

chukueni nafaka kwa ajili ya nyumba zenu

Hapa "nyumba" ina maana ya familia. "beba nafaka hadi nyumbani kusaidia familia zenu wakati wa njaa hii"

ili kwamba maneno yenu yathibitishwe

Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili niweze kujua kile mnachosema ni kweli"

nanyi hamtakufa

Hii inaashiria ya kwamba Yusufu angewafanya maaskari wake kuwaua ndugu iwapo angetambua ya kwamba walikuwa wapelelezi.

Genesis 42:21

kwani tuliona tabu ya nafsi yake

Neno "nafsi" ina maana ya Yusufu. "kwa sababu tuliona jinsi gani Yusufu alivyotaabika" au "kwa sababu tuliona ya kwamba Yusufu aliteseka"

Kwa hiyo taabu hii imeturudia

Nomino inayojitegemea "taabu" inaweza kuwekwa kama kitenzi "kuteseka" "Ndio maana tunateseka hivi sasa"

Je sikuwambia, 'Msitende dhambi juu ya kijana,' lakini hamkusikia?

Rubeni anatumia swali kuwakaripia ndugu zake. "Niliwaambia kutomuumiza kijana, lakini hamkunisikiliza!"

Je sikuwambia, 'Msitende dhambi juu ya kijana'

Hii inaweza kuwa nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Je sikuwaambia msimtendee dhambi kijana" au "Niliwaambia msimdhuru kijana"

Basi, tazama

Hapa "basi" haimaanishi "katika muda huu" lakini yote maneno "Sasa" na "tazama" yanatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

damu yake inatakiwa juu yetu

Hapa "damu" ina maana ya kifo cha Yusufu. Ndugu zake walidhani Yusufu alikufa. Msemo "inatakiwa juu yetu" una maana wanatakiwa kuadhibiwa kwa kile walichokifanya. "tunapata kile tunachostahili kwa kifo chake" au"tunateseka kwa kumuua yeye"

Genesis 42:23

hawakuja ... mkalimani kati yao

Hii inabadilisha kutoka kwenye simulizi kuu kwenda kwenye taarifa ya nyuma ambayo inaelezea kwa nini ndugu walidhani Yusufu hakuweza kuwaelewa.

mkalimani

"Mkalimani" ni mtu ambaye hutafsiri kile mtu anazungumza katika lugha nyingine. Yusufu aliweka mkalimani kati yake na ndugu zake kufanya ionekane kana kwamba hakuzungumza lugha yake.

Akatoka kwao na kulia

Inasemekana ya kwamba Yusufu alilia kwa sababu alipatwa na hisia baada kusikia walichosema ndugu zake.

kuongea nao

Yusufu aliendelea kuzingumza katika lugha nyingine na kutumia mkalimani kuzungumza na ndugu zake.

kumfunga mbele ya macho yao

Hapa "macho" ina maana ya machoni mwao. "alimfunga machoni mwao" au "alimfunga huku wakitazama"

na kuwapa mahitaji

"kuwapatia mahitaji waliyohitaji"

Wakatendewa hivyo

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Watumishi walifanya kwao kila kitu ambachoYusufu aliwaamuru"

Genesis 42:26

Mmoja wao alipofungua gunia lake ili kumlisha punda wao katika sehemu waliyokuwa, akaona pesa yake. Tazama, ilikuwa mdomoni mwa gunia lake

"Waliposimama mahali usiku huo, mmoja wa ndugu alifungua gunia lake kupata chakula kwa ajili ya punda wake. Ndani ya gunia akakuta fedha!"

Tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa inayoshangaza inayofuata.

Pesa yangu imerudishwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu amerudisha fedha yangu"

Tazama

"Tazama ndani ya gunia langu!"

Mioyo yao ikazimia

Kuwa na hofu inazungumziwa kana kwamba mioyo yao ilikuwa ikizama. Hapa "mioyo" ina maana ya ujasiri. "Wakawa na hofu sana"

Genesis 42:29

bwana wa nchi

"bwana wa Misri"

aliongea nasi kwa ukali

"aliongea kwa jazba"

kuwa wapelelezi

Wapelelezi ni watu ambao kwa siri hujaribu kupata taarifa kuhusu nchi ili kuisaidia nchi nyingine.

Tukamwambia, 'Tu watu wa kweli sisi. Sisi siyo wapelelezi. Tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu. Mmoja hayupo hai tena ... nchi ya Kanaani

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Tulimwambia ya kwamba sisi ni watu waaminifu na sio wapelelezi. Tulisema kwamba tu ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu, na kwamba ndugu yetu hayupo hai tena ... nchi ya Kaanani"

Mmoja hayupo hai tena

Neno "ndugu" linaeleweka. "Ndugu mmoja hayupo hai tena"

mdogo yupo na baba yetu

Neno "ndugu" linaeleweka. "ndugu yetu mdogo yupo na baba yetu kwa sasa"

Genesis 42:33

bwana wa nchi

"bwana wa Misri"

chukueni chakula kwa ajili ya njaa katika nyumba zenu

Hapa "nyumba" ina maana ya "familia". "chukua nafaka isaidie familia yenu wakati wa njaa"

mwondoke

"nendeni nyumbani" au "ondokeni"

na mtafanya biashara katika nchi

"na nitawaruhusu mnunue na kuuza katika nchi hii"

Genesis 42:35

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama kwa tukio muhimu katika simulizi.

tazama

"kwa mshangao wao". Neno "tazama" hapa inaonyesha ya kwamba ndugu walishangazwa kwa kile walichokiona.

Mmeniharibia watoto wangu

"umeninyima watoto wangu" au "umesababisha kupoteza watoto wangu wawili"

Mambo haya yote ni kunyume changu

"mambo haya yote yaliniumiza"

Genesis 42:37

Mweke mikononi mwangu

Hili ni ombi la Rubeni kumchukua Benyamini pamoja naye na kumtunza katika safari hiyo. "Niweke kama msimamizi juu yake" au "Niache nimtunze"

Mwanangu hatashuka pamoja nanyi

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" walipokuwa wakizungumzia safari ya Kaanani kuelekea Misri. "Mwanangu, Benyamini, hatakwenda nawe hadi Misri"

pamoja nanyi

Hapa "nanyi" ni wingi na ina maana ya wana wa yakobo wakubwa.

Kwani ndugu yake amekufa na yeye peke yake amebaki

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Kwa maana mke wangu, Raheli, alikuwa na watoto wawili pekee. Yusufu amekufa na Benyamini amebaki mwenyewe tu"

katika njia mnayoiendea

"utakapokuwa ukisafiri kwenda Misri na kurudi" au "utakapokuwa mbali". Hapa "njia" ina maana ya kusafiri.

ndipo mtakapozishusha mvi zangu kaburini kwa huzuni

"mtakapozishusha ... kuzimu" ni njia ya kusema watamsababisha afariki na kushuka kuzimu. Anatumia neno "chini" kwa sababu iliaminika kuzimi ni sehemu chini ya ardhi. "basi mtanisababisha, mtu mzee, kufariki na huzuni"

mvi zangu

Hii ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "mimi, mtu mzee"