Genesis 41

Genesis 41:1

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

mwishoni mwa miaka miwili mizima

Miaka miwili ilipita baada ya Yusufu kutafsiri kwa usahihi ndoto za mnyweshaji wa Farao na mwokaji, ambao walikuwa gerezani pamoja na Yusufu.

Tazama, alikuwa amesimama

Neno "tazama" hapa linaweka alama ya mwanzo wa tukio jipya katika simulizi kuu.

amesimama

"Farao alikuwa amesimama"

Tazama

"Ghafla". Neno la "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa kwa kile alichokiona.

wakupendeza na wanene

"wenye afya na wanene"

wakajilisha katika nyasi

"walikuwa wakila nyasi kando kando ya mto"

nyasi

nyasi ndefu, nyembamba ambazo huota katika maeneo ya unyevunyevu

Tazama, ng'ombe wengine saba

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa tena kwa kile alichokiona.

wasiopendeza na wamekondeana

"wagonjwa na wembamba"

ukingoni mwa mto

"kando kando ya mto" au "kando ya mto". Hii ni sehemu ya juu ya ardhi pembeni mwa mto.

Genesis 41:4

wasiopendeza na waliokonda

"dhaifu na nyembamba"

wanapendeza na walionenepa

"yenye afya na iliyolishwa vizuri"

akaamka

"aliamshwa"

mara ya pili

Neno "mara ya pili" ni mpangilio wa namba. "tena"

Tazama, masuke saba

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa kwa kile alichokiona.

masuke ya nafaka

Vichwa ni sehemu ya mmea wa mahindi ambao mbegu huota.

yalichipua katika mche mmoja

"yaliota katika shina moja" Shina ni sehemu nene au ndefu ya mmea.

katika mche mmoja, mema na mazuri

"katika mche mmoja na ilikuwa yenye afya na nzuri"

membamba na yaliyokaushwa na upepo wa mashariki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo ilikuwa nyembamba na kuchomwa kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"

upepo wa mashariki

Upepo kutoka mashariki ulivuma kutoka jangwani. Joto la upepo wa mashariki mara kwa mara ulikuwa wenye uharibifu.

yakachipua

"yaliota" au "kukua"

Genesis 41:7

Masuke membamba

Maneno "ya mbegu" inaeleweka. "Vichwa vyembamba vya mbegu"

yakayameza

"wakala". Farao anaota ya kwamba mahindi ambayo hayana afya yanaweza kumeza mahindi yenye afya kama mtu anavyokula chakula.

masuke saba mema yote

"vichwa vyenye afya na vizuri"

akaamka

"aliamshwa"

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa na kile alichokiona.

ilikuwa ni ndoto

"alikuwa akiota"

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

roho yake ikafadhaika

Hapa neno "roho" lina maana ya utu wake na hisia zake. "alifadhaishwa ndani ya utu wake" au "alisononeshwa"

Akatuma na kuwaita

Inaeleweka ya kwamba aliwatuma watumishi. "Alituma watumishi wake kuwaita" au "Aliwatuma watumishi wake na kuwaita"

waganga na wenye hekima wote wa Misri

Wafalme wa zamani na watawala walitumia wachawi na wenye hekima kama washauri.

Genesis 41:9

mkuu wa wanyweshaji

Mtu muhimu zaidi ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.

Leo ninayafikiri makosa yangu

Neno "Leo" linatumika kuonyesha msisitizo. "makosa" yake ni kwamba alitakiwa kumwambia Farao kitu mapema zaidi lakini hakufanya hivyo. "Nimegundua ya kwamba nimesahau kukuambia jambo"

Farao aliwakasirikia

Mnyweshaji ana maana ya Farao katika mtu wa utatu. Hii ni njia ya kawaida ya mtu mwenye nguvu ya chini kuzungumza na mtu mwenye nguvu zaidi. "Wewe, Farao, ulikuwa na hasira"

watumishi wake

Hapa "wake" ina maana ya Farao. Hapa "watumishi" ina maana ya mnyweshaji na mkuu wa waokaji. "na sisi, watumishi wako"

kuniweka kifungoni katika nyumba ya kapteni wa walinzi, mkuu wa waokaji na mimi

"kuniweka mkuu wa waokaji na mimi gerezani ambapo kapteni wa walinzi alikuwa msimamizi" hapa "nyumba" ina maana ya gereza.

kapteni wa walinzi

Askari msimamizi wa walinzi wa kifalme.

mkuu wa waokaji

Mtu muhimu zaidi ambaye alitengeneza chakula kwa ajili ya mfalme.

Tuliota ndoto usiku huo mmoja, yeye na mimi

"Usiku mmoja wote wawili tulipata ndoto"

Tuliota

Hapa "Tuliota" ina maana ya mkuu wa mnyweshaji na mkuu wa waokaji.

Kila mmoja aliota kwa kadili ya tafsiri yake

"Ndoto zetu zilikuwa na maana tofauti"

Genesis 41:12

Taarifa ya Jumla:

Mkuu wa wanyweshaji anaendelea kuzungumza na Farao.

Pamoja nasi kulikuwa

"Gerezani kulikuwa na mkuu wa waokaji na mimi"

kapteni wa walinzi

Askari msimamizi wa walinzi wa kifalme.

Tulimwambia na akatutafsiria ndoto zetu

"Tulimwambia ndoto zetu na kutueleza maana zake kwetu"

Alitutafsiria kila mmoja wetu kulingana na ndoto yake

Hapa "yake" ina maana ya mnyweshaji na muokaji mmoja mmoja, sio kwa yule anayetafsiri ile ndoto. "Alifafanua kile kilichokuwa kinakuja kutokea kwetu wawili"

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio muhimu la simulizi.

alivyotutafsiria, ndivyo ilivyokuwa

"alivyotafsiri kuhusu ndoto ndivyo kilichotokea hapo baadae"

Farao alinirudisha katika nafasi yangu

Hapa mnyweshaji anatumia jina la Farao katika kuongea naye kama njia ya kumheshimu yeye. "Uliniruhusu nirudi katika kazi yangu!"

yule mwingine

"mkuu wa waokaji"

akamtundika

Hapa "akamtundika" ina maana ya Farao. Na ina maana ya maaskari ambao Farao aliwaamuru kumnyonga mkuu wa waokaji. "uliwaamuru maaskari wako kumnyonga"

Genesis 41:14

Farao alipotuma na kumwita

Inaeleweka ya kwamba Farao aliwatuma watumishi. "Farao aliwatuma watumishi wake kumfuata Yusufu"

wakamtoa gerezani

"nje ya gereza" au "nje ya ile jela"

Akajinyoa mwenyewe

Ilikuwa utaratibu wa kawaida kunyoa ndevu na nywele za kichwani mnapoandaa kwenda mbele ya Farao.

akaingia kwa Farao

Hapa "akaingia" inaweza kuwekwa kama "kwenda". "alikwenda mbele ya Farao"

hakuna wa kuitafsiri

"hakuna awezaye kueleza maana yake"

unaweza kuitafsiri

"unaweza kuelezea maana yake"

Siyo katika mimi

"Mimi siye ambaye naweza kueleza maana yake"

Mungu atamjibu Farao kwa fadhila zake

"Mungu atamjibu Farao kwa fadhila"

Genesis 41:17

tazama, nilisimama

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

ukingo wa mto Nile

Hii ni ardhi iliyo juuzaidi katika ukingo wa Mto Nile.

Tazama, ng'ombe saba

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

wanene na wakuvutia

"waliolishwa vizuri na wenye afya"

wakajilisha katika nyasi

"walikuwa wakila nyasi kando ya mto"

Genesis 41:19

Tazama, ng'ombe wengine saba

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

wabaya, na wembamba

"dhaifu, na wembamba"

wabaya kama hao

Nomino inayojitegemea ya "kutotamanika" inaweza kutafsiriwa kwa kivumishi. "ng'ombe wabaya sana" au "ng'ombe wasiofaa kabisa"

ng'ombe wanene

"ng'ombe waliolishwa vizuri"

haikujulikana kama walikuwa wamewala

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hakuna aliyeweza kutambua ya kwamba ng'ombe wembamba waliwameza ng'ombe wanene"

Genesis 41:22

Taarifa ya Jumla:

Farao anaendelea kumwambia Yusufu ndoto zake.

Niliona katika ndoto yangu

Hii inaanza sehemu inayofuata ya ndoto ya Farao baadaya kuamka na kurudi kulala. "Kisha nikaota tena"

tazama, masuke saba

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

masuke saba

Maneno "ya masuke" inaeleweka. "masuke saba"

yakatoka katika bua moja

"yakatoka katika bua moja". Shina ni sehemu ya mmea mnene na mrefu.

Tazama, masuke saba zaidi

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "yalinyauka, yamekaushwa, myembamba, na kukaushwa na jua kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"

kunyauka

"kuoza" au "nyauka"

upepo wa mashariki

Upepo unaotoka kutoka mashariki ulivuma kutoka jangwani. Joto la upepo wa mashariki mara kwa mara ulikuwa uharibifu kwa mazao.

yakachipua

"yakaota" au "kustawi"

masuke membamba

Maneno "ya masuke" yanaeleweka. "masuke membamba"

yakayameza

"yakala". Farao anaota ya kwamba mahindi dhaifu yanaweza kumeza mahindi yenye afya kama mtu anavyokula chakula.

hakuna aliyeweza

"hapakuwa na mtu mmoja ambaye" au "hakuna kati yao ambaye"

Genesis 41:25

Ndoto za Farao zinafanana

Inadokezwa ya kwamba maana zinafanana. "Ndoto zote mbili zina maana moja"

Mungu amemwambia Farao kuhusu jambo analokwenda kulifanya

Yusufu anazungumza na Farao katika utatu. Kwa njia hii anaonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika upili wa mtu. "Mungu anakuonyesha kile atakachofanya hivi karibuni"

masuke saba mema

Maneno ya "masuke" yanaeleweka. "masuke saba mazuri"

Genesis 41:27

Taarifa ya Jumla

Yusufu anaendelea tafsiri yake kwa ndoto za Farao.

ng'ombe saba wembamba na wabaya

"ng'ombe wembamba na dhaifu"

masuke saba membamba yaliyokaushwa na upepo wa mashariki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Masuke saba yaliyokaushwa na jua kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"

Hilo ni jambo nililomwambia Farao ... nililomwambia Farao

Yusufu anazungumzia kwa Farao katika utatu. Hii ni njia ya kuonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Matukio haya yatatokea kama nilivyokuambia ... imefunuliwa kwako, Farao"

amemfunulia

"amefanya ijulikane"

Tazama

hii inatumika kuweka msisitizo kile ambacho Yusufu anachosema baadae. "Vuta nadhari kwa kile nachosema"

miaka saba yenye utele mwingi inakuja katika nchi yote ya Misri

Hii inazungumzia kuhusu miaka ya wingi kana kwamba muda ni kitu kinachosafiri na kufika mahali. "kutakuwa na miaka saba ambayo kutakuwa na chakula kingi katika nchi yote ya Misri"

Genesis 41:30

Taarifa ya Jumla

Yusufu anaendelea tafsiri ya ndoto za Farao.

miaka saba ya njaa itakuja baada yake

Hii inazungumzia kuhusu miaka saba ya njaa kana kwamba miaka ni kitu kinachosafiri na kufika mahali. "Kisha kutakuwa na miaka saba ambayo kutakuwa na chakula kichache"

wingi wote katika nchi ya Misri utasahaulika ... na njaa itaiaribu nchi. Wingi hautakumbukwa ... kwa sababu ya njaa itakayofuata

Yusufu anaonyesha wazo kwa njia mbili kusisitiza umuhimu wake.

wingi wote katika nchi ya Misri utasahaulika

Hapa "nchi" ina maana ya watu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu wa Misri watasahau kuhusu miaka saba ambayo kulikuwa na chakula kingi"

itaiaribu nchi.

Hapa "nchi" ina maana ya udongo, watu, na nchi nzima.

kwa sababu ya njaa itakayofuata

Hii inazungumzia kuhusu njaa kana kwamba ilikuwa kitu kinachosafiri na kufuata nyuma ya kitu kingine. "kwa sababu ya muda wa njaa utakaotokea hapo baadae"

Kwamba ndoto ilijirudia kwa Farao sababu ni kwamba jambo hili limeanzishwa na Mungu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu alikupatia ndoto mbili kukuonyesha ya kwamba hakika atasababisha mambo haya kutokea"

Genesis 41:33

Maelezo ya Jumla:

Yusufu anaendelea kuongea na Farao.

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Farao atafute

Yusufu anazungumza na Farao katika lugha ya utatu. Hii ni namna ya kuonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Wewe, Farao, unapaswa kutafuta"

kumweka juu ya nchi ya Misri

Msemo "kumweka juu" una maana ya kumpatia mtu mamlaka. "kumpatia mamlaka juu ya ufalme wa Misri" au "kumpa usimamizi juu ya ufalme wa Misri"

nchi ya Misri

Hapa "nchi" ina maana ya watu wote na kila kitu ndani ya Misri.

Na wachukue sehemu ya tano ya mazao ya Misri

Neno "tano" ni sehemu. "Na wagawanishe nafaka ya Misri katika sehemu tano za kufanana, kisha wachukue moja ya sehemu hizo"

katika miaka saba ya shibe

"katika miaka saba ambayo kutakuwa na wingi wa chakula"

Genesis 41:35

Maelezo ya Jumla

Yusufu anaendelea kumshauri Farao.

Na wakusanye

"Waruhusu wageni kukusanya"

cha hii miaka myema ijayo

Hii inazungumzia miaka kana kwamba ni kitu kinachosafiri na kufikia mahali. "katika miaka mizuri ambayo hivi karibuni itatokea"

kuitunza nafaka chini ya mamlaka ya Farao

Msemo "chini ya mamlaka ya Farao" ina maana ya Farao kuwapa mamlaka. "tumia mamlaka ya Farao kutunza nafaka"

Wakiifadhi

Hifadhi nafaka kwa muda wakati ambao kuna chakula kidogo. "Wasimamizi wanatakiwa kuwaacha walinzi pale kulinda nafaka"

Chakula kitakuwa akiba ya nchi

Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Chakula hiki kitakuwa kwa ajili ya watu"

Kwa njia hii nchi haitaaribiwa na njaa

Hapa "nchi" ina maana ya watu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa njia hii watu hawatashinda njaa kipindi cha njaa"

Genesis 41:37

Ushauri huu ukawa mwema machoni pa Farao na machoni pa watumishi wake wote

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Farao na watumishi wake walifikiri huu ulikuwa mpango mzuri"

watumishi wake

Hii ina maana ya watumishi wa Farao.

mtu kama huyu

"mtu kama vile Yusufu alivyomfafanua"

ambaye ndani yake kuna Roho wa Mungu

"ambaye Roho wa Mungu anaishi ndani mwake"

Genesis 41:39

hakuna mtu mwenye ufahamu

"hakuna mtu mwenye uwezo wa kufanya maamuzi"

Utakuwa juu ya nyumba yangu

Hapa "nyumba" ina maana ya kasri ya mfalme na watu ndani ya kasri. Msemo "utakuwa juu" una maana ya Yusufu kuwa na mamlaka juu ya. "Utakuwa na mamlaka juu ya kila mtu ndani ya kasri yangu"

watu wangu watatawaliwa kwa kadili ya neno lako

Hapa "neno" lina maana ya amri au kilichosemwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utatawala juu ya watu wangu na wao watafanya kile unachoamuru"

kiti cha enzi peke yake

Hapa "enzi" ina maana ya utawala wa Farao kama mfalme. "Katika nafasi yangu pekee kama mfalme"

Tazama, nimekuweka

Neno "Tazama" linaweka msisitizo kwa kile Farao anachosema baadae. "Tazama, nimekuweka"

nimekuweka juu ya nchi yote ya Misri

Msemo "nimekuweka juu" una maana ya kutoa mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekuweka kuwa na mamlaka ya kila mtu ndani ya Misri"

Genesis 41:42

Farao akavua pete yake ya mhuri ... mkufu wa dhahabu shingoni mwake

Matendo haya yote yanaashiria ya kwamba Farao anampatia Yusufu mamlaka kufanya kila kitu ambacho Yusufu alipanga.

pete ya mhuri

Pete hii ilikuwa na mhuri wa Mfalme uliochongwa juu yake. Hii ilimpatia Yusufu mamlaka na fedha iliyohitajika kutekeleza mipango yake.

mavazi ya kitani safi

"Kitani" ni kitambaa kilaini, kigumu kinachotengenezwa na mmea wa kitani.

Akataka apandishwe katika kibandawazi cha pili alichokuwa nacho

Tendo hili linadhihirisha wazi kwa watu ya kwamba Yusufu ni wa pili tu kutoka kwa Farao.

Pigeni magoti

"Inama chini na mheshimu Yusufu". Kupiga goti na kuinama chini ilikuwa ishara ya heshima na taadhima.

Farao akamweka juu ya nchi yote

Msemo "kukuweka juu" una maana ya kumpatia mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekupa mamlaka juu ya kila mmoja ndani ya Misri"

Genesis 41:44

Mimi ni Farao, mbali na wewe

Farao anasisitiza mamlaka yake. "Kama Farao, ninaamuru hivi mbali na wewe"

mbali na wewe, hakuna mtu atakayeinua mkono wake au mguu wake katika nchi ya Misri

Hapa "nchi" na "mguu" zina maana ya matendo ya mtu. "hakuna mtu ndani ya Misri ataweza kufanya kitu chochote bila ruhusa yako" au "kila mtu ndani ya Misri lazima akuombe ruhusa kabla hajafanya jambo lolote"

hakuna mtu

Hapa "mtu" ina maana ya binadamu kwa ujumla, iwe wa kiume au wakike.

Zafenathi Panea

Jina la Zafenathi Panea kina maana ya "mfunuaji wa siri"

Akampa Asenathi, binti wa Potifera kuhani wa On, kuwa mke wake

Makuhani wa Misri walikuwa tabaka la juu kabisa na upendeleo. Ndoa hii inaashiria nafasi ya Yusufu ya heshima na upendeleo.

Akampa Asenathi

"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Farao alimpatia Yusufu kuwa mke wake.

binti wa Potifera

"Potifera" ni baba wa Asenathi.

kuhani wa Oni

Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.

Yusufu akaenda juu ya nchi yote ya Misri

Yusufu alisafiri katika nchi kusimamia maandalizi ya ujio wa ukame.

Genesis 41:46

umri wa miaka thelathini

"umri wa miaka 30"

aliposimama mbele ya Farao

Hapa "aliposimama" ina maana ya Yusufu kuanza kumtumikia Farao. "alipoanza kumtumikia Farao"

kwenda katika nchi yote ya Misri

Yusufu anakagua nchi anapoandaa kutekeleza mipango yake.

Katika miaka saba ya shibe

"Katika miaka mizuri saba"

nchi ilipozaa kwa wingi

"nchi ilizaa mavuno makubwa"

Genesis 41:48

Akakusanya ... kukiweka

Hapa "Akakusanya" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwaamuru watumishi wake kukusanaya ... Wakaweka"

Yusufu akahifadhi nafaka kama mchanga wa bahari

Hii inalinganisha nafaka na mchanga wa bahari kuweka msisitizo wa idadi yake kubwa. "Nafaka ambayo Yusufu alihifadhi ilikuwa nyingi kama mchanga wa baharini.

Yusufu akahifadhi ... akaacha

Hapa "Yusufu" na "akahifadhi" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwafanya watumishi wake wahifadhi ... wakaacha"

Genesis 41:50

Kabla miaka ya njaa kuingia

Hii inazungumzia kuhusu miaka saba kana kwamba ni kitu kinachosafiri na kuja kutulia mahali. "kabla ya miaka saba ya njaa kuanza"

Asenathi

"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Faro alimpatia Yusufu kama mke wake.

binti wa Potifera

"Potifera" ni baba wa Asenathi.

kuhani wa Oni

Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.

Manase

"Jina la 'Manase' lina maana ya "kusababisha kusahau""

nyumba ya baba yake

Hii ina maana ya baba wa Yusufu Yakobo na familia yake.

Efraimu

"Jina la 'Efraimu' lina maana ya 'kuwa na uzao' au 'kupata watoto'"

amenipa uzao

Hapa "uzao" ina maana ya kufanikiwa au kupata watoto.

katika nchi ya mateso yangu

Nomino inayojitegemea "mateso" inaweza kuwekwa kama "nimeteseka". "katika nchi hii ambayo nimeteseka".

Genesis 41:53

katika nchi yote

Katika mataifa yanayozunguka mbele zaidi ya Misri, kujumuisha na nchi ya Kanaani.

lakini katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula

Inasemekana ya kwamba kulikuwa na chakula kwa sababu Yusufu aliwaamuru watu wake kuhifadhi chakula katika kipindi cha miaka saba mizuri.

Genesis 41:55

Nchi yote ya Misri ilipokuwa na njaa

Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Ambapo Wamisri waliposhikwa na njaa"

Njaa ilikuwa juu ya uso wote wa nchi

Neno "uso" lina maana ya sehemu ya juu ya ardhi. "Njaa ilisambaa katika nchi yote"

Yusufu akafungua ghala zote na kuuza chakula kwa Wamisri

Hapa "Yusufu" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwafanya watumishi wake kufungulia maghala yote na kuuza nafaka kwa Wamisri"

Dunia yote ilikuwa inakuja Misri

Hapa "dunia" ina maana ya watu kutoka maeneo yote. "Watu walikuwa wakija Misri kutoka maeneo yaliyozunguka"

katika dunia yote

"katika nchi yote". Inawezekana ya kwamba wafanyabiashara tofauti na mataifa ambayo yalikuwa sehemu ya njia za biashara na Misri yalioguswa na ukame walikuja Misri kwa ajili ya nafaka.