Genesis 33

Genesis 33:1

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari juu ya sehemu mpya ya simulizi ya kushangaza.

watu mia nne

"wanamume 400"

Yakobo akawagawanya watoto ... wajakazi wawili wakike

Hii haimaanishi Yakobo aliwagawanya watoto wake sawa sawa ili kwamba kila mwanamke awe na idadi sawa ya watoto pamoja nao. Yakobo aliwagawa watoto ili kila mmoja aondoke na mama yake.

watumishi wa kike

"watumishi wa kike wake zake". Hii ina maana ya Bilha na Zilpa"

Yeye mwenyewe akatangulia mbele yao

Hapa "mwenyewe" inasisitiza ya kwamba Yakobo aliondoka peke yake mbele ya wenzake.

Akasujudu

Hapa neno "sujudu" lina maana ya kuinama chini kuonyesha kwa unyenyekevu heshima na taadhima kwa mtu.

Genesis 33:4

kumlaki

"kukutana na Yakobo"

akamkumbatia, akakumbatia shingo yake na kumbusu

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Esau aliweka mikono yake kumzunguka Yakobo, kumkumbatia, na kumbusu"

Kisha wakalia

Hii inaweza kusemwa kwa uwazi zaidi. "Kisha Esau na Yakobo wakalia kwa sababu walikuwa na furaha kuonana tena"

aliona wanawake na watoto

"akawaona wanawake na watoto waliokuwa na Yakobo"

Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako

Msemo "mtumishi wako" ni njia ya upole ya Yakobo akimaanisha yeye mwenyewe. "Hawa ni watoto ambao Mungu amenipatia mtumishi wako, kwa neema yake"

Genesis 33:6

watumishi wa kike

"watumishi wa kike wake zake". Hii ina maana ya Bilha na Zilpa.

wakasujudia

Hii ni ishara ya unyenyekevu na heshima mbele za mtu mwingine.

Unamaanisha nini kwa makundi haya yote niliyokutana nayo?

Msemo wa "makundi haya yote" una maana ya makundi ya watumishi ambao Yakobo aliwatuma kutoa zawadi kwa Esau. "Kwa nini ulituma makundi haya yote tofauti kuja kukutana nami?"

Kutafuta kibali machoni mwa bwana wangu.

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Ili kwamba wewe, bwana wangu, ufurahishwe na mimi"

bwana wangu

Msemo "bwana wangu" ni njia ya upole inayomaanisha Esau.

Genesis 33:9

Ninayo ya kutosha

Neno "wanyama" au "mali" linaeleweka. "Nina wanyama wa kutosha" au "Nina mali ya kutosha"

ikiwa nimeona kibali machoni pako

Hapa "machoni" ina maana ya fikra au mawazo ya mtu. "Kama unapendezwa na mimi"

zawadi yangu kutoka mkononi mwangu

Hapa "mkononi" ina maana ya Yakobo. "zawadi hii nayokupatia"

mkononi mwangu, kwa maana

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "mkono wangu. Kwa uhakika"

nimeona uso wako, na ni kama kuona uso wa Mungu

Maana ya tashbihi hii haipo wazi. Maana zaweza kuwa 1) Yakobo amefurahi ya kwamba Esau amemsamehe kama Mungu alivyomsamehe au 2) Yakobo anashangazwa kumuona kaka yake tena kama alivyoshangazwa kumuona Mungu au 3) Yakobo ananyenyekea kuwa mbele ya Esau kama alivyonyenyekea kuwa mbele za Mungu.

nimeona uso wako

Hapa "uso" ina maana ya Esau. Ni vyema kutafsiri kama "uso" kwa sababu ya umuhimu wa neno "uso" hapa pamoja na "uso wa Mungu" na "uso kwa uso" katika 32:29.

uliyoletewa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambazo watumishi wangu wamekuletea"

Mungu amenitendea kwa neema

"Mungu amenitendea wema sana" au "Mungu amenibariki sana"

Hivyo Yakobo akamsihi, na Esau akamkubali

Ilikuwa utamaduni kukataa zawadi kwanza, lakini kukubali zawadi ile baadae kabla ya mtoaji kukwazika.

Genesis 33:12

Bwana wangu anajua

Hii ni njia ya upole na maalumu ya kumhusu Esau. "Wewe, bwana wangu, unajua"

watoto ni wadogo

Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "watoto ni wadogo sana kusafiri haraka"

Ikiwa watapelekwa kwa haraka hata siku moj

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "tukiwalazimisha kwenda haraka sana hata kwa siku moja"

Tafadhari bwana wangu na amtangulie mtumishi wake

Hii ni njia ya upole na maalumu ya Yakobo kujitaja mwenyewe. "Bwana wangu, mimi ni mtumishi wako. Tafadhali nenda mbele yangu"

kwa kadili ya mifugo iliyo mbele yangu

"kwa kasi ya wanyama naowatunza wanaweza kwenda"

Seiri

Hili ni eneo lenye milima katika eneo la Edomu.

Genesis 33:15

Kwa nini kufanya hivyo?

Yakobo anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba Esau hahitaji kubakiza wanamume. "Usifanye hivyo!" au "Hahitaji kufanya hivyo!"

Bwana wangu amekuwa

Hii ni njia ya upole na maalumu ya kumaanisha Esau. "Wewe, bwana wangu, umekuwa"

Sukothi

"Jina la Sukothi lina maana ya "hifadhi".

akajijengea nyumba

Inasemekana ya kwamba nyumba ni ya familia yake pia. "alijenga nyumba kwa ajili yake mwenyewe na familia yake"

kwa ajili ya mifugo wake

"kwa wanyama aliowatunza"

Genesis 33:18

Taarifa ya Jumla:

Hii inaanza sehemu mpya ya simulizi. Mwandishi anaelezea kile Yakobo alichofanya baada ya kupumzika Sukothi.

Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu

"Baada ya Yakobo kuondoka Padani Aramu"

Yakobo ... alipokuja ... Akapiga kambi

Hii inamtaja Yakobo pekee kwa sababu ni kiongozi wa familia. Inasemekana ya kwamba familia yake ilikuwa pamoja naye.

Akapiga kambi karibu

"Aliweka kambi yake karibu"

sehemu ya ardhi

"kipande cha ardhi"

Hamori

Hili ni jina la mwanamume.

baba wa Shekemu

Shekemu ni jina la mji na jina la mwanamume.

mia

"100"

El Elohe Israeli

"Jina la El Elohe Israeli lina maana ya "Mungu, Mungu wa Israeli"