Genesis 20

Genesis 20:1

Shuri

Hili ni eneo la jangwa upande wa mashariki wa mpaka wa Misri.

akatuma watu wake kumchukua Sara

"aliwafanya wanamume wake kumfuata Sara na kumleta kwake"

Mungu akamtokea Abimeleki

"Mungu akamtokea Abimeleki"

Tazama

Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "Nisikilize"

wewe ni mfu

Hii ni njia ya nguvu ya kusema mfalme atakufa. "hakika utakufa hivi karibuni" au "Nitakuua"

mke wa mtu

"mwanamke aliyeolewa"

Genesis 20:4

Basi ... hajamkaribia

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya kubadilisha kutoka kwenye simulizi kwenda kwa taarifa kuhusu Abimeleki.

Abimeleki alikuwa bado hajamkaribia

Hii ni njia ya upole ya kusema hakufanya ngono pamoja naye. "Abimeleki hakulala na Sara" au "Abimeleki hakumgusa Sara"

hata taifa lenye haki

Hapa "taifa" lina maana ya watu. Abimeleki ana wasiwasi ya kwamba Mungu atawaadhibu sio yeye tu, lakini watu wake pia. "hata watu wasio kuwa na hatia"

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?' Hata Sara mwenyewe alisema, 'ni kaka yangu.'

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Zinaweza kutajwa kwa nukuu isiyo dhahiri. "Je sio yeye mwenyewe aliyeniambia ya kwamba huyo ni dada yaek? Hata yeye mwenyewe alinimbia ya kwamba ni kaka yake"

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?

Abimeleki alitumia swali la balagha kumkumbusha Mungu juu ya jambo alilokuwa akilifahamu tayari. Hii inaweza kufanywa kuwa kauli. "Abrahamu mwenyewe aliniambia 'Huyu ni dada yangu'" au "Abrahamu alisema ya kwamba ni dada yake".

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, ...Hata Sara mwenyewe

Maneno "yeye mwenyewe" na "Sara mwenyewe" yanatumika kuweka msisitizo kuleta nadhiri kwa Abrahamu na Sara na kuwalaumu kwa kilichotokea.

Nimefanya hili katika uadilifu wa moyo wangu na katika mikono isiyo na hatia.

Hapa "moyo" una maana ya mawazo yake au nia zake. Pia "mikono" hapa ina maana ya matendo yake. "Nimefanya hili kwa nia njema na matendo mema" au "Nimefanya hivi bila mawazo au matendo ya uovu"

Genesis 20:6

Mungu akasema naye

"Mungu akasema kwa Abimeleki"

umefanya hili katika uadilifu wa moyo wako

Hapa"moyo" una maana ya mawazo na nia zake. "ulifanya hivi kwa nia njema" au "ulifanya hivi bila kuwa na nia ya uovu"

umshike

Hii ni lugha ya upole kwa kufanya ngono na Sara. "kulala naye"

mke wa mtu

"Mke wa Abrahamu"

utaishi

"Nitakuruhusu uishi"

wote walio wa kwako

"nyie watu wote"

Genesis 20:8

Akawasimulia mambo haya yote

"Aliwaambia kila kitu ambacho Mungu alimwambia"

Umetufanyia jambo gani?

Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumshtaki Abrahamu. "Umefanya jambo hili baya kwetu!" au "Tazama ulichokifanya kwetu!"

Umetufanyia

Neno "umetufanyia" hapa linajitegemea na halimhusu Abrahamu na Sara.

Ni kwa jinsi gani nimekutenda dhambi kwamba umeniletea ... dhambi?

Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumkumbusha Abrahamu ya kwamba hakufanya dhambi dhidi ya Abrahamu. "Sijafanya jambo dhidi yako kusababisha wewe ulete ... dhambi."

kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi hii kubwa

Kumsababishia mtu awe na hatia ya kutenda dhambi inazungumzwa kana kwamba "dhambi" ilikuwa jambo linaloweza kuwekwa juu ya mtu. "ya kwamba umetufanya mimi na ufalme wangu kuwa na hatia kwa dhambi hii mbaya"

ufalme wangu

Hapa "ufalme" ina maana ya watu. "juu ya watu wa ufalme wangu"

Umenifanyia mimi jambo ambalo halipaswi kufanywa

"Usingefanya jambo hili kwangu"

Genesis 20:10

Nini kilikushawishi wewe kutenda jambo hili?

"Nini kilisababisha ufanye hivi?" au "Kwa nini ulifanya hivi?" Kile ambacho Abrahamu alifanya kinaweza kuwekwa wazi. "Kwa nini uliniambia ya kwamba Sara ni dada yako?"

kwasababu nilifikiri hakika hakuna hofu ya Mungu katika sehemu hii, na kwamba wataniua kwa ajili ya mke wangu.

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika nukuu tofauti. "Kwa sababu nilidhani ya kwamba kwa kuwa hakuna mwenye hofu ya Mungu hapa, mtu anaweza kuniua ili amchukue mke wangu"

hakuna hofu ya Mungu katika sehemu hii

Hapa "sehemu" ina maana ya watu. "hakuna mtu hapa Gerari mwenye hofu ya Mungu"

hofu ya Mungu

Hii ina maana ya kumheshimu Mungu sana na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii.

Licha ya kwamba kweli ni dada yangu

"Pia, ni kweli ya kwamba Sara ni dada yangu" au "Pia, Sara ni dada yangu ki ukweli"

binti wa baba yangu, ingawa si binti wa mama yangu

"tuna baba mmoja, lakini mama tofauti"

Genesis 20:13

Taarifa ya Jumla:

Mstari wa 13 ni muendelezo wa jibu la Abrahamu kwa Abimeleki.

nyumba ya baba yangu

Hapa "nyumba" ina maana ya familia ya Abrahamu. "baba yangu na familia yangu yote" au "nyumba ya baba yangu"

nilimwambia mke wangu, kwa kila sehemu tutakayo kwenda, unioneshe uaminifu wako kama mke wangu: Kila mahali tutakapo kwenda, useme juu yangu kuwa, "Ni kaka yangu."'''

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika nukuu tofauti. "Nilisema kwa Sara ya kwamba nataka awe mwaminifu kwangu kwa kuwaambia watu kila mahali tuendapo ya kwamba mimi ni kaka yake"

Abimeleki akatwaa

"Abimeleki akaleta baadhi"

Genesis 20:15

Abimeleki akasema

"Abimeleki akasema kwa Abrahamu"

Tazama

Hapa na katika mstari wa 16 neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

Nchi yangu i mbele yako

Hii ni njia ya kusema "ninaifanya nchi yangu yote iwe wazi kwako"

Kaa mahali utakapopendezewa

"ishi popote upendapo"

elfu

"1,000"

ni kwa ajili ya kufunika kosa lolote dhidi yako machoni pa wote walio pamoja na wewe

Kutoa fedha kuthibitisha kwa wengine ya kwamba Sara hana hatia inazungumzwa kana kwamba anaweka mfuniko juu ya kosa ili mwingine asilione. "Ninampatia hili kwake, ili kwamba wale ulionao wajue haujafanya kosa"

machoni

Hapa "macho" ina maana ya mawazo na fikra za mtu.

mbele ya kila mtu ambaye umemfanya kuwa na haki

Msemo huu wa "umemfanya kuwa na haki" unaweza kuwa katika hali ya kutenda. "kila mtu atajua ya kwamba huna hatia"

Genesis 20:17

tasa kabisa

"kutoweza kupata watoto kabisa"

kwa sababu ya Sara, mke wa Abraham

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu Abimeleki alimchukua mke wa Abrahamu Sara"