Genesis 45

Genesis 45:1

hakuweza kujizuia mwenyewe

Hii ina maana hakuweza kuzuia hisia zake. Inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "alikuwa akitaka kuanza kulia"

kando yake

"karibu naye"

nyumba ya Farao

Hapa "nyumba" ina maana ya watu katika kasri ya Farao. "kila mtu ndani ya kasri ya Farao"

walitishwa na uwepo wake

"walimuogopa"

Genesis 45:4

mliyemwuza Misri

Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "ambaye mlimuuza kama mtumwa kwa wafanyabiashara walionileta huku Misri"

msihuzunike

"msihuzunike" au "msiteseke"

mliniuza huku

Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "ya kwamba mliniuza kama mtumwa na kunituma huku Misri"

kutunza uhai

Hapa "uhai" ina maana ya watu ambao Yusufu aliwaokoa na kifo wakati wa njaa. "Ili niweze kuokoa maisha ya wengi"

bado kuna miaka mitano ambayo hakutakuwa na kulima wala kuvuna.

"kutakuwa na miaka mitano zaidi bila ya kupanda au kuvuna". Hapa "bila ya kupanda au kuvuna" ina maana ya ukweli kwamba mimea haitaota kwa sababu ya ukame. "na njaa itadumu kwa miaka mitano zaidi"

Genesis 45:7

kuwahifadhi kama masalia duniani

"ili kwamba wewe na familia yenu msipotee kutoka duniani" au "kuhakikisha vizazi vyako vinaendelea kuishi"

kuwaweka hai kwa ukombozi mkuu

Nomino inayojitegemea "ukombozi" inaweza kuwekwa kama "kuokoa". "kukuweka hai kwa kuwaokoa kwa njia ya juu"

amenifanya baba kwa Farao

Yusufu kumshauri na kumsaidia Farao inazungumziwa kana kwamba Yusufu alikuwa baba wa Farao. "amenifanya niwe kiongozi kwa Farao" au "amenifanya kuwa mshauri mkuu kwa Farao"

nyumba yake yote

Hapa "nyumba" ina maana ya watu wanaoishi ndani ya kasri yake. "miongoni mwa nyumba yake yote" au "kati ya wote wa kasri yake"

mtawala wa nchi yote ya Misri

Hapa "nchi" ina maana ya watu. "mtawala juu ya watu wote wa Misri"

mtawala

Hapa Yusufu anamanisha ya kwamba yeye ni mtawala katika nafasi ya pili kutoka kwa Farao, mfalme wa Misri. Taarifa hii inayoeleweka inaweza kuwekwa wazi.

Genesis 45:9

mwende kwa baba yangu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri. "kurudi kwa baba yangu"

mmwambie, 'Hivi ndivyo asemavyo Yusufu mwanao, "Mungu amenifanya ... yote uliyonayo

Hii ni nukuu yenye madaraja matatu. Inaweza kurahisishwa katika madaraja mawili. "muambieni ya kwamba hivi ndivyo nilivyosema: "Mungu amenifanya ... yote uliyonayo"

Shuka kwangu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri. "Njooni hapa kwangu"

ukaingia katika uhitaji

Hii inazungumzia kuhusu "uhitaji" kana kwamba ilikuwa kikomo cha safari. "kupotea bure" au "kushinda njaa"

Genesis 45:12

macho yenu yanaona, na macho ya Benjamini ndugu yangu

Neno "macho" ina maana ya mtu mzima. "Nyie wote na Benyamini mnaweza kuona"

kwamba ni kinywa changu kinachoongea nanyi

Neno "kinywa" ina maana ya mtu mzima. "ya kwamba mimi, Yusufu, nazungumza na nyinyi"

juu ya heshima yangu yote huku Misri

"jinsi watu wa Misri wanavyoniheshimu sana"

baba yangu huku chini

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri. "baba yangu huku kwangu"

Genesis 45:14

Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shingoni mwake

"Yusufu alimkumbatia ndugu yake Benyamini, na wote wakalia"

Akawabusu ndugu zake wote

Katika kipindi cha zamani cha Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimia jamaa kwa busu.

kulia kwa ajili yao

Hii ina maana ya Yusufu alilia alipowabusu.

Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye

Awali walikuwa na hofu juu yake. Sasa walijisikia wanaweza kuongea naye kwa uhuru. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Baada ya hapo ndugu zake waliongea naye kwa uhuru"

Genesis 45:16

Habari ya jambo hili ikasemwa katika nyumba ya Farao: "Ndugu zake Yusufu wamekuja"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. Pia hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kila mtu katika kasri ya Farao alisikia ya kwamba ndugu zake Yusufu walikuja"

nyumba ya Farao

Hii ina maana ya kasri ya Farao

Wambie ndugu zako, 'Fanyeni hivi: Wapakieni wanyama wenu na mwende katika nchi ya Kanaani. Mchukueni baba yenu na nyumba zenu mnijie. Nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Waambie ndugu zako kupakiza wanyama wao na kwenda Kaanani kumfuata baba yao na familia zao. Waambie waje hapa, nami nitawapa ardhi nzuri katika Misri na chakula bora tunachoweza kutoa"

nitawapa mema ya nchi ya Misri

"Nitawapa sehemu bora ya nchi ya Misri"

mtakula unono wa nchi

Chakula bora ambacho nchi huzaa inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni sehemu nene ya nchi. "utakula chakula bora katika nchi"

Genesis 45:19

Maelezo ya Jumla

Farao anaendelea kumwambia Yusufu kipi cha kuwaambia ndugu zake.

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja. Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "pia waambie kuchukua mikokoteni kutoka katika nchi ya Misri kwa ajili ya watoto na wake zao, na kumchukua baba yao aje hapa. Hawatakiwi kuwa na wasiwasi kuhusu kuleta mali zao, kwa maana nitawapatia mambo mazuri tuliyonayo ndani ya Misri"

mmeamriwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nami nakuamuru kuwaambia" au "pia waambie"

chukueni mikokoteni

"Mikokoteni" ni gari dogo la abiria na mizigo lenye magurudumu mawili au manne. Wanyama huvuta mikokoteni.

Genesis 45:21

na akawapa mahitaji ya safari

"na kuwapa walichohitaji kwa ajili ya safari yao"

Akawapa wote mavazi ya kubadilisha

Kila mtu alipokea idadi ya nguo mbili isipokuwa kwa Benyamini aliyepokea idadi ya nguo tano.

vipande mia tatu

"vipande 300"

punda kumi ... punda majike kumi

Punda walijumlishwa kama sehemu ya zawadi.

Genesis 45:24

msijemkagombana

Maana zaweza kuwa 1) "msibishane" na 2) "msiwe na hofu"

Wakapanda kutoka Misri

Ilikuwa kawaida kutumia neno "panda" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

ndiye mtawala juu ya nchi yote ya Misri

Hapa "nchi ya Misri" ina maana ya watu wa Misri. "anatawala watu wote wa Misri"

moyo wake ulishikwa na mshangao

Hapa "moyo" ina maana ya mtu mzima. "na alishtuka" au "na alishangazwa sana"

hakuwaamini walichomuambia

"hakupokea kile walichosema kilikuwa ni cha kweli"

Genesis 45:27

Wakamwambia

"Wakamwambia Yakobo"

maneno yote ya Yusufu aliyokuwa amewaambia

Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "kila kitu ambacho Yusufu alikisema kwao"

roho ya Yakobo baba yao ikafufuka

Neno la "roho" lina maana ya mtu mzima. "Yakobo baba yao alipona" au "Yakobo baba yao akawa na furaha sana"