Genesis 43

Genesis 43:1

Njaa ilikuwa kali katika nchi

Neno "Kaanani" linaeleweka. Taarifa hii inaweza kuwekwa wazi. "Njaa ilikuwa kali katika nchi ya Kaanani"

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

walipokuwa wametumia chakula

"Yakobo na familia yake walipokuwa wamekula"

walichokitoa

"wana wakubwa wa Yakobo walileta"

mtununulie

Hapa "mtununulie" ina maana ya Yakobo, wanawe, na familia yake iliyobaki.

Genesis 43:3

Yuda akamwambia

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"

Yule mtu

Hii ina maana ya Yusufu, lakini ndugu hawakujua alikuwa Yusufu. Walimtaja kama "mtu" au "yule mtu, bwana wa nchi" kama katika 42:29.

alituonya, "Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"

alituonya kwa ukali

"alikuwa na hali ya ukali alipotuonya, akisema"

Hamtauona uso wangu

Yuda anatumia msemo huu mara mbili katika 43:3-5 kuweka msisitizo kwa baba yake ya kwamba hawawezi kurudi Misri bila Benyamni. Msemo "uso wangu" una maana ya yule mtu, ambaye ni Yusufu. "Hamtaniona"

ndugu yenu awe nanyi

Yuda ana maana ya Benyamini, mtoto wa Raheli wa mwisho kabla yeye hajafa.

hatutashuka

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.

Genesis 43:6

Kwa nini mlinitendea mimi vibaya hivyo

"Kwa nini mlinisababishia matatizo makubwa hivi"

Yule mtu alituuliza habari zetu

"Yule mtu aliuliza maswali mengi"

juu yetu

Hapa "yetu" inajitegemea na ina maana ya ndugu waliokwenda Misri na kuzungumza na"yule mtu".

Akasema, 'Je baba yenu bado yuko hai? Je mnaye ndugu mwingine?

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Alituuliza kwa kuzunguka kama baba yetu alikuwa bado yu hai na kama tuna ndugu mwingine".

Tukamjibu kulingana na maswali haya

"Tulimjibu maswali aliyotuuliza"

Tungejuaje kwamba angetwambia, 'Mleteni ndugu yenu

Wana hawa wanatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hawakujua ni kitu gani yule mtu angewaambia kufanya. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hatukujua ya kwamba angetuambia ... chini!"

angetwambia, 'Mleteni ndugu yenu?"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "angetuambia kumfuata ndugu yetu huku chini Misri"

Mleteni ndugu yenu chini

Ilikuwa kawaida kutumia neno la "chini" katika kuzungumzia safari ya kutoka Kanaani kwenda Misri.

Genesis 43:8

Tutainuka na kwenda ili kwamba tuishi tusife, wote sisi, wewe, na hata watoto wetu

Misemo hii "ili kwamba tuishi" pamoja na "tusife" ina maana moja. Yuda anaweka msisitizo ya kwamba wanalazimu kununua chakula Misri ili kwamba waishi. "Tutakwenda Misri na kupata nafaka ili familia yetu yote iweze kuishi"

Tutainuka

Hapa "tutainuka" ina maana ya ndugu ambao watasafiri kwenda Misri.

ili kwamba tuishi

Hapa "tuishi" ina maana ya ndugu, Israeli na familia nzima.

wote sisi

Hapa "sisi" ina maana ya hawa ndugu.

sisi, wewe

Hapa "wewe" ni umoja na ina maana ya Israeli.

na hata watoto wetu

Hapa "wetu" ina maana ya hawa ndugu. Hii ina maana ya watoto wadogo ambao wangeweza kufa katika kipindi cha njaa.

Mimi nitakuwa mdhamini wake

Nomino inayojitegemea "mdhamini" inaweza kuwekwa kama kitenzi "ahidi". "Ninaahidi kumrudisha"

Utaniwajibisha mimi

Jinsi ambavyo Yakobo atamuwajibisha Yuda inaweza kuwekwa wazi. "Utanifanya niwajibike kwako kuhusu kitakachotokea kwa Benyamini"

basi nibebe lawama

Hii inazungumzia kuhusu "lawama" kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kubeba. "Unaweza kunilaumu"

Kwani kama tusingekawia

Yuda anaelezea jambo ambalo lingetokea hapo nyuma lakini halikutokea. Yuda anamkaripia baba yake kwa kusubiri muda mrefu sana kuwatuma wanawe Misri kufuata chakula zaidi.

tungekuwa tumekwisha rudi mara ya pili

"tungekuwa tumerudi mara mbili"

Genesis 43:11

Kama ni hivyo, basi fanyeni hivi

"Iwapo huu ni uchaguzi wetu pekee, basi fanyeni"

Mchukulieni

Ilikuwa kawaida kutumia neno "chini" katika kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.

malhamu

kitu chenye mafuta chenye harufu tamu kinachotumiwa kwa ajiliya kuponya na kulinda ngozi. "dawa"

viungo

vikolezo

jozi

karanga ndogo, itokayo kwenye mti wa kijani

lozi

karanga ya mti yenye ladha tamu

Chukueni pesa mara mbili mikononi mwenu

Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. "Chukua mara mbili ya pesa pamoja nawe"

Pesa iliyorudishwa katika magunia yenu, muichukue tena katika mikono yenu

Hapa "mikononi" ina maana ya mtu mzima. Msemo wa "iliyorudishwa" unaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "pesa iliyowekwa kwenye magunia yenu na mtu, muirudishe Misri"

Genesis 43:13

Mchukueni ndugu yenu pia

"Mchukueni pia Benyamini"

mwende tena

"mrudi"

Mungu Mwenyezi na awape kuona rehema mbele ya huyo mtu

Nomino inayojitegemea "rehema" inaweza kuwekwa kama kivumishi "huruma". "Mungu mwenye uwezo asababishe yule mtuawe na huruma kwenu"

ndugu yenu mwingine

"Simoni"

Kama nikipotelewa na watoto, nimepotelewa

"Kama nikipoteza watoto wangu, basi nipoteze watoto wangu". Hii ina maana ya kwamba Yakobo anajua inapaswa akubali kitakachotokea kwa watoto wake.

mikono yao wakachukua

Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Wakachukua"

wakashuka Misri

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

Genesis 43:16

Benjamini akiwa nao

"Benyamini pamoja na ndugu wa Yusufu wakubwa"

mtunzaji wa nyumba yake

"Mtunzaji" aliwajibika na kusimamia matukio ya nyumba ya Yusufu.

Akawaleta wale watu

Hapa "akawaleta" inaweza kutafsiriwa kama "kuwachukua"

nyumbani kwa Yusufu

"ndani ya nyumba ya Yusufu"

Genesis 43:18

Wale ndugu wakaogopa

"Ndugu wa Yusufu waliogopa"

walivyoletwa katika nyumba ya Yusufu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "walikwenda ndani ya nyumba ya Yusufu" au "mtunzaji aliwapeleka ndani ya nyumba ya Yusufu"

Ni kwa sababu ya pesa iliyorudishwa katika magunia yetu mara ya kwanza tulipoletwa ndani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtunzaji anatuleta ndani ya nyumba kwa sababu ya pesa ambayo mtu alirudisha ndani ya magunia yetu"

kwamba atafute nafasi kinyume chetu. Kwamba aweze kutukamata

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Anasubiria nafasi ya kutushtaki, ili kwamba aweze kutukamata"

tulikuja

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

Genesis 43:21

Kauli Kiunganishi:

Ndugu wanaendelea kuzungumza na mtunzaji wa nyumba.

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio muhimu la simulizi.

tulipofika katika eneo la kupumzikia

"tulipofika mahali ambapo tulikwenda kukaa usiku ule"

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba ndugu walishangazwa kwa kile walichokiona.

pesa ya kila mtu ilikuwa katika gunia lake, pesa yetu kwa kiasi kamili

"kila mmoja wetu alikuta pesa kamili katika gunia lake"

Tumeileta katika mikono yetu.

Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Tumerudisha pesa pamoja nasi"

Tumekuja na pesa nyingine pia mikononi mwetu ili kununua chakula

Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Tumekuja na pesa zaidi pia kununua chakula zaidi"

Tumekuja na

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

Amani iwe kwenu

Nomino inayojitegemea "Amani" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "Tulia" au "Tulieni"

Mungu wenu na Mungu wa baba yenu

Mtunzaji hazungumzi kuhusu Mungu wawili tofauti. "Mungu wenu, Mungu ambaye baba yenu anamwabudu"

Genesis 43:24

wakaosha miguu yao

Utamaduni huu ulisaidia wasafiri waliochoka kujiburudisha baada ya kutembea umbali mrefu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Akawalisha punda wao

"malisho" ni chakula kilichokauka ambacho huwekwa kando kwa ajili ya wanyama.

Genesis 43:26

wakaleta nyumbani zawadi iliyokuwa mikononi mwao

Hapa "mikononi" ina maana ya mtu mzima. "ndugu hawa walileta zawadi ambazo walikuwa nazo"

wakainama mbele yake

Hii ni njia ya kuonyesha heshima na taadhima.

Genesis 43:28

Mtumishi wako baba yetu

Walimuelezea baba yao kama "Mtumishi wako" kuonyesha heshima. "Baba yetu anayekutumikia"

Wakajinyenyekeza na kuinama chini

Maneno haya yana maana moja. Walilala chini mbele ya yule mtu kumuonyesha heshima. "Waliinama chini mbele yake"

Alipoinua macho yake

Hii ina maana "alitazama juu"

mwana wa mamaye, naye akasema

Hii inaweza kutafsiriwa na sentensi mpya. "mwana wa mamaye. Yusufu akamwambia"

Je huyu ndiye mdogo wenu ... mliyemsema?

Maana zaweza kuwa 1) Yusufu anauliza kwa dhati swali kupata uthibitisho ya kwamba mtu huyu ni Benyamini, au 2) ni swali la balagha. "Kwa hiyo huyu ndiye ndugu yenu mdogo ... mliyesema?"

mwanangu

Hii ni njia ya kirafiki mtu huzungumza kwa mtu mwingine wa cheo cha chini. "kijana"

Genesis 43:30

akaharakisha kutoka chumbani

"aliharakisha nje ya chumba"

kwani aliguswa sana kuhusu nduguye

Msemo "aliguswa sana" una maana ya kuwa na huruma kubwa au hisia ambapo jambo muhimu hutokea. "kwa maana alipatwa na hisia kali za huruma kwa nduguye" au "kwa maana akawa na hisia za upendo kwa ndugu yake"

akasema

Inaweza kuwekwa wazi ni kwa nani Yusufu anazungumza. "na akasema kwa watumishi wake"

karibuni chakula

Hii ina maana ya kusambaza chakula ili kila mtu aweze kula.

Genesis 43:32

Watumishi wakamhudumia Yusufu peke yake na wale ndugu peke yao. Wamisri pale wakala pamoja naye peke yao

Hii ina maana ya kwamba Yusufu, ndugu zake, na Wamisri wengine wanakula katika sehemu tatu tofauti ndani ya chumba kimoja. "Watumishi walimhudumia Yusufu peke yake na ndugu zake peke yao na Wamisri, ambao walikuwa wakila naye, peke yao"

Wamisri pale wakala pamoja naye peke yao

Inawezekana hawa ni maafisa Wamisri wengine ambao walikula pamoja na Yusufu, lakini bado waliketi tofauti kutoka kwake na ndugu zake wa Kiebrania.

kwa sababu Wamisri hawakuweza kula mkate na Waebrania, kwani hilo ni chukizo kwa Wamisri

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Walifanya hivi kwa sababu Wamisri walidhani ilikuwa aibu kula pamoja na Waebrania"

hawakuweza kula mkate

Hapa "mkate" ina maana ya chakula kwa ujumla.

Wale ndugu wakakaa mbele yake

Inasemekana ya kwamba Yusufu alipanga ni wapi kila ndugu angeketi. Unaweza kuweka wazi taarifa iliyodokezwa. "Ndugu walikaa upande wa pili na yule mtu, kulingana na jinsi alivyopanga nafasi zao"

mzaliwa wa kwanza kwa kulingana na haki yake ya uzaliwa, na mdogo kulingana na ujana wake

"mzaliwa wa kwanza" na "mdogo kuliko wote" inatumika pamoja kumaanisha ya kwamba ndugu wote walikaa kulingana na umri wao.

Wale watu wakashangaa wote

"Hawa watu walishangazwa walipogundua hili"

Lakini sehemu ya Benjamini ilikuwa mara tano zaidi ya kila ndugu zake

Msemo "mara tano" unaweza kuwekwa kwa ujumla zaidi. "Lakini Benyamini alipokea sehemu ambayo ilikuwa kubwa zaidi ya kile walichopokea ndugu zake"