Genesis 40

Genesis 40:1

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio jipya la simulizi.

mnyweshaji

Huyu ni mtu ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.

mwokaji wa mfalime

Huyu ni mtu ambaye alitengeneza chakula cha mfalme.

walimkosa bwana wao

"walimkwaza bwana wao"

maafsa wawili, mkuu wa wanyweshaji na mkuu wa waokaji

""mnyweshaji kiongozi na mwokaji kiongozi"

Akawaweka katika lindo katika nyumba ya kapteni wa walinzi

"Akawaweka katika gereza liliokuwa katika nyumba ambayo ilisimamiwa na kapteni wa walinzi"

Akawaweka

Mflame hakuwaweka gerezani lakini aliwaamuru wafungwe. "Akafanya wawekwe" au "Aliamuru walinzi wake kuwaweka"

katika gereza lile Yusufu alimofungwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hili lilikuwa gereza lile lile ambalo Yusufu alikuwemo" au "Hili lilikuwa gereza lile lile ambalo Potifa alimweka Yusufu"

Genesis 40:4

Walikaa kifungoni kwa muda fulani

"Walikaa kifungoni kwa muda mrefu"

Genesis 40:6

Yusufu akaja kwao

"Yusufu akaja kwa mnyweshaji na mwokaji"

Tazama, walikuwa na uzuni

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yusufu alishangazwa na kile alichokiona. "Alishangazwa kuona ya kuwa walikuwa na huzuni"

maafsa wa Farao waliokuwa pamoja naye

Hii ina maana ya mnyweshaji na mwokaji"

kifungoni katika nyumba ya bwana wake

"Gerezani katika nyumba ya bwana wake". "Bwana wake" ina maana ya bwana wa Yusufu, kapteni wa walinzi.

Je tafsiri haitoki kwa Mungu?

Yusufu anatumia swali kuonyesha msisitizo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "tafsiri ni za Mungu!" au "Ni Mungu ambaye anaweza kusema maana ya ndoto!"

Niambieni, tafadhari

Yusufu anawaomba wamumbie ndoto zao. "Tafadhali niambieni ndoto"

Genesis 40:9

Mkuu wa wanyweshaji

Mtu muhimu zaidi ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.

Katika ndoto yangu, tazama, kulikuwa na mzabibu mbele yangu

"Katika ndoto yangu, tazama, kulikuwa na mzabibu mbele yangu!" Mnyweshaji anatumia neno "tazama" hapa kuonyesha ya kwamba alishangazwa kwa kile alichokiona katika ndoto yake na kumuamsha Yusufu avute nadhari.

kuzaa vichala vya zabibu

"vichala vyake vikaiva kuwa zabibu"

kuzikamua

Hii ina maana ya kwamba alikamua juisi kutoka kwao. "akakamua juisi kutoka kwao"

Genesis 40:12

Tafsiri yake ni hii

"Hivi ndivyo ndoto inavyomaanisha"

Yale matawi matatu ni siku tatu

"Matawi matatu yanawakilisha siku tatu"

Ndani ya siku tatu

"Katika siku tatu zaidi"

atakiinua kichwa chako

Hapa Yusufu anaongea na Farao kumuachia mnyweshaji kutoka gerezani kana kwamba Farao alisababisha yeye kuinua kichwa chake. "atakuachia kutoka gerezani"

kukurudisha katika nafasi yako

"atakurudishia kazi yako"

kama ulivyokuwa

Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. "kama ulivyofanya ulipokuwa"

Genesis 40:14

unionesha wema

"na tafadhali unioneshe wema kwangu"

Unitaje kwa Farao na kuniondoa hapa gerezani

Yusufu ana maana ya mnyweshaji kumwambia Farao juu yake ili kwamba Farao amfungulie kutoka gerezani. "Nisaidie kutoka katika gereza hili kwa kumwambia Farao juu yangu"

Maana hakika nilitekwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Maana hakika watu walinichukua" au "Maana hakika Waishmaeli walinichukua"

nchi ya Waebrania

"nchi ambayo Waebrania huishi"

hapa sijafanya chochote kinachonipasa niwekwe gerezani

"na pia nilipokuwa hapa Misri, sijafanya jambo lolote ambalo nastahili kuwekwa gerezani"

Genesis 40:16

Mkuu wa waokaji

Hii ina maana ya mtu kiongozi aliyetengeneza chakula cha mfalme.

Mimi pia niliota ndoto, na

"Mimi pia nilipata ndoto, na ndani ya ndoto yangu"

tazama, vikapu vitatu vya mikate vilikuwa juu ya kichwa changu

"kulikuwa na vikapu vitatu vya mikate juu ya kichwa changu!" Mwokaji anatumia neno "tazama" hapa kuonyesha ya kwamba alishangazwa kwa kile alichokiona ndani ya ndoto yake na kumuamsha Yusufu kuvuta nadhari.

bidhaa ya kuokwa kwa Farao

"alioka vyakula kwa ajili ya Farao"

Genesis 40:18

Tafsiri ni hii

"Hii ndio maana ya ndoto"

Vikapu vitatu ni siku tatu

"Vikapu vitatu vinawakilisha siku tatu"

atakiinua kichwa chako kutoka kwako

Yusufu pia alitumia msemo huu "atainua kichwa chako" alipoongea kwa mnyweshaji katika 40:12. Hapa ina maana tofauti. Maana zaweza kuwa 1) "atainua kichwa chako na kuweka kamba katika shingo yako" au 2) "atainua kichwa chako kukikata"

mwili

Hapa "mwili" una maana ya sehemu laini katika mwili wa mtu.

Genesis 40:20

Ikawa

"Hapo baadae, katika siku ya tatu". msemo "ikawa" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio jipya katika simulizi.

Akafanya sherehe

"Akawa na sherehe"

mkuu wa wanyweshaji

Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa na kuhudumia vinywaji kwa mfalme.

mkuu wa waokaji

Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa chakula kwa ajili ya mfalme.

Akamrudisha mkuu wa wanyweshaji katika majukumu yake

"majukumu" wa mkuu wa wanyweshaji una maana ya kazi yake kama mkuu wa manyweshaji. "Alimrudishia mkuu wa wanyweshaji kazi yake"

Lakini akamtundika mkuu wa waokaji

Farao hakumnyonga mwokaji yeye binafsi, ila aliaamuru anyongwe. "Lakini aliamuru mkuu wa waokaji anyongwe" au "Lakini aliamuru walinzi wake kumnyonga mkuu wa waokaji"

kama Yusufu alivyokuwa amewatafsiria

Hii ina maana ya pale ambapo Yusufu alitafsiri ndoto zao. "kama vile Yusufu alivyosema kingetokea pale alipotafsiri ndoto za wanamume wale wawili"