Genesis 38

Genesis 38:1

Ikawa wakati ule Yuda

Hii inatambulisha sehemu mpya ya simulizi ambayo inamlenga Yuda.

Mwadulami fulani, jina lake Hira

Hira ni jina la mwanamume aliyeishi Adulami. Mwadulami ni utaifa wake.

jina lake Shua

Shua ni mwanamke wa Kaanani aliyeolewa na Yuda.

Genesis 38:3

Akawa mjamzito

"mke wa Yuda akawa mjamzito"

Akaitwa Eri

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Baba yake akamuita Eri"

Eri ... Onani ... Shela

Haya ni majina ya wana wa Yuda.

akamwita jina lake

"akamwita"

Kezibu

Hili ni jina la mahali.

Genesis 38:6

Eri

Hili ni jina la mmoja wa watoto wa Yuda.

alikuwa mwovu machoni pa Yahwe

Msemo "machoni pa" una maana ya yahwe kuona uovu wa Eri.. "alikuwa muovu na Yahwe akauona"

Yahwe akamwua

Yahwe akamuua kwa sababu alikuwa muovu. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Kwa hiyo Yahwe akamuua"

Genesis 38:8

Onani

Hili ni jina la mmoja wa watoto wa Yuda.

Fanya wajibu wa shemeji kwake

shemeji kwake - Hii ina maana ya utamaduni ambao mwana mkubwa anapofariki kabla yeye na mkewe kupata mwana, ndugu anayefuata kiumri angemuoa na kulala na mjane. Mjane atakapozaa mwana wa kwanza, mtoto yule alijulikana kuwa mwana wa ndugu wa kwanza na angepokea urithi wa kaka wa kwaza.

lilikuwa ovu mbele za Yahwe

Msemo huu "machoni pa" una maana ya Yahwe kuona uovu wa Onani. "alikuwa muovu na Yahwe aliuona"

Yahwe akamwua pia

Yahwe akamuua kwa sababu alichofanya kilikuwa kiovu. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Kwa hiyo Yahwe akamuua pia"

Genesis 38:11

mkwewe

mkwewe - "mke wa mwanawe mkubwa"

katika nyumba ya baba yako

Hii ina maana ya yeye kuishi katika nyumba ya baba yake. "na kuishi katika nyumba ya baba yako"

hadi Shela, mwanangu, atakapokuwa

Yuda anakusudia kwa Tamari kuja mumuoa Shela atakapokua mkubwa. "na pale ambapo Shela, mwanangu, atakapokua, ataweza kukuoa"

Shela

Hili ni jina la mmoja wa wana wa Yuda.

Kwani aliogopa, "Asije akafa pia, kama nduguze

Yuda aliogopa ya kwamba iwapo Shela atamuoa Tamari angekufa pia kama kaka zake walivyokufa. "Kwa maana alihofia, 'akimuoa na yeye angeweza kufa kama kaka zake walivyokufa"

Genesis 38:12

Shua

Hili ni jina la mwanamume.

Yuda akafarijika na

"Yuda alipokuwa haombolezi, ali"

wakatao kondoo wake manyoya huko Timna

"Timna, ambapo wanamume wake walikuwa wakinyoa manyoya ya kondoo"

Timna ... Enaimu

Haya ni majina ya mahali.

yeye na rafiki yake, Hira Mwadulami

"Rafiki yake Hirami, kutoka Adulami, alikwenda naye"

Hira Mwadulami

"Hira" ni jina la mwanamume, na "Adulami" ni jina la kijiji ambapo aliishi.

Tamari akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu akamwambia Tamari"

Tazama, mkweo

mkweo - "Sikiliza". Hapa neno "tazama" linatumika kushika nadhari ya Tamari.

mkweo

mkweo - "baba wa mume wako"

ya ujane

"ambayo wajane huvaa"

ushungi

kitambaa chembamba sana kinachotumika kufunika kichwa na uso wa mwanamke.

na akajifunika

Hii ina maana alijificha kwa nguo yake ili kwamba watu wasiweze kumtambua. Kitamaduni, sehemu za nguo za wanawake zilikuwa kubwa walizojizungushia nazo. "na akajifunika na kitambaa chake ili watu wasiweze kumtambua"

kando ya njia

"kando ya barabara" au "njiani"

hakupewa kuwa mke wake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yuda hakupatiwa kwa Shela kuwa mke"

Genesis 38:15

kwa maana alikuwa amefunika uso wake

Yuda hakufikiria ya kwamba alikuwa kahaba kwa sababu tu alifunika uso wake lakini pia kwa sababu alikuwa amekaa langoni. "kwa sababu alikuwa amefunika kichwa chake na kukaa mahali makahaba hukaa mara kwa mara"

Akamwendea kando ya njia

Tamari alikuwa amekaa kando ya njia. "Alikwenda mahali alipokuwa amekaa kando na njia"

Njoo

"Njoo kwangu" au "Njoo sasa"

Yuda alipomwona

"Yuda alipomwona Tamari"

mkwewe

mkwewe - "mke wa mwanawe"

Genesis 38:17

kutoka kwa kundi

"kutoka kwa kundi la mbuzi wangu"

Mhuri wako na mshipi ... fimbo

"Mhuri" ni sawa na sarafu yenye mchoro uliochongwa juu yake, unaotumika kuchapa nta iliyoyeyushwa. "Mshipi" uliwekwa katika mhuri ili kwamba mmiliki angeweza kuvaa shingoni mwake. Fimbo ilikuwa mti mrefu wa mbao uliosaidia kutembea juu ya ardhi ngumu.

Akawa na uja uzito wake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alimsababisha aweze kupata mimba"

Genesis 38:19

ushungi

kitambaa chembamba sana kinachotumika kufunika kichwa na uso wa mwanamke.

vazi la ujane wake

"ambayo wajane huvaa"

kutoka kundini

"kutoka katika kundi lake"

Mwadulami

"Adulami" ni jina la kijiji ambapo Hiramu aliishi.

aichukue rehani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "chukua rehani"

kutoka katika mkono wa mwanamke

Hapa "mkono" unasisitiza ya kwamba vilikuwa katika umiliki wake. Mkono wa mwanamke una maana ya mwanamke. "kutoka kwa mwanamke"

Genesis 38:21

Mwadulami

"Adulami" ni jina la kijiji ambapo Hiramu aliishi.

watu wa sehemu

"baadhi ya wanamume ambao waliishi pale"

kahaba wa kidini

"kahaba aliyetumika katika hekalu"

Enaimu

Hili ni jina la mahali.

tusije tukaaibika

Watu wangekuja kugundua kilichotokea wangemkejeli Yuda na kumcheka. Hii inaweza kuwekwa wazi na kusemwa katika hali ya kutenda. "la sivyo watu watatucheka wakigundua kilichotokea"

Genesis 38:24

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Yuda akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu akamwambia Yuda"

Tamari mkweo

mkweo - "Tamari, mke wa mwana wako mkubwa"

yeye ni mjamzito kwa tendo hilo

Hapa neno la "hilo" lina maana ya "ukahaba" alioufanya. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "limemfanya aweze kuwa na mimba" au "ana mimba"

Mleteni hapa

"Mleteni nje"

ili achomwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "tutamchoma mpaka kufa"

Alipoletwa nje

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walipomleta nje"

mkwewe

mkwewe - "baba wa mume wake"

mhuri huu na mshipi na fimbo

"Mhuri" ni sawa na sarafu yenye mchoro uliochongwa juu yake, unaotumika kuchapa nta iliyoyeyushwa. "Mshipi" uliwekwa katika mhuri ili kwamba mmiliki angeweza kuvaa shingoni mwake. Fimbo ilikuwa mti mrefu wa mbao uliosaidia kutembea juu ya ardhi ngumu.

Shela

Haya ni majina ya wana wa Yuda.

Genesis 38:27

Muda ukafika

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

tazama

Neno "tazama" linatuamsha kwa mshtuko ya kwamba Tamari alikuwa amebeba mapacha, ambayo haikujulikana awali.

Muda wake wa kujifungua ukafika

Msemo huu "ukafika" unaweka alama kwa tukio muhimu katika simulizi.

mmoja akatoa mkono

"mmoja wa watoto akatoa mkono wake nje"

mkunga

Huyu ni mtu ambaye humsaidia mwanamke anayezaa mtoto.

kitambaa cha rangi ya zambarau

"kitambaa cha rangi nyekundu iliyoiva"

katika mkono wake

"kuzunguka kifundo cha mkono wake"

Genesis 38:29

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza inayofuata.

Umetokaje

Hii inaonyesha mshangao wa mkunga kuona mtoto wa pili akitoka kwanza. "Kwa hiyo hivi ndivyo unavyojitokeza kwanza!" au "Umejitokeza nje kwanza!"

akaitwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "akamuita"

Peresi

Hili ni jina la mtoto wa kiume. "Jina la Peresi lina maana ya "kuvunja nje".

Zera

Hili ni jina la mtoto wa kiume. "Jina la Zera lina maana ya "kitambaa cha rangi nyekundu".