Genesis 7

Genesis 7:1

Taarifa ya jumla:

Matukio ya sura hii yanatokea baadaya Nuhu kujenga safina, kukusanya chakula, na kukiweka ndani ya safina.

Njoo ...katika safina ...utakuja nao

"Ingia ... ndani ya safina .. chukua". Tafsiri nyingi husema "Nenda .. ndani ya safina .. chukua"

wewe

Neno hapa "wewe" linamaana ya Nuhu la lipo katika umoja.

nyumba yako

"familia yako"

mwenye haki mbele yangu

Hii inamaana ya kwamba Mungu alimwona Nuhu kuwa mwenye haki.

katika kizazi hiki

Hii inamaana ya watu wote ambao walikuwa wakiishi katika muda huo. "Kati ya watu wote wanaoishi sasa"

mnyama aliye safi

Huyu alikuwa ni myama ambaye Mungu aliruhusu watu wake wamle na kutoa sadaka.

wanyama wasio safi

Hawa ni wanyama ambao Mungu hakuruhusu watu wale au kutoa sadaka.

kuhifadhi kizazi chao

"ili kwamba waweze kuwa na kizazi kitakachoishi" au "ili kwamba, baada ya gharika, wanyama waendelee kuishi"

Genesis 7:4

siku arobaini mchana na usiku

Hii ilikuwa siku arobaini kamili. Haikuwa jumla ua siku themanini. "siku arobaini mchana na usiku"

hai

Hii inamaana ya uhai wa mwili

Genesis 7:6

Taarifa ya jumla

Mistari ya 6-12 inarudia kwa mara ya pili na kutoa kwa utondoti jinsi gani Nuhu alivyoinbgia ndani ya safina na familia yake pamoja na wanyama katika 7:1. Hili sio tukio jipya.

ilipokuja juu ya nchi

"ilipotokea" au "ikaja juu ya nchi"

kwa sababu ya maji ya gharika

"kwa sababu ya gharika itakayokuja" au "kutoroka maji ya gharika"

Genesis 7:8

Taarifa ya jumla:

Mistari ya 6-12 inarudia kwa mara ya pili na kutoa kwa utondoti jinsi gani Nuhu alivyoinbgia ndani ya safina na familia yake pamoja na wanyama katika 7:1. Hili sio tukio jipya.

Wanyama ambao ni safi

Hawa walikuwa wanyama ambao Mungu aliruhusu watu wake kuwala na kuwatoa kama sadaka kwake.

wanyama ambao si safi

Hawa walikuwa wanyama ambao Mungu hakuruhusu watu wake wale au kuwato kama sadaka kwake.

wawili wawili

Wanyama waliingia kwenye safina katika makundi ya dume mmoja na jike mmoja.

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama kuhusu tukio muhimu katika simulizi hii. Mwanzo wa gharika.

baada ya zile siku saba

"baadaya siku saba" au"siku saba baadaye"

maji ya gharika yakaja juu ya nchi

Habari inayojitokeza, "ikaanza kunyesha" inaweza kufanywa kuwa wazi. "ikaanza kunyesha na maji ya gharika yakaja juu ya nchi"

Genesis 7:11

Taarifa ya jumla:

Mistari ya 6-12 inarudia kwa mara ya pili na kutoa kwa utondoti jinsi gani Nuhu alivyoinbgia ndani ya safina na familia yake pamoja na wanyama katika 7:1. Hili sio tukio jipya.

Katika mwaka wa mia sita wa maisha yake Nuhu

"Nuhu alipokuwa na umri wa miaka 600"

mwezi wa pili, katika siku ya kumi na saba ya mwezi

Kwa kuwa Musa aliandika kitabu hiki, inawezekana inamaanisha mwezi wa pili katika kalenda ya Kiebrania. Lakini hii haina uhakika

katika siku iyo hiyo

Hii ina maana siku bayana ambapo mvua ilianza. Msemo huu unasisitiza jinsi gani matukio yote makubwa yalivyotokea haraka muda ulipowadia.

chemchemi zote za vilindi vikuu zilipasuka na kufunguka

"maji kutoka chini ya ardhi yalifunguka juu kwenye sakafu ya nchi"

vilindi vikuu

Hii ina maana ya bahari ambalo inasadikiwa lilikuwa chini ya ardhi.

madirisha ya mbinguni yakafunguka

Hii ina maana ya mvua. Inaelezea anga kama dari ambalo hutunza maji juu yake kutodondoka ardhini. Madirisha, au milango, ya anga yalipofunguliwa, maji yalifunguka chini kupitia kwao. "anga ikafungua" au "milango ya anga ikafunguka"

mvua

Mvua kubwa

Genesis 7:13

Taarifa ya jumla

Mistari ya 13-18 inarudia kwa mara ya tatu na kutoa kwa undani kuhusu jinsi gani Nuhu aliingia katika safina pamoja na familia yake na wanyama katika 7:1. Hili si tukio jipya.

Katika siku iyo hiyo

"Katika siku hiyo hasa". Hii ina maana ya siku ambayo mvua ilianza kunyesha. Mistari ya 13-16 inaeleza Nuhu alichofanya kabla tu ya mvua kuanza.

mnyama wa mwitu ... mnyama wa kufugwa ... kila kitambaacho ... ndege

Vikundi hivi vinne vinaorodheshwa kuonyesha ya kwamba kila aina ya mnyama alijumuishwa.

kila kitambaacho

Hii ina maana ya wanyama watambaao juu ya ardhi, kama wanyama wagugunaji, wadudu, mjusi na nyoka.

kwa jinsi yake

"ili kwamba kila aina ya mnyama azalishe zaidi ya kila aina yake"

Genesis 7:15

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 13-18 inarudia kwa mara ya tatu na kutoa ufafanuzi zaidi jinsi gani Nuhu aliingia katika safina pamoja na familia yake na wanyama. Hili sio tukio.

Viwili viwili katika kila chenye mwili

Hapa "mwili" inawakilisha wanyama.

ambacho kilikuwa na pumzi ya uhai

Hapa "pumzi" inawakilisha uhai. "alivyoishi"

kilikuja kwa Nuhu

Neno "kilikuja" linaweza kutafsiriwa kama "alikwenda".

wote wenye mwili

Hapa "mwili" inawakilisha wanyama. "katika kila aina ya mnyama"

akawafungia

Maana kamili yaweza kutajwa wazi. "walipoingia ndani ya safina"

Genesis 7:17

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 13-18 inarudia kwa mara ya tatu na kutoa ufafanuzi zaidi jinsi gani Nuhu aliingia katika safina pamoja na familia yake na wanyama. Hili sio tukio.

na maji yakaongezeka

Hii ilitokea katika kipindi cha siku arobaini wakati maji yalipokuwa yakija. "na maji yakawa na kina kirefu sana"

na kuinua safina

"na ikasababisha safina kuelea"

kuinua juu ya nchi

inasababisha safina kuinuka juu ya nchi" au "safina ilielea juu ya maji ya kina kirefu"

Genesis 7:19

Maji yakaongezeka zaidi juu ya nchi

"Maji yalishinda kabisa nchi"

dhiraa kumi na tano

"mita sita"

Genesis 7:21

vilitembea juu

"vilisogea kote kote" au "vilitangatanga"

viumbe hai vyote kwa wingi vilivyoishi juu ya nchi

Hii ina maanisha wanyama wote wanatembea kote kote juu ya nchi kwa makundi makubwa.

vilivyo pumua pumzi ya uhai kwa njia ya pua

Hapa "pua" inawakilisha mnyama mzima au mwanadamu. "kila mtu apumuaye"

pumzi ya uhai

Maneno "pumzi"na "uhai" yanawakilisha nguvu inayosababisha watu na wanadamu kuwa na uhai.

vilikufa

Hii ina maana kifo cha kimwili

Genesis 7:23

Hivyo kila kilichokuwa hai ... kilifutwa

Ikiwezekana, hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa hiyo kila kiumbe hai ... kikatoweka" au "Kwa hiyo gharika iliangamiza kabisa kila kiumbe hai"

Vyote viliangamizwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliwaangamiza wote"

kutoka kwenye nchi

"kwa hiyo hawakuwa katika nchi"

na wale waliokuwa naye

"na watu pamoja na wanyama waliokuwa naye"

walisalia

"walibaki" au "waliishi" au"walibaki hai"

Maji yalitawala nchi

"Maji yenye kina kirefu yalifunika nchi yote" au "Maji yalibaki na gharika kubwa juu ya nchi"