Sura 12

1 Kisha Miriamu na Haroni wakasema kinyume na Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi ambaye alikuwa amemwoa. 2 Walisema. " Hivi BWANA amesema na Musa tu? Ni kweli hajawahi kusema nasi pia? Sasa BWANA akasikia kile walichokuwa wanaongea. Sasa 3 Musa alikuwa mtu mpole sana, mpole kuliko mtu yeyote duniani. 4 Wakati huo, BWANA akanena na Musa, Haroni na Miriamu: "tokeni nje ninyi watatu kwenye hema ya kukutania." kwa hivyo wale watatu wakatoka inje. 5 Kisha BWANA akashuka katika nguzo ya wingu. Akasimama kwenye lango la hema na akamwita Haroni na Miriamu. wote wakaja mbele. 6 BWANA akasema, "Sasa sikilizeni maneno yangu, Nabii wangu anapokuwa nanyi, Mimi nitajifunua kwake kwa maono na kusema naye katika ndoto. 7 Lakini si hivyo kwa mtumishi wangu Musa. Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote. 8 Mimi huongea na Musa moja kwa moja, si kwa maono wala mafumbo. Yeye huniona umbo langu. Kwa hiyo, kwa nini hamuogopi kumnenea kinyume, mtumishi wangu Musa?" 9 Hasira ya BWANA ikawawakia, kisha akawaacha. 10 Lile wingu likainuka juu ya hema, Miriamu akapata ukoma ghafla - akawa mweupe kama theluji. Naye Haroni alipogeuka kumwona Miriamu, akamwona amepata ukoma. 11 Haroni akamwambia Musa, "Bwana wangu, usituadhibu kwa uovu wetu huu. Tumenena katka upumbuvu, na tumetenda dhambi. 12 Tafadhali nakuomba usimwache akawa kama mtoto mchanga aliyekufa ambaye nusu ya nyama yake imeoza tangu kuzaliwa" 13 Kwa hivyo Musa akamwomba BWANA, akasema, "Mungu ninakusihi umponye tafadhali." 14 BWANA akamwambia Musa, " kama baba yake angemtemea mate usoni angepata aibu kwa muda wa siku saba. Umfungie nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Kisha umrejeshe ndani tena." 15 Kwa hivyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba. Watu hawakusafiri mpaka aliporudi kambini. 16 Kisha watu wakasafiri kutoka Hazeroti na kuweka kambi kwenye jangwa la Parani.