Sura 14

1 Yahweh akasema na Musa na kumwambia, 2 "Waambie Waisraeli wageuke na kuweka kambi mbele ya Pi Hahirothi, katikati ya Migdoli na bahari, mbele ya Baali Zefoni. Wapaswa kuweka kambi pembenni ya Pi Hahirothi. 3 Farao atasema kuhusu Waisraeli, 'Wanaangaika kwenye nchi. Nyikani imewafunika.' 4 Nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, na yeye atawakimbiza. Nitapata utukufu kwa sababu ya Farao na jeshi lake lote. Wamisri watajua mimi ni Yahweh." Kisha Waisraeli wakaweka kambi kama walivyo elekezwa. 5 Mfalme wa Misri alipo ambiwa Waisraeli wametoroka, nia ya Farao na watumishi wake ikageuka dhidi ya watu. Wakasema, "Tumefanya nini kwa kuwaacha Waisraeli waende uhuru na wasitutumikie?" 6 Kisha Farao akachukua magari yake ya farasi na jeshi lake. 7 Alichukua magari ya farasi mia sita imara na magari yote ya farasi ya Misri, pamoja na maafisa wa hayo magari. 8 Yahweh akaufanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, na mfalme akawafukuzia Waisraeli. Sasa Waisraeli waliondoka kwa shangwe. 9 Lakini Wamisri wali wafukuzia, pamoja na farasi na magari ya farasi, wapanda farasi, na jeshi lake. Walikuta Waisraeli wameeka kambi pembezoni mwa bahari kati ya Pi Hahirothi na Baali Zefoni. 10 Farao alipo karibia, Waisraeli walitazama juu na kushangaa. Wamisri walikuwa wakija kwao, na waliogopa. Waisraeli walimlilia Yahweh. 11 Walimwambia Musa, "Ni kwasababu hakukuwa na makaburi Misri, hadi umetuleta tufe huku nyikani? Kwanini umetutendea hivi, kwa kututoa Misri? 12 Hili si ndilo tulilo kwambia Misri? Tulikwambia, 'Utuache, ili tuwafanyie Wamisri kazi.' Ingekuwa bora kwetu sisi kuwafanyia kazi kuliko kufa nyikani." 13 Musa akawaambia watu, "Msiogope. Simameni imara na muone wokovu Yahweh atakao uleta kwenu leo. Kwa maana hamtawaona tena Wamisri mnao waona leo. 14 Yahweh atawapigania, na ninyi mtasimama imara." 15 Kisha Yahweh akamwambia Musa, "Kwanini wewe, Musa, unaendelea kuniita mimi? Waambie Waisraeli waendelee mbele. 16 Nyanyua gongo lako juu, nyoosha mkono wako kuelekea baharini na uigawanye sehemu mbili, ili watu wa Israeli wapite baharini kwenye nchi kavu. 17 Jitahadharishe kuwa nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu ili wawafuate. Nitapata utukufu kwasababu ya Farao na jeshi lake lote, magari yake ya farasi, na wapanda farasi. 18 Kisha Wamisri watajua kuwa mimi ni Yahweh nitakapo pata utukufu kwa sababu ya Farao, magari yake na farasi, na wapanda farasi wake." 19 Malaika wa Mungu, aliyeenda mbele ya Waisraeli, aliama na kwenda nyuma yao. Nguzo ya wingu ili sogea mbele yao na kwenda kusimama nyuma yao. 20 Wingu lilikuja katikati ya kambi ya Misri na kambi ya Israeli. Lilikuwa wingu jeusi kwa Wamisri, lakini liliangaza usiku kwa ajili ya Waisraeli, hivyo upande mmoja haukuweza kuja karibu na ya mwingine usiku wote. 21 Musa akanyoosha mkono wake kuelekea bahari. Yahweh akasogeza bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku huo wote na kufanya bahari nchi kavu. Kwa namna hii maji yaligawanyika. 22 Waisraeli walienda katikati ya bahari kwa nchi kavu. Maji yaliunda ukuta mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto. 23 Wamisri wakawafukuzia. Waliwafuata hadi katikati ya bahari - farasi wote wa Farao, magari ya farasi, na wapanda farasi. 24 Lakini masaa ya mapema ya asubui, Yahweh alitazama chini jeshi la Wamisri kupitia nguzo ya moto na wingu. Alisababisha hofu miongoni mwa Wamisri. 25 Magari yao ya farasi yalikuwa yana kwama matairi, na wapanda farasi waliendesha kwa ugumu. Hivyo Wamisri walisema, "Acha tuwakimbie Waisraeli, kwa kuwa Yahweh anawapigania dhidi yetu." 26 Yahweh akamwambia Musa, "Nyoosha mkono kuelekea bahari ili maji yawarudie Wamisri, magari yao ya farasi, na wapanda farasi wao." 27 Hivyo Musa akanyoosha mkono wake kuelekea bahari, na ikarudi kwenye hali yake ya kawaida kulilipo pambazuka. Wamisri walikimbilia ndani ya bahari, na Yahweh akawaingiza Wamisri kati kati yake. 28 Maji yakarudi na kufunika magari ya farasi ya Farao, wapanda farasi, na jeshi lake lote lililo fuata magari ya farasi kwenye bahari. Hakuna aliyepona. 29 Walakini, Waisraeli walitembea kwenye nchi kavu kati kati ya bahari. Maji yalikuwa ukuta kwa mkono wa kulia na mkono wa kushoto. 30 Hivyo Yahweh akaokoa Israeli kutoka kwa mkono wa Wamisri, na Israeli ikaona maiti za Wamisri ufuoni. 31 Israeli ilipoona nguvu kubwa Yahweh aliyo itumia dhidi ya Wamisri, watu walimsifu Yahweh, na kumwamini Yahweh na mtumishi wake Musa.