Sura 25

1 Halafu kwa wakati ule, Ufalme wa mbinguni utafanana na wabinti kumi waliotwaa taa zao na kwenda kumupokea bwana-arusi. 2 Watano kati yao walikuwa wajinga na watano walikuwa wenye akili. 3 Wale wajinga walitwaa taa zao tu, lakini hawakupeleka mafuta ya kutia ndani yao. 4 Lakini wale wenye akili walitwaa machupa ya mafuta pamoja na taa zao. 5 Na kwa kuona bwana-arusi alikawia kufika, wote wakasinzia na kulala usingizi. 6 Ilipokuwa katikati ya usiku, kelele likasikilika, likisema: «Angalia, bwana-arusi anakuja! Muondoke kwenda kumupokea! 7 Halafu wale wabinti kwakatengeneza taa zao. 8 Wale wajinga wakawaambia wenye akili: “Mutusaidie na mafuta kidogo, kwa sababu taa zetu zinaanza kuzimika.” 9 Lakini wale wenye akili wakajibu: “Haiwezekani, mafuta tunayokuwa navyo hayatutoshelei. Afazali muende kwa wachuuzi na kujinunulia yenu.”» umi wakaamuka, 10 Wale wajinga walipokwenda kununua mafuta, bwana-arusi akafika. Wale wenzao watano waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika karamu ya ndoa. Kisha mulango ukafungwa. 11 Nyuma, hao mabikira wengine wakafika, na kuanza kusema: «Bwana, bwana, utufungulie! 12 Lakini bwana akajibu: “Kweli ninawaambia: mimi siwajui ninyi.” 13 Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.”» 14 Maana mambo hayo ya Ufalme wa mbinguni ni kama mtu aliyetaka kwenda safari. Yeye akawaita watumishi wake, akawagawanyia mali yake. 15 Akamupatia mmoja furushi tano za zahabu, mwingine furushi mbili na mwingine furushi moja kwa kadiri ya uwezo wa kila mmoja, kisha akasafiri. 16 Mara moja yule mtumishi aliyepata furushi tano, akaenda kufanya uchuuzi na mali ile, akafaidia zingine tano. 17 Na yule aliyepata furushi mbili akafaidia zingine mbili. 18 Lakini yule aliyepewa furushi moja, akachimba shimo katika udongo na kuficha ile mali ya bwana wake mule. 19 Kulipopita siku nyingi, bwana wa watumishi wale akarudi, akafanya hesabu ya mali yake pamoja nao. 20 Yule mtumishi aliyepewa furushi tano za zahabu, akakuja, akaleta faida ya zingine tano. Na akasema: «Bwana, umenipatia furushi tano za zahabu, na sasa angalia, kuna faida ya zingine tano. 21 Bwana wake akamwambia: “Ni vizuri, wewe mtumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mengi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako.” 22 Halafu mtumishi aliyepewa furushi mbili akakuja, akasema: “Bwana, umenipatia furushi mbili; na sasa angalia, kuna faida ya zingine mbili.” 23 Bwana wake akamwambia: “Ni vizuri, wewe mtumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mingi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako!” 24 Kisha yule mtumishi aliyepewa furushi moja akakuja, akasema: “Bwana, nilijua kuwa wewe ni mtu mugumu anayevuna nafasi asipopanda, na kukusanya nafasi asiposambaza. 25 Kwa hiyo niliogopa, nami nikaenda kuficha ile mali yako ndani ya udongo. Basi mali yako ndiyo hii, uitwae.” 26 Naye bwana wake akamujibu: “Wewe mtumishi mubaya na muvivu! Ulijua kama ninavuna nafasi nisipopanda, na kukusanya nafasi nisiposambaza. 27 Basi, ungepaswa kuweka mali yangu ndani ya banki, kusudi siku ya kurudi kwangu, ningepata mali yangu pamoja na faida yake. 28 Mumunyanganye ile furushi moja na kuitoa kwa yule anayekuwa na furushi kumi. 29 Kwa maana mtu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine; lakini mtu asiyekuwa na kitu, ataondolewa hata kidogo anachokuwa nacho. 30 Na zaidi ya hii, mumutupe huyu mtumishi asiyekuwa na mafaa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.”» 31 Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu. 32 Mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atayatenga kwa makundi mawili kama vile mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi. 33 Ataweka kondoo kwa upande wake wa kuume, na mbuzi kwa upande wake wa kushoto. 34 Halafu mfalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: «Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia. 35 Kwa maana nilisikia njaa, mukanipa chakula; nilisikia kiu, mukanipa maji; nilikuwa mugeni, mukanikaribisha; 36 nilikuwa uchi, mukanipatia nguo; nilikuwa mugonjwa, mukanisaidia; nilikuwa katika kifungo, mulikuja kuniangalia. 37 Halafu wenye haki watamujibu: “Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukisikia njaa, tukakupa chakula, au uliposikia kiu, tukakupa maji? 38 Ni wakati gani tulipokuona uko mugeni, tukakukaribisha, ulipokuwa uchi, tukakupatia nguo? 39 Na ni wakati gani tulipokuona uko mugonjwa au uko katika kifungo tukakuja kukuangalia?” 40 Mfalme atawajibu: “Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mmoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.” 41 Kisha mfalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: “Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake! 42 Kwa maana nilisikia njaa, nanyi hamukunipa chakula; nilisikia kiu, nanyi hamukunipa maji; 43 nilikuwa mugeni, nanyi hamukunikaribisha; nilikuwa uchi, nanyi hamukunipatia nguo; nilikuwa mugonjwa na nilikuwa katika kifungo, nanyi hamukukuja kuniangalia.” 44 Halafu nao watajibu: “Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukisikia njaa, au kiu, au ukikuwa mugeni, au uchi, au mugonjwa, au mufungwa, nasi hatukukusaidia?” 45 Naye mfalme atawajibu: “Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokosa kumutendea mmoja wa hawa wanaohesabiwa kuwa wadogo, hamukunitendea mimi. 46 Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”»