"Wakati Raheli alipogundua ya kwamba hawezi kupata mimba"
Raheli anatumia ukuzaji kuonyesha jinsi alivyohuzunika ya kuhusu kutopata watoto. "Nitajisikia sina maana yoyote kabisa"
"Nisababishie kupata mimba"
Hasira ya Yakobo inazungumziwa kana kwamba ilikuwa moto. "Yakobo alimkasirikia sana Raheli"
Hili ni swali la balagha ambalo Yakobo anatumia kumkaripia Raheli. Inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mimi si Mungu! Mimi siye ninayekuzuia kupata watoto"
"Raheli akasema"
"Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachotaka kukuambia". Hii inaongeza msisitizo kwa kile Raheli anachosema baadae"
Katika kipindi hicho, njia hii ilikuwa inakubalika kwa mwanamke tasa kupata watoto ambao kisheria wangekuwa wa kwake. Maana kamili inaweza kuwekwa wazi.
Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.
Hii ni namna ya kusema ya kwamba mtoto ambaye Bilha anamzaa atakuwa wa Raheli. "wa kwangu"
"na kwa njia hii atanifanya niwe na watoto"
Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.
"akazaa mtoto wa kiume kwa Yakobo"
"Raheli akmpatia jina"
"Jina la Dani lina maana ya "alihukumu".
"Bilha ... akawa mimba tena"
"na akazaa mtoto wa kiume wa pili kwa Yakobo"
Msemo huu "mashindano nimeshindana" ni msemo unaotumiwa kwa msisitizo. Pia ni sitiari inayozungumzia jaribio la Raheli kupata mtoto kama dada yake kana kwamba alikuwa akigombana kimwili na Lea. "nimepambana sana kupata watoto kama dada yangu, Lea"
"na nimeshinda" au "nimefaulu"
"Jina la Naftali lina maana ya 'mapambano yangu'"
"Lea alipopata ufahamu wa jambo hilo"
"alimpatia Zilpa, mtumishi wake, kwa Yakobo kama mke"
Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.
"akazaa mtoto wa kiume kwa Yakobo"
"Bahati gani!" au "Bahati gani hii!"
"Jina la Gadi lina maana ya "mwenye bahati"
Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.
"akazaa mtoto wa pili wakiume kwa Yakobo"
"Jinsi nilivyobarikiwa!" au "Jinsi nilivyo na furaha!"
"wanawake" au "wanawake wadogo"
"Jina la Asheri lina maana ya "furaha"
"Rubeni alitoka nje"
Hapa msemo "siku za" ni sitiari yenye maana ya majira au kipindi cha mwaka. "katika kipindi cha mwaka cha mavuno ya ngano" au "wakati wa mavuno ya ngano"
Hili ni tunda ambalo linasemekana kuongeza uwezo wa kuzaa na kuongeza hamu ya mtu kulala na mpenzi wake. "tunda la upendo"
"Je haujali ... mume wangu?" Hili ni swali la balagha limetumika kumkaripia Raheli. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli, "ni mbaya sana .. mume wangu"
Hili ni swali la balagha limetumika kumkaripia Raheli. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli, "Na sasa unataka ... pia?"
"Basi Yakobo atalala" au "Basi nitamruhusu Yakobo alale"
"kwa bei ya tunguja za mwanangu"
"akawa mimba"
"na akazaa mtoto wa kiume wa tano kwa Yakobo"
Mungu kumzawadia Lea inazungumzwa kana kwamba alikuwa bosi anayelipa mshahara kwa mtu anayefanya kazi kwake. "Mungu amenipa stahiki yangu" au "Mungu amenizawadia"
"Jina la Isakari lina maana ya "kuna dhawabu"
"Lea akawa mimba tena"
"na kuzaa mtoto wa kiume wa sita kwa Yakobo"
"Jina la Zabuloni lina maana ya "heshima"
Hili ni jina la binti wa Lea.
Msemo huu "akamkumbuka" una maana kukumbuka. Hii haimaanishi Mungu alimsahau Raheli. Ina maana alimfikiria juu ya ombi lake. "Mungu alimfikiria Raheli na kumpatia kile alichokitaka"
Mungu kusababisha Raheli kutosikia aibu tena inazungumziwa kana kwamba "aibu" ni kitu ambacho mtu anaweza kukichukua kutoka kwa mtu mwingine. Nomino inayojitegemea "aibu" inaweza kuwekwa kama "kuona aibu". "Mungu amenisababishia nisione aibu tena"
"Jina la Yusufu maana yake ni "na aongeze"
watoto wa kwanza wa Raheli walitokana na mtumishi wa kike wa Bilha.
"Baada ya Raheli kumzaa Yusufu"
"ili niondoke"
Yakobo anamkumbusha Labani kuhusu mkataba wake (29:26) Nomino inayojitegemea "huduma" inaweza kusemwa kama "kutumika". "unafahamu ya kwamba nimekutumikia muda wa kutosha"
"Labani akamwambia Yakobo"
Msemo wa "machoni pako" ni lugha inayomaanisha mawazo na maoni ya Yakobo. Iwapo nimepata kibali na wewe" au "Iwapo unapendezwa na mimi"
Hii ni lahaja yenye maana ya mtu amekubalika na mtu mwingine.
"tafadhali kaa, kwa sababu"
"Nimegundua kwa desturi yangu ya kiroho na uchawi"
"kwa sababu yako"
Hii inaweza kuwekwa wazi. "Niambie nahitaji kukulipa kiasi gani kukuweka hapa"
"Yakobo alimwambia Labani"
"jinsi mifugo wako walivyokuwa vizuri tangu nimeanza kuwatunza"
"mifugo wako walikuwa wadogo kabla sijakutumikia"
"lakini sasa utajiri wako umeongezeka sana"
"Basi ni lini nitatunza familia yangu?" Yakobo anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba anataka kujitoa kwa familia yake. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "basi ninataka kutunza familia yangu!"
"Nitakulipa nini" au "Nikupatie nini". Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "Nitakulipa nini ili kwamba ubaki na kunitumikia"
Neno la kiunganishi "ikiwa" inaweza kuongezwa kuonyesha ya kwamba hili ni jambo moja ambalo Yakobo anataka. "Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu"
"nitalisha na kuwatunza mifugo wako"
"na kutoa kila kondoo wa madoia, kila kondoo mweusi, na kila mbuzi mwenye madoa"
"Hii itakuwa gharama ya kuniweka hapa"
Neno "uadilifu" lina maana ya "uaminifu". Hii inazungumzia kuhusu uadilifu kana kwamba ni mtu ambaye anaweza kushuhudia kwa ajili au dhidi ya mtu mwingine. "Na baadae utajua kama nimekuwa mwaminifu na wewe au la"
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Iwapo utakuta mbuzi yeyote asiyena madoa au kondoo yeyote ambaye sio mweusi, utawahesabu kuwa wameibiwa"
Hapa "neno" ina maana ya kitu kilichosemwa. "Itakuwa kana kwamba unasema" au "Tutafanya kile ulichosema"
"ambazo zilikuwa na milia na madoa"
"yaliyokuwa na madoa"
"kila mbuzi ambaye alikuwa na weupe ndani yake"
"na kondoo wote weusi"
Hapa "mikono" ina maana ya kutawala au kutunza. "akawafanya wanawe kuwatunza"
Hii yote ni miti ya mbao nyeupe
"na kutoa maganda ya mti ili kwamba mbao nyeupe ya chini ionekane"
vyombo virefu vya wazi vinavyoshikilia maji kwa ajili ya wanyama kunywa
"Wanyama wa mifugo walizalishana" au "Wanyama walipandana"
"wakazaa watoto weney milia na madoa"
Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba hii ilitokea katika kipindi cha miaka kadhaa. "Katika kipindi cha miaka kadhaa iliyofuata, Yakobo akawagawanya"
"kutazama kuelekea"
"aliwatenganisha mifugo wake"
Hapa "macho" ina maana ya "kuona". "ili kwamba mifugo waweze kuona"
"mbele ya fito"
"wanyama wenye nguvu chache"
"Kwa hiyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wale wenye nguvu wakawa wa Yakobo". Unaweza kuiweka wazi zaidi. "Kwa hiyo wanyama dhaifu hawakuwa na milia au madoa na wakawa wa Labani, na wale wenye nguvu hawakuwa na milia au madoa na wakawa wa Yakobo"
"Yakobo"
"akafanikiwa sana" au "akawa tajiri sana"