Genesis 26

Genesis 26:1

Kwa nini Isaka alikwenda katika mji wa Gerari ambako Abimeleki alikuwa mfalme wa Wafilisti?

Isaka alikwenda Gerari kwa sababu kulikuwa na njaa katika nchi.

Genesis 26:2

Yahwe alikuwa amemwambia nini Isaka kabla ya Isaka kwenda Gerari?

Yahwe alimwambia Isaka kutokwenda Misri na kukaa katika nchi ambayo alikwenda kumwambia Isaka.

Yahwe alimwambia nini Isaka kuhusu kiapo alichoapa Yahwe kwa baba yake Abrahamu?

Yahwe alimwambia Isaka ya kwamba atatimiza kiapo ambacho Yahwe aliapa kwa Abrahamu.

Genesis 26:4

Yahwe alisema alikwenda kufanya nini?

Yahwe alisema alikwenda kufanya hivyo kwa sababu Abrahamu alitii sauti yake na kushika maelekezo, amri, maagizo na sheria zake.

Genesis 26:6

Isaka alisema nini kwa wanamume wa Gerari kuhusu Rebeka, mke wake?

Isaka aliwaambiwa wanamume wa Gerari ya kwamba Rebeka alikuwa dada yake.

Genesis 26:9

Kulingana na Abimeleki, ni jambo gani lingeleta hatia juu ya watu kwa sababu ya uongo wa Isaka?

Kwa sababu ya uongo wa Isaka, mtu angeweza kulala na Rebeka na kuleta hatia juu ya watu.

Abimeleki alitoa amri gani kuhusu Rebeka?

Abimeleki aliamuru ya kwamba yeyote atakayemgusa Rebeka atauawa.

Genesis 26:15

Abimeleki alitoa sababu gani kwa kumuuliza Isaka kuondoka kwa Wafilisti?

Abimeleki alimwambia Isaka kuondoka kwa Wafilisti kwa sababu alisema, "... kwa kuwa wewe una nguvu kuliko sisi"

Genesis 26:18

Kwa nini Isaka ilimbidi kuchimbua visima vya maji ambavyo vilichimbwa katika siku za Abrahamu?

Ilimpasa Isaka kuchimbua visima vya maji ambavyo vilichimbwa katika siku za Abrahamu kwa sababu Wafilisti walivizuia baada ya kifo cha Abrahamu.

Genesis 26:21

Isaka alitajaje kisima ambacho wachungaji wa Gerari hawakukigombania na yeye?

Isaka alikiita kisima, ambacho wachungaji wa Gerari hawakukigombania naye, Rehobothi.

Genesis 26:23

Yahwe alimhakikishia nini Isaka alipomtokea Beersheba?

Yahwe alimhakikishia ya kwamba angembariki Isaka na kuvizidisha vizazi vyake.

Genesis 26:28

Abimeleki alitaka kufanya agano gani na Isaka, na kwa nini?

Abimeleki alitaka kufanya agano ambalo pande zote hazitamdhuru mwenzake, kwa sababu aliona ya kuwa Yahwe alikuwa pamoja na Isaka.

Genesis 26:30

Isaka alipokeaje ombi la Abimeleki kwa agano kati yao?

Isaka alifanya sherehe, na wakaapa kiapo kati yao.

Genesis 26:34

Wake wa Esau walitokana na makundi yapi mawili?

Wake wawili wa Esau walitoka kwa Wahiti.

Uhusiano kati ya wake wa Esau na Isaka na Rebeka ulikuaje?

Wake wa Esau walileta huzuni kwa Isaka na Rebeka.