Genesis 25

Genesis 25:1

Abrahamu alifanya nini baada ya mke wake Sara kufariki?

Abrahamu alichukua mke mwingine aliyeitwa Ketura.

Genesis 25:5

Abrahamu aligawanishaje utajiri wake?

Abrahamu alitoa zawadi kwa wana wa masuria wake, na kutoa kila alichokuwa nacho kwa mwanawe Isaka.

Genesis 25:7

Abrahamu aliishi miaka mingapi?

Abrahamu aliishi miaka mia moja na sabini na tano?

Genesis 25:9

Nani alimzika Abrahamu?

Wote Isaka na Ishmaeli walimzika Abrahamu.

Genesis 25:17

Wana kumi na mbili wa Ishmaeli waliishije kati yao?

Wana kumi na wawili wa Ishmaeli waliishi kwa uadui kati yao.

Genesis 25:21

Isaka alifanya nini kwa sababu Rebeka kuwa tasa?

Isaka aliomba kwa Yahwe kwa ajili ya mke wake, na Yahwe alijibu maombi yake, na Rebeka akabeba mimba.

Genesis 25:23

Yahwe alisema nini kuhusu wale watoto wawili waliopambana tumboni mwa Rebeka?

Yahwe alisema ya kwamba kutakuwa na mataifa mawili tumboni mwake, mtu mmoja mwenye nguvu zaidi ya mwenzake, na mkubwa atamtumikia mdogo.

Genesis 25:24

Nani alizaliwa kwanza, na alionekanaje?

Esau alizaliwa kwanza, naye alikuwa mwekundu kote kama vazi la nywele.

Nani alizaliwa wa pili, na alikuwa akifanya nini alipozaliwa?

Yakobo alizaliwa wa pili, naye alikuwa akikamata kisigino cha Esau alipozaliwa.

Genesis 25:27

Esau alikuwa mtu wa namna gani?

Esau alikuwa mwindaji hodari na mtu wa nyikani.

Yakobo alikuwa mtu wa namna gani?

Yakobo alikuwa mtu mkimya aliyetumia muda wake katika mahema.

Isaka alipenda nini, na Rebeka alimpenda nani?

Isaka alimpenda Esau, na Rebeka alimpenda Yakobo.

Genesis 25:29

Jina lingine la Esau lilikuwa ni lipi?

Edomu lilikuwa ni jina lingine la Esau.

Genesis 25:31

Yakobo aliomba nini kwa ajili ya mchuzi wa dengu ambao Esau alitaka kula kwa sababu alikuwa na njaa kali?

Yakobo alimuomba Esau haki yake ya kuzaliwa kwa ajili ya mchuzi wa dengu.

Jibu la Esau lilikuwa ni lipi kwa ahadi ya Yakobo?

Esau aliapa kiapo na kuuza haki yake ya kuzaliwa kwa Yakobo.

Esau alikuwa akitendeaje haki yake ya kuzaliwa alipokuwa akitoa jibu kwa njia kwa ahadi ya Yakobo?

Esau alikuwa akidharau haki yake ya kuzaliwa alipokuwa akijibu ahadi ya Yakobo kwa namna hii.