Genesis 24

Genesis 24:1

Abrahamu alimfanya mtumishi wake mkubwa kuapa jambo gani?

Abrahamu alimfanya mtumishi wake mkubwa kuapa ya kwamba angemtafutia mke kwa ajili ya Isaka kutoka kwa jamaa za Abrahamu.

Genesis 24:5

Abrahamu alisistiza ya kwamba mtumishi asifanye nini na Isaka?

Abrahamu alisisitiza ya kwamba mtumishi asimpeleke Isaka katika nchi ambayo Abrahamu alitoka.

Genesis 24:12

Mtumishi wa Abrahamu alimuomba Mungu afanye nini ili kumuonyesha ni mwanamke yupi Mungu amemchagua kwa ajili ya Isaka?

Mtumishi alimuuliza ya kwamba mwanamke ambaye atamuuliza kutua mtungi wake kupata maji na kufanya vile na kutoa maji kwa ngamia wake pia.

Genesis 24:15

Rebeka alikuwa na uhusiano gani kwa Abrahamu?

Rebeka alikuwa mjukuu wa Nahori, kaka yake Abrahamu.

Genesis 24:17

Rebeka alifanya nini pale mtumishi wa Abrahamu alipomuomba maji ya kunywa?

Rebeka alimpatia mtumishi maji.

Genesis 24:19

Rebeka alisema nini baada ya kumpatia mtumishi maji?

Baada ya Rebeka kumaliza kumpatia mtumishi maji alisema, "Nitachota maji kwa ajili ya ngamia wako pia, mpaka watakapomaliza kunywa".

Genesis 24:26

Mtumishi alifanya nini aliposikia ya kwamba Rebeka alikuwa na uhusiano kwa Abrahamu na kwamba angeweza kukaa usiku huo na familia yake?

Mtumishi alimuabudu Yahwe na kumbariki.

Genesis 24:31

Labani alifanya nini alipokutana na mtumishi wa Abrahamu?

Labani alimkaribisha mtumishi wa Abrahamu kukaa katika nyumba yake.

Genesis 24:33

Mtumishi wa Abrahamu alisisitiza kufanya nini kabla ya kula?

Mtumishi wa Abrahamu alisisitiza kusema kwa nini alikuja kabla hajala.

Genesis 24:39

Abrahamu alisemaje ya kwamba Yahwe angebariki njia ya mtumishi?

Abrahamu alisema ya kwamba Yahwe angetuma malaika wake pamoja na mtumishi kufanikisha njia yake.

Genesis 24:47

Mtumishi alimpatia nini Rebeka aliposikia alikuwa na uhusiano kwa Abrahamu.

Mtumishi wa Abrahamu alimpatia Rebeka pete ya dhahabu kwa ajili ya pua yake na bangili kwa ajili ya mikono yake.

Genesis 24:50

Labani na Bethueli walimjibuje mtumishi wa Abrahamu alipowauliza walitaka kufanya nini kuhusu Rebeka?

Labani na Bethueli walimjibu ya kwamba mtumishi amchukue Rebeka na kuondoka naye, ili kwamba Rebeka aweze kuwa mke wa mwana wa Abrahamu.

Genesis 24:52

Mtumishi wa Abrahamu alifanya nini aliposikia jibu kutoka kwa Labani na Bethueli?

Mtumishi aliinama chini kwa Yahwe na kutoa zawadi kwa Rebeka na kwa kaka na mama yake.

Genesis 24:54

Walipoamka asubuhi iliyofuata, kaka wa Rebeka na mama walimtaka mtumishi kufanya nini?

Walipoamka asunuhi iliyofuata, walimtaka mtumishi wa Abrahamu kubaki nao kwa angalau siku kumi zaidi.

Genesis 24:56

Mtumishi wa Abrahamu aliposema alitaka kwenda mara moja, Rebeka alisema alitaka kufanya nini?

Rebeka alisema ya kwamba anataka kuondoka pamoja na mtumishi.

Genesis 24:59

Familia ya Rebeka ilitoa baraka gani kwake alipoondoka na mtumishi wa Abrahamu?

Familia ya Rebeka ilimbariki ya kwamba aweze kuwa mama wa maelfu na makumi elfu na kwamba uzao wake waweze kumiliki lango la wale wanao wachukia.

Genesis 24:63

Isaka alikuwa akifanya nini Rebeka alipofika katika nyumba yake?

Isaka alikuwa nje shambani akitafakari.

Rebeka alifanya nini alipomwona Isaka?

Alipomwona Isaka, Rebeka aliruka chini kutoka kwenye ngamia na kujifunika kwa shela.

Genesis 24:66

Isaka alifanya nini baada ya mtumishi wa Abrahamu kurejea mambo yote aliyoyafanya?

Isaka alimchukua Rebeka katika hema la mama yake Sara na kumfanya kuwa mke wake.