Genesis 20

Genesis 20:1

Abrahamu alisema nini kuhusu Sara walipokuwa wakiishi Gerari?

Abrahamu alisema ya kwamba Sara alikuwa dada yake.

Mungu alisema nini kwa Abimeleki baada ya kumchukua Sara?

Mungu alikuja kwa Abimeleki katika ndoto na kumwambia ya kwamba alikuwa mtu mfu kwa sababu alichukua mke wa mtu.

Genesis 20:4

Abimeleki alisema nini kwa Mungu ya kuwa aliambiwa na Abrahamu na Sara?

Abimeleki alisema kwa Mungu ya kwamba Abrahamu alimwambia Sara alikuwa dad yake, na Sara alimwambia Abrahamu alikuwa kaka yake.

Genesis 20:6

Mungu alimwambia Abimeleki afanye nini, na Mungu alisema nini kingetokea iwapo hatafanya hivyo?

Mungu alimwambia Abimeleki kumrudisha Sara kwa Abrahamu; la sivyo, yeye na watu wake wote wangekufa.

Genesis 20:8

Watu wa Abimeleki waliitikiaje waliposikia kile ambacho Mungu alimwambia Abimeleki?

Watu wa Abimeleki waliogopa sana waliposikia kile ambacho Mungu alimwambia.

Genesis 20:10

Kwa nini Abrahamu alisema ya kuwa alimwambia Abimeleki ya kwamba Sara alikuwa ni dada yake?

Abrahamu alisema ya kwamba aliogopa Abimeleki angemuua kwa sababu ya Sara.

Kwa njia gani haswa Sara alikuwa dada yake Abrahamu?

Sara alikuwa binti wa baba wa Abrahamu lakini sio wa mama yake.

Genesis 20:15

Abimeleki alimpatia Abrahamu wanyama na watu gani?

Abimeleki alimpatia Abrahamu kondoo, maksai, watumwa wa kiume na kike.

Ni sababu ipi ambayo Abimeleki alimpatia Sara ni kwa nini alimpa kaka yake vipande elfu vya fedha?

Abimeleki alimwambia Sara ya kuwa amempatia vipande vya fedha kwa kaka yake kufunika kosa lolote dhidi ya Sara machoni pa wote waliokuwa na Sara, na mbele ya kila mtu.

Genesis 20:17

Abrahamu alipoomba kwa Mungu kwa ajili ya Abimeleki na watu wake nini kilitokea?

Mungu alimponya Abimeleki, mke wake, na watumwa wake wa kike ili waweze kupata watoto.