Genesis 50

Genesis 50:1

akauangukia uso wa baba yake

Msemo "akauangukia" ni lahaja ya kuzidiwa. "hadi akaanguka juu ya baba yake kwa majonzi"

watumishi wake matabibu

"watumishi wake ambao waliangalia maiti"

kumtia dawa babaye

"kumtia dawa" ni njia maalumu ya kuhifadhi maiti kabla haijazikwa. "kuandaa mwili wa baba yake kabla ya mazishi"

Wakatimiza siku arobaini

"Wakatimiza siku 40"

siku sabini

"siku 70"

Genesis 50:4

Siku za maombolezo

"siku za kumuomboleza" au "siku za kumlilia"

Yusufu akaongea na watumishi wa baraza la kifalme

Hapa "baraza la kifalme" ina maana ya maafisa ambao huunda baraza la kifalme la Farao. "Yusufu alizungumza na maafisa wa Farao"

Ikiwa nimepata kibali machoni penu

Msemo "machoni penu" ni lugha nyingine yenye maana ya fikra na mawazo ya Yakobo. "Iwapo nimepata kibali kwako" au "kama umefurahishwa na mimi"

nimepata kibali

Hii ni lahaja yenye maana ya kwamba mtu amekubalika na mtu mwingine.

tafadhali ongeeni na Farao, kusema, 5'Baba yangu aliniapisha, kusema, "Tazama, ninakaribia kufa. Unizike katika kaburi nililolichimba kwa ajili yangu mwenyewe katika nchi ya Kanaani. Ndipo utakaponizika." Basi sasa niruhusu niende nimzike baba yangu, na kisha nitarudi."

Hii ina madaraja mawili ya nukuu na madaraja matatu ya nukuu. Hizi zinaweza kuwekwa kama nukuu zisizo moja kwa moja. "tafadhali mwambie Farao ya kwamba baba yangu alinifanya niape ya kuwa baada ya kufa kwake nitamzika katika kaburi ambalo alilichimba kwa ajili yake katika nchi ya Kaanani. Tafadhali muombe Farao aniruhusu niende kumzika baba yangu, na kisha nitarudi.

Tazama, ninakaribia kufa

"Tazama, ninakufa"

niruhusu niende juu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kwenda juu" pale izungumzwapo safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Farao akajibu

Inasemekana ya kwamba wajumbe wa baraza walizungumza na Farao, na sasa Farao anamjibu Yusufu.

kama alivyokuwapisha

"kama ulivyoapa kwake"

Genesis 50:7

Yusufu akaenda juu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kwenda juu" inapozungumziwa safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Maofisa wote ... washauri ... maofisa waandamizi

viongozi wote muhimu wa Farao walihudhuria tukio la mazishi.

washauri

Huyu mtu alikuwa mshauri wa kifalme.

washauri wa nyumba yake

Hapa "nyumba" ina maana ya baraza la kifalme la Farao.

nchi ya Misri, pamoja na nyumba yote ya Yusufu na ndugu zake, na nyumba yote ya baba yake

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "nchi ya Misri. Nyumba ya Yusufu, ndugu zake, na nyumba ya baba yake walikwenda naye"

nyumba ya Yusufu ... nyumba ya baba yake

Hapa "nyumba" ina maana ya familia zao.

Vibandawazi

Hapa ina maana ya wanamume wanaoendesha ndani ya vibandawazi.

Lilikuwa kundi kubwa sana la watu

"ulikuwa mkusanyiko mkubwa sana"

Genesis 50:10

Hata walipokuja

Neno "walipokuja" lina maana ya washiriki katika tukio la mazishi.

sakafu ya Atadi

Maana zaweza kuwa 1) neno la "Atadi" lina maana ya "mwiba" na lina maana ya sehemu ambapo kuna idadi kubwa ya miiba inayoota, au 2) inaweza kuwa jina la mtu anayemiliki sakafu ya kupigia.

wakaomboleza kwa majonzi ya huzuni kubwa

"walikuwana huzuni kubwa na walilia sana"

ya siku saba

"ya siku 7"

katika sakafu ya Atadi

"katika sakafu ya kupigia ya Atadi"

Hili ni tukio la kuhuzunisha sana kwa Wamisri

"maombolezo ya Wamisri ni mkubwa sana"

Abeli Mizraimu

"Jina la Abeli Mizraimu lina maana ya "maombolezo ya Misri"

Genesis 50:12

wanawe

"Kwa hiyo wana wa Yakobo"

kama alivyokuwa amewaagiza

"kama alivyokuwa amewaagiza"

Wanawe wakambeba

"Wanawe waliuchukua mwili wake"

Makpela

Makpela ni jina la jina la eneo au sehemu.

Mamre

Hili lilikuwa jina jingine la mji wa Hebroni. Inawezekana lilikuwa jina baada ya Mamre, rafiki wa Abrahamu aliyeishi kule.

Efroni Mhiti

Hili ni jina la mwanamume. "Mhiti" ina maana ya "uzao wa Hethi"

Yusufu akarudi Misri

"Yusufu alirudi Misri"

wote waliokuwa wamemsindikiza

"wale wote waliokuja pamoja nami"

Genesis 50:15

Itakuwaje ikiwa Yusufu atatukasirikia

Hapa hasira inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu cha kimwili ambacho Yusufu alikishika kwa mkono wake. "Je iwapo Yusufu atakuwa bado na hasira na sisi"

akataka kutulipa kikamilifu kwa ajili ya uovu tuliomtenda

Kulipiza mwenyewe dhidi ya mtu mwingine aliyemdhuru inazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa akilipa mtu mwingine kile walichodai. "anataka kulipiza kwa uovu tuliofanya kwake"

Baba yako alitoa maelekezo kabla hajafa, kusema, 'Mwambieni hivi Yusufu, "Tafadhali samehe makosa ya ndugu zako na dhambi yao uovu waliokutenda."

Hii ina madaraja mawili ya nukuu na madaraja matatu ya nukuu. Zinaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Baba yako alituagiza kabla ya kufa tukuambie ya kwamba utusamehe kwa uovu tuliokufanyia kwako"

Baba yako alitoa maelekezo kabla hajafa, kusema

Yakobo alikuwa baba wa ndugu wote. Hapa wanasema "baba yako" kusisitiza ya kwamba Yusufu anahitaji kuvuta nadhari kwa kile baba yake alichosema. "Kabla baba yetu hajafa alisema"

na dhambi yao uovu waliokutenda

"kwa mambo maovu waliyokufanyia kwako"

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Basi wasamehe watumishi wa Mungu wa baba yako

Ndugu wanajitambulisha kama "watumishi wa Mungu wa baba yako". Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "tafadhali tusamehe, watumishi wa Mungu wa baba yetu"

Yusufu akalia walipomwambia.

"Yusufu alilia aliposikia ujumbe huu"

Genesis 50:18

kuinamisha nyuso zao mbele zake

Walilala chini kifudifudi kuelekea ardhini. Hii ni ishara ya unyenyekevu na heshima kwa Yusufu.

Je mimi ni badala ya Mungu?

Yusufu anatumia swali kuwatia moyo ndugu zake. "Mimi sipo katika nafasi ya Mungu" au "Mimi sio Mungu"

mlikusudia kunidhuru

"mlikusudia kutenda uovu dhidi yangu"

Mungu alikusudia mema

"Mungu alikusudia kwa wema"

Hivyo basi msiogope

"Kwa hiyo msiniogope"

Nitawahudumia ninyi na watoto wenu wadogo

"Nitahakikisha nyie pamoja na watoto wenu mnapata chakula cha kutosha"

aliwatia moyo na kuongea na mioyo yao kwa upole.

"Aliwatia moyo kwa kuzungumza nao kwa upole"

Genesis 50:22

miaka mia moja na kumi

"miaka 110"

Efraimu hata kizazi cha tatu

"Watoto na wajukuu wa Efraimu"

Makiri

Hili ni jina la mjukuu wa Yusufu"

waliowekwa katika magoti ya Yusufu

Msemo huu una maana ya kwamba Yusufu alitwaa watoto hawa wa Makiri kama watoto wake. Hii ina maana wangekuwa na haki ya urithi maalumu kutoka kwa Yusufu.

Genesis 50:24

atawajilia

Katika 50:24 neno "atawajilia" lina maana ya ndugu wa Yusufu, lakini pia lina maana ya uzao wake.

kuwaongoza kutoka katika nchi hii na kuwapeleka katika nchi

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kupanda" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani. "kuwaleta kutoka nchi hii na kuwapeleka katika nchi"

Wakampaka dawa

"kumpaka dawa" ni njia maalumu ya kuhifadhi maiti kabla haujazikwa.

akawekwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "walimweka"

katika jeneza

"ndani ya sanduku" au "katika kasha". Hili ni sanduku ambalo mtu aliyekufa kuwekwa ndani.