Genesis 46

Genesis 46:1

akaja Beersheba

"alikuja Beersheba"

Mimi hapa

"Ndio, ninasikiliza"

kushuka Misri

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

nitakufanya taifa kubwa

Hapa "nitakufanya" ni katika umoja na una maana ya Yakobo. Hii "nitakufanya" pia ina maana ya uzao wa Israeli ambao watakuwa taifa kubwa. "Nitakupatia uzao mkubwa, nao watakuwa taifa kubwa"

huko Misri

"huko Misri"

Nami nitakupandisha huku tena bila shaka

Ahadi ilifanywa kwa Yakobo, lakini ahadi hii ingetimizwa kwa uzao wote wa Yakobo. "Hakika nitaleta uzao wako kutoka Misri tena"

nitakupandisha huku tena

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kupanda" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Na Yusufu akayafunika macho yako kwa mikono yake

Msemo huu "akayafunika macho yako kwa mikono yake" ni njia ya kusema ya kwamba Yusufu atakuwepo pale ambapo Israeli atakufa na Yusufu atauafumba macho ya Yakobo katika kipindi cha kifo chake. "Na Yusufu pia atakuwepo pamoja na wewe katika kipindi cha kifo chako"

akayafunika macho yako

Ilikuwa ni utamaduni kufunika kope za macho pale mtu anapokufa na macho yake wazi. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Genesis 46:5

akainuka kutoka

"kuwekwa kutoka kwa"

katika mikokoteni

"Mikokoteni" ni gari dogo la abiria na mizigo lenye magurudumu mawili au manne. Wanyama huvuta mikokoteni.

walizokuwa wamezipata

"ambazo walikusanya" au "waliopata"

Akaja pamoja nao

"Yakobo akaja pamoja nao"

wanawe

"wajukuu wake"

wana wa binti zake

"wajukuu wake wa kike"

Genesis 46:8

Haya ni majina

Hii ina maana ya majina ya watu ambao mwandishi anataka kuwaorodhesha.

ya watoto wa Israeli

"ya watoto wa familia ya Israeli"

Hanoki na Palu na Hezroni na Karmi ... Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli ... Gershoni, Kohathi, na Merari

Haya ni majina ya wanamume.

Genesis 46:12

Eri, Onani, Shela

Hawa walikuwa wana wa Yuda kwa mke wake, Shua.

Shela na Zera

Hawa walikuwa wana wa Yuda kwa mkwe wake, Tamari.

Hezroni ... Hamuli ... Tola, Puva, Lobu ... Shimroni ... Seredi, Eloni ... Yahleeli

Haya ni majina ya wanamume.

Dina

Hili ni jina la binti wa Lea.

Wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu

watatu - Hapa "wanawe" na "mabinti" ina maana ya wana wa Yakobo, mabinti , na wajukuu wenye uhusuiano na Lea. "Kwa pamoja alikuwa na watoto 33, mabinti na wajukuu"

Genesis 46:16

Zifioni ... Hagi, Shuni ... Ezboni, Eri, Arodi ... Areli ... Imna ... Ishva, Ishvi ... Beria ... Heberi ... Malkieli

Haya ni majina ya wanamume.

Sera

Hili ni jina la mwanamke

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

Wana hawa aliomzalia Yakobo - kumi na sita kwa ujumla

Hii ina maana ya watoto 16, wajukuu, na watukuu ambao walikuwa na uhusiano na Zilpa.

Genesis 46:19

Asenathi

"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Farao alimpa Yusufu kuwa mke wake.

Potifera

"Potifera" ni baba yake Asenathi.

kuhani wa Oni

Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.

Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu, na Ardi

Haya ni majina ya wanamume.

jumla yao kumi na wanne

Hii ina maana ya wana 14 na wajukuu waliokuwa wamehusiana na Raheli.

Genesis 46:23

Hushimu ... Yahzeeli, Guni, Yezeri ... Shilemi

Haya ni majina ya wanamume.

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

wote walikuwa saba

Hii ina maana ya wana 7 na wajukuu waliokuwa wamehusiana na Bilha.

Genesis 46:26

sitini na sita

sita - "66"

sabini

"70"

Genesis 46:28

kuonesha njia mbele yake kwenda Gosheni

"kuwaonyesha njia ya kuelekea Gosheni"

Yusufu akaandaa kibandawazi chake na akaenda

Hapa "Yusufu" ina maana ya watumishi wake. "Watumishi wa Yusufu waliaanda kibandawazi chake na Yusufu akenda juu"

akaenda kukutana na baba yake Israeli

Msemo wa "kwenda juu" unatumika kwa sababu Yusufu anasafiri kwenye kwenye mwinuko kukutana na baba yake" "akaenda kukutana na baba yake"

akaikumbatia shingo yake, na akalia shingoni mwake kwa muda mrefu

"akaweka mikono yake kumzunguka baba yake, na kulia kwa muda mrefu"

Basi na nife sasa

"Sasa nipo tayari kufa" au "Sasa nitakufa na furaha"

kwa kuwa nimeuona uso wako, kwamba bado uko hai

Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. Yakobo anaonyesha furaha ya kumuona Yusufu. "kwa maana nimekuona ukiwa hai tena"

Genesis 46:31

nyumba ya baba yake

Hapa "nyumba" ina maana ya familia yake. "familia ya baba yake" au "nyumba ya baba yake"

Nitakwenda na kumwambia Farao

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kwenda juu" pale mtu azungumzapo na mtu mwenye mamlaka makubwa. "Nitakwenda kumwambia Farao"

kumwambia Farao, kusema, 'Ndugu zangu ... vyote walivyonavyo.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "mwambie Farao ya kwamba ndugu zangu ... vyote walivyonavyo"

Genesis 46:33

Itakuwa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama kwa tukio muhimu ambalo linataka kutokea katika simulizi.

na kuwauliza, 'Kazi yenu ni ipi?' mwambieni,

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa ... sisi, na baba zetu."

mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa ...sisi, na baba zetu."

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa ... sisi, na baba zetu."

Watumishi wako

Familia ya Yusufu wanajitambulisha kama "watumishi wako" wanapozungumza na Farao. Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "Sisi, watumishi wako"

kila mfugaji ni chukizo kwa Wamisri

Nomino inayojitegemea ya "chukizo" inaweza kutafsiriwa na kivumishi "yenye maudhi". "Wamisri wanadhani ufugaji ni maudhi"