Genesis 16

Genesis 16:1

Sasa

Neno hili linatumika kutambulisha sehemu mpya ya simulizi na taarifa ya nyuma kuhusu Sarai.

mtumishi wa kike

"mtumwa wa kike". Mtumwa wa namna hii alikuwa akimtumikia mwanamke wa nyumbani.

kutopata watoto

"kutoweza kuzaa watoto"

niweze kupata watoto kupitia yeye

"Nitajenga familia yangu kupitia kwake"

Abram akasikiliza sauti ya Sarai

"Abramu alifanya kile Sarai alichosema"

akamdharau bibi yake

"alimdharau bibi yake" au "alifikiria alikuwa na thamani zaidi ya bibi yake"

bibi yake

Hapa ina maana ya Sarai. Bibi alikuwa na uwezo juu ya mtumwa wake. "mmiliki wake" au "Sarai"

Genesis 16:5

Jambo hili baya kwangu

"Udhalimu huu dhidi yangu"

ni kwa sababu yako

"ni wajibu wako" au "ni kosa lako"

Nilimtoa mtumishi wangu wa kike katika kumbatio lako

Sarai alitumia neno "kumbatia" hapa kumaanisha yeye kulala naye. "Nilimpa mtumishi wangu ili uweze kulala naye"

nilidharaulika machoni pake

Hii inaweza kuwa katika hali ya kutenda. "alinichukia" au"alianza kunichukia" au "alidhani yeye ni bora zaidi yangu"

Na sasa acha Yahwe aamuwe kati yangu na wewe

"Ninataka Yahwe aseme kama hili ni kosa langu au lako" au "Nataka Yahwe kuamua nani kati yetu yupo sahihi." Msemo "aamue kati ya" una maana ya kuamua nani yuko sawa katika ugomvi kati yao"

Tazama, hapa

"Nisikilize mimi" au "Sikiliza kwa makini"

katika uwezo wako

"chini ya mamlaka yako"

Sarai akakabiliana naye kwa ukatili

"Sarai alimtendea Hajiri vibaya sana"

na akatoroka

"na Hajiri akatoroka kwa Sarai"

Genesis 16:7

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

jangwa

Eneo la jangwa aliloenda lilikuwa ni nyikani. "jangwa"

Shuri

Hii ilikuwa jina ya sehemu kusini mwa Kaanani mashariki mwa Misri.

bibi yangu

Hapa ina maana ya Sarai. Bibi alikuwa na mamlaka juu ya mtumwa wake. "mmiliki wangu".

Genesis 16:9

Malaika wa Yahwe akamwambia

"Malaika wa Yahwe alimwambia Hajiri"

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

bibi yako

Hapa ina maana ya Sarai. Bibi alikuwa na uwezo juu ya mtumwa wake. "mmiliki wake" au "Sarai"

Kisha Malaika wa Yahwe akamwambia, "Nita

Aliposema "Nita" alikuwa ana maana ya Yahwe.

Nitazidisha uzao wako maradufu

"Nitakupatia uzao mwingi sana"

wengi wasioweza kuhesabika

"wengi sana hadi hakuna mtu atakayeweza kuwahesabu"

Genesis 16:11

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini"

utazaa mtoto kiume

"kuzaa mtoto wa kiume"

utamwita jina lake

"utamuita jina lake". Neno "utamuita" linamlenga Hajiri.

Ishmaeli, kwa sababu Yahwe amesikia

Watafsiri wanaweza kuweka maelezo mafupi yanayosema "Jina la 'Ishmaeli' lina maana ya 'Mungu amesikia'".

mateso

Alikuwa ameteswa na mawazo na mateso.

Atakuwa punda mwitu wa mtu

Hili halikuwa tusi. Inaweza kumaanisha Ishmaeli angekuwa anajitegemea na mwenye nguvu kama punda mwitu. "Atakuwa kama punda mwitu miongoni mwa watu"

Atakuwa adui dhidi ya kila mtu

"Atakuwa adui wa kila mtu"

kila mtu atakuwa adui yake

"Kila mtu atakua adui yake"

na ataishi kando na

Hii inaweza pia kumaanisha "ataishi kwa uadui pamoja na"

ndugu

"ndugu wa karibu"

Genesis 16:13

Yahwe aliye zungumza naye

"Yahwe, kwa sababu alizungumza naye"

je ninaendelea kweli kuona, ... mimi?

Hajiri alitumia swali hili la balagha kuonyesha mshangao wake wa kuwa hai hata baada ya kukutana na Mungu. Watu walitarajia iwapo wanakutana na Mungu, wangekufa. "Ninashangaa ya kwamba bado nipo hai, ... mimi"

Kwa hiyo kisima kiliitwa Beerlahairori

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi yanayosema "Beerlahairori ina maana ya 'kisima cha yule anayeniona mimi"

Tazama, kiko kati ya Kadeshi na Beredi.

Neno "tazama" hapa linavuta ukweli kwamba kisima kilikuwa katika eneo ambalo mwandishi na wasomaji wake walijua. "tena, ilikuwa kati ya Kadeshi na Beredi"

Genesis 16:15

Hajiri akamzalia

Ujio wa Hajiri kwa Sarai na Abramu unajitokeza wazi. Unaweza kufanya hivi kuwa wazi. "Kwa hiyo Hajiri alirudi na kuzaa"

akamwita mwanawe, ambaye Hajiri amemzaa

"alimwita mtoto wake kwa Hajiri" au "alimuita wake na mtoto wa Hajiri"

Abram alikuwa

Hii inatambulisha taarifa ya nyuma kuhusu umri wa Abramu ambapo vitu hivi vilipotokea. Lugha inaweza kuwa na namna maalumu ya kutaja taarifa ya nyuma.

alipomzaa Ishmaeli kwa Abram

Hii inamaanisha "alimzaa mtoto wa Abramu, Ishmaeli." Lengo lipo kwa Abramu kupata mtoto.