Genesis 14

Genesis 14:1

Taarifa ya Jumla:

Maeneno katika 14:1 yote ni miji inayojitegemea

ikaja kuwa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

katika siku

"katika muda wa"

walifanya vita

"walienda vitani" au "walianzisha vita" au "walijiandaa kwa vita"

Genesis 14:3

Hawa wafalme watano wa mwisho waliungana pamoja

Taarifa ya kwamba majeshi yao walikuwa pamoja nao inaweza kuwekwa wazi. "Wafalme hawa watano wa nyuma na majeshi yao waliungana"

miaka kumi na mbili walimtumikia

Matukio katika mistari ya 4-7 yalitokea kabla ya mstari wa 3. Lugha yakoinaweza kuwa na namna ya kuonyesha hivi.

walimtumikia Kedorlaoma

Inawezekana walitakiwa kumlipa kodi na kumtumikia jeshini. "walikuwa chini ya utawala wa Kedorlaoma"

waliasi

"walikataa kumtumikia" au "walisitisha kumtumika"

walikuja na kuwashambulia

Walifanya hivi kwa sababu wafalme wengine waliasi.

Warefai ... Wazuzi ... Waemi ... Wahori

Haya ni majina ya makundi ya watu.

Ashteroth Karnaimu ... Hamu ... Shawe Kiriathaimu ... Seiri ...El Parani

Haya ni majina ya sehemu.

El Parani iliyo karibu na jangwa

Huu msemo unasaidia wasomaji kuelewa El parani ilikuwa wapi. Inaweza kutafsiriwa katika sentensi tofauti kama italazimu. "El Parani. El Parani ipo karibu na jangwa"

Genesis 14:7

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 8 na 9 inarudia kile kilichosemwa katika 14:3 na kuendelea kueleza yaliyojiri baada ya wafalme kukutana pamoja kupigana.

wakarudi wakaja

Neno "wakarudi" lina maana ya wafalme wanne wageni ambao walikuwa wakishambulia eneo la Kanaani. Majina yao yalikuwa Amrafeli, Arioko, Kadorlaoma na Tidali. "wakageuka na kuondoka"

Waamori ambao waliishi Hasasoni Tamari

Msemo huu unaelezea juu ya watu wa Waamori walioshindwa. Hawa walikuwa Waamori wengine walioishi katika maeneno mengine.

na mfalme wa Bela (pia ikiitwa Soari)

Mji wa Bela pia ulikuwa unaitwa Soari. Taarifa hii inaweza kuwekwa mwishoni mwa sentensi. "na mfalme wa Bela akaondoka na kujiandaa kwa vita. Bela pia inaitwa Soari.

kujiandaa kwa vita

"kujiunga vitani" au "kuanza mistari ya vita" Baadhi ya watafsiri wanaweza kusema kuwa majeshi yalipigana.

afme wanne dhidi ya wale watano

Kwa kuwa wafalme watano waliorodheshwa kwanza, baadhi ya lugha inaweza kutafsiri hii kama "wafalme watano dhidi ya wanne".

Genesis 14:10

Sasa

Neno hili linatambulisha taarifa ya nyuma kuhusu bonde la Sidimu. Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kutambulisha taarifa hii ya nyuma.

lilikuwa limejaa mashimo ya lami

"ilikuwa na mashimo ya lami mengi". Haya yalikuwa mashimo katika ardhi ambayo yalikuwa na lami ndani mwao.

lami

kimiminiko kinene, kinachonata, cheusi kinachotoka ardhini.

wafalme wa Sodoma na Gomora

Huu ni usemi mwingine kwa ajili ya wafalme na majeshi yao. "wafalme wa Sodoma na Gomora na majeshi yao"

wakaanguka pale

Maana zaweza kuwa 1) baadhi ya wanajeshi wao walianguka ndani ya mashimo ya lami au 2) wafalme wenyewe walianguka ndani ya mashimo ya lami. Kwa kuwa 14:17 unasema ya kwamba mfalme wa Sodoma alikwenda kukutana na Abramu, maana ya kwanza yaweza kuwa sahihi zaidi.

Wale waliosalia

"Wale ambao hawakufa vitani na hawakuanguka ndani ya mashimo"

adui

Hii ina maana ya mfalme Kedorlaoma na wafalme wengine na majeshi yao aliokuwa nao waliokuwa wakishambulia Sodoma na Gomora.

mali zote za Sodoma na Gomora

Maneno "Sodoma" na "Gomora" ni lugha nyingine kwa ajili ya watu walioishi katika miji ile. "utajiri wa watu wa Sodoma na Gomora" au "mali za watu wa Sodoma na Gomora"

vyakula vyao vyote

"chakula na vinywaji vyao"

wakaenda zao

"wakaenda njia zao"

wakamchukua pia Lutu, mtoto wa ndugu yake na Abramu ambaye aliishi Sodoma, pamoja na mali zake zote

Misemo ya "mwana wa kaka wa Abramu" na "aliyekuwa akiishi Sodoma" unamkumbusha msomaji juu ya mambo yaliyoandikwa mapema kuhus Lutu. "walimchukua Lutu pia, pamoja na na mali zake zote. Lutu alikuwa mwana wa kaka wa Abramu na alikuwa akiishi Sodoma kwa kipindi hicho"

Genesis 14:13

Mmoja ambaye alitoroka alikuja

"Mwanamume alitoroka vitani na kuja"

Alikuwa anaishi

"Abramu alikuwa anaishi" Hii inatambulisha taarifa ya nyuma.

walikuwa washirika wa Abram

"walikuwa washirika wa mkataba na Abramu" au "alikuwa na makubaliano ya amani na Abramu"

ndugu yake

Hii inahusu mpwa wa Abramu Lutu

wanaume waliofunzwa

"wanamume waliofunzwa kupigana"

wanaume waliozaliwa nyumbani mwake

"wanamume waliozaliwa nyumbani mwa Abramu". Walikuwa watoto wa watumishi wa Abramu.

akawafukuza

"akawafukuza"

Dani

Huu ni mji wa kaskazini wa Kanaani, mbali ya kambi ya Abramu.

Genesis 14:15

Akawagawanya watu wake dhidi yao usiku na kuwavamia

Yawezekana hii ina maana ya mipango ya vita. "Abramu aliwagawa wanamume katika makundi kadhaa, na wakawashambulia maadui zao katika pande zote"

mali zote

Hii ina maana ya vitu ambavyo maadui waliiba kutoka miji ya Sodoma na Gomora.

mali zake

"na mali za Lutu ambazo maadui waliiba kutoka kwa Lutu"

pamoja na wanawake na watu wengine

"pamoja na wanawake na watu wengine ambao wafalme wanne waliwakamata"

Genesis 14:17

kurudi

Taarifa inayodokezwa kuhusu wapi alipokuwa anarudi inaweza kuwekwa wazi. "alirudi hadi pale alipokuwa akiishi"

Melkizedeki, mfalme wa Salemu

Hii ni mara ya kwanza mfalme huyu anatajwa.

mkate na divai

Watu hula mkate na divai mara kwa mara.

Genesis 14:19

Alimbariki

Mfalme Melkizedeki alimbariki Abramu.

Abarikiwea Abramu na Mungu aliye juu sana, muumba wa mbingu na nchi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi, ambariki Abramu"

mbingu

Hii ina maana ya sehemu ambayo Mungu huishi.

Mungu aliye juu sana, ambaye amekupatia

"Mungu aliye juu sana, kwa sababu amekupatia". Msemo unaoanza na "ambaye amekupatia" unatueleza jambo zaidi kuhusu Mungu aliye juu sana.

Abarikiwe Mungu aliye juu sana

Hii ni njia ya kumsifu Mungu.

mikono yako

"ndani ya utawala wako" au "ndani ya uwezo yako"

Genesis 14:21

Nipatie watu

Msemo "watu" unaweza kuwa na maana ya watu wa Sodoma ambao maadui waliwakamata. Abramu aliwaokoa alipomuokoa Lutu.

Nimeinua juu mkono wangu

Hii ina maana "nimetoa kiapo" au "nimefanya ahadi".

Sitachukua chochote isipokuwa kile ambacho vijana wamekula

"Ninachukua kutoka kwako kile tu vijana wangu walishakwisha kula". Abramu alikuwa akikataa kupokea chochote kwa ajili yake, lakini alikiri kuwa wanajeshi wake wamekula sehemu ya akiba wakati wa safari ya kurudi Sodoma baada ya vita.

sehemu za watu waliokwenda nami.

Maana kamili ya kauli hii yawezwa kuwekwa wazi. "sehemu ya mali iliyokombolewa iliyokuwa ya wanamume walionisaidia kurudi"

Aneri, Eskoli, na Mamre

Hawa ni washirika wa Abramu (14:13). Kwa kuwa walikuwa washirika wa Abramu walipigana vita pamoja naye. Maana kamili ya kauli inaweza kufanywa wazi. "washirika wangu Aneri, Eskoli na Mamre"