Genesis 10

Genesis 10:1

Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu

"Hii ni habari ya wana wa Nuhu." Sentensi hii inatambulisha habari ya vizazi vya Nuhu katika Mwanzo 10:1-11:9

Genesis 10:2

Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na

"Wana wa yafethi na vizazi vyake waligawanyika na kuhamia pwani na visiwani"

watu wa pwani

Hii ina maana ya watu waliokuwa wakiishi kando ya pwani na visiwani.

ardhi zao

"makazi yao". Hizi ni sehemu ambazo watu waliohama waliishi.

kila mtu na lugha yake

"Kila kundi la watu lilizungumza lugha yake" au " Makundi ya watu walijigawa kulingana na lugha zao"

Genesis 10:6

Misraimu

Misraimu ni jina la Kihebrania la "Misri".

Genesis 10:8

hodari

Maana zaweza kuwa 1) "hodari mwenye nguvu" au 2) "mwanamume mwenye nguvu" au 3) "mtawala mwenye uwezo".

mbele za Yahwe

Maana zaweza kuwa 1) "machoni pa Yahwe" au 2) "kwa msaada wa Yahwe"

Hii ndiyo sababu hunenwa

Hii inatambulisha methali. Lugha yako yaweza tambulisha methali na misemo kwa namna tofauti. "Hii ni sababu watu husema"

Miji ya kwanza

Maana zaweza kuwa 1) miji ya kwanza aliyoijenga au 2) miji muhimu.

Genesis 10:11

alikwenda Ashuru

Nimrodi alikwenda Ashuru

Misraimu akawa

orodha ya vizazi vya Nuhu inaendelea.

Misraimu

Misraimu alikuwa mmoja wa wana wa Hamu. Vizazi vyake vikawa watu wa Misri. Misraimu ni jina la Kihebrania la Misri.

Genesis 10:15

Myebusi ... Mwamori ... Mgirgashi

Majina haya yana maana ya makundi makubwa ya watu walioshuka kutoka Kanaani.

Genesis 10:19

mpaka

"eneo" au "mpaka wa eneo"

ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza

Mwelekeo wa kusini waweza elezwa wazi kama itahitajika. "Kutoka mji wa Sidoni magharibi hata mji wa Gaza, ambao uko karibu na Gerari"

na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha

Mwelekeo ni "mashariki" au "bara" inaweza kuelezwa wazi kama itahitajika. "kisha mashariki mwa miji ya Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hata Lasha"

Hawa walikuwa wana wa Hamu

Neno "hawa" lina maana ya watu na makundi ya watu waliorodhoshwa katika mistari ya 10:6

kwa lugha zao

"waligawanyika kulingana na lugha zao tofauti"

katika ardhi zao

"katika makazi yao"

Genesis 10:24

Arfaksadi

Arfaksadi alikuwa mmoja wa wana wa Shemu.

Pelegi

Jina Pelegi lina maana ya "mgawanyiko"

nchi iligawanyika

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu wa duniani walijigawa wenyewe" au "watu wa duniani waligawanyika kati yao" au "Mungu aligawanya watu wa duniani"

Genesis 10:26

Yoktani

Yoktani alikuwa mmoja wa wana wa kiume wa Eberi.

Hawa

Hapa "hawa" ina maana ya wana wa kiume wa Yoktani.

Genesis 10:30

Mpaka wao

"ardhi walioitawala" au "ardhi walipoishi"

Hawa walikuwa wana wa Shemu

Neno "hawa" ina maana ya vizazi vya Shemu.

Genesis 10:32

Hizi zilikuwa koo

Hii inarudi nyuma kwa watu wote waliorodheshwa katika 10:1

kulingana na

"imeorodheshwa kwa"

kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi

"kutoka kwa koo hizi mataifa yaligawanyika na kusambaa nchini kote" au "Koo hizi ziligawanyika baina yao na kuunda mataifa ya dunia"

baada ya gharika

Hii inaweza kuelezwa dhahiri au kwa uwazi zaidi. "baada ya gharika kuangamiza nchi"