Genesis 47

Genesis 47:1

Akawachukua watano katika ndugu zake

tafsiri inaorodhesha tukio pamoja na Farao katika mpangilio, wakati tafsiri zingine huorodhesha matukio kama mwandishi alivyoandika.

Genesis 47:3

Watumishi wako ni wafugaji

"Watumishi wako wanafuga mifugo"

Watumishi wako

Ndugu wa Yusufu wanajitambua kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. Hii inaweza katika lugha ya mtu wa kwanza. "Sisi, watumishi wako" au "Sisi"

kama mababu zetu

"wote sisi na baba zetu" au "wote sisi na mababu zetu"

Tumekuja kukaa kwa muda katika nchi

"Tumekuja kukaa kwa muda mfupi Misri"

Hakuna malisho

"Hakuna nyasi ya kula"

Hivyo

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Genesis 47:5

Nchi ya Misri iko mbele yako

"Nchi ya Misri ipo wazi kwako" au "Nchi yote ya Misri ipo wazi kwako"

Mkalishe baba yako na ndugu zako katika eneo zuri, nchi ya Gosheni

"Muweke baba yako na ndugu zako katika nchi ya Gosheni, ambayo ni sehemu bora zaidi"

Ikiwa unafahamu watu wenye uwezo miongoni mwao

Inasemekana ya kwamba walikuwa na uwezo wa kuchunga wanyama. "Kama unawajua wanamume wowote miongoni mwao wenye uwezo wa kutunza mifugo"

Genesis 47:7

Yakobo akambariki Farao

Hapa "kubarikiwa" ina maana ya kuonyesha hamu ya mambo chanya na yenye manufaa kutokea kwa mtu huyo.

Umeishi kwa muda gani?

"Una umri gani?"

Miaka ya safari zangu ni mia moja na thelathini

Msemo wa "miaka ya safari zangu" ina maana ya muda ambao aliishi duniani akisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine. "Nimesafiri duniani kwa miaka 130"

Miaka ya maisha yangu imekuwa mifupi ... Siyo kama miaka ya baba zangu.

Yakobo ina maana ya kwamba maisha yake ni mafupi kulinganisha na maisha ya Abrahamu na Isaka.

na ya maumivu

Yakobo ameonyesha maumivu mengi na matatizo wakati wa maisha yake.

Genesis 47:11

Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake

"Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake na kuwasaidia kuimarisha sehemu watakapoishi"

eneo la Ramesesi

Hili ni jina la nchi ya Gosheni.

kulingana na hesabu ya wahitaji wao

Hapa, neno "wahitaji" lina maana ya watoto wadogo katika familia. "kulingana na idadi ya watoto wadogo ndani ya familia zao"

Genesis 47:13

Basi

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya pumziko katika zimulizi kuu. Hapa mwandishi anaanza kuelezea sehemu mpya ya simulizi.

Nchi ya Misri na nchi ya Kanaani

Hii ina maana ya watu wanaoishi katika nchi hizi. "watu wa Misri na watu wa Kaanani"

ikaharibika

"ikawa nyembamba na dhaifu"

Yusufu akakusanya pesa yote iliyokuwa katika nchi ya Misri na nchi ya Kanaani, kwa kuwauzia wakaaji wake nafaka

"Watu wa Misri na Kaanani walitumia pesa yao kununua nafaka kutoka kwa Yusufu"

Yusufu akakusanya ... Yusufu akaleta

Inawezekana Yusufu aliwaamuru watumishi wake kukusanya na kuleta ile pesa"

Genesis 47:15

Pesa yote ya nchi za Misri na Kanaani ilipokwisha

Hapa "nchi" ina maana ya watu wanaoishi katika nchi zile. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Pale ambapo watu wa Misri na Kaanani watakapomaliza pesa yao yote"

ya nchi za Misri na Kanaani

"kutoka katika nchi ya Misri na kutoka katika nchi ya Kaanani"

Kwa nini tufe mbele zako kwa maana pesa yetu imekwisha?

Watu walitumia swali kuweka msisitizo jinsi gani walivyokuwa na haja ya kununua chakula kutokana na kukata tamaa. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Tafadhali, usituruhusu tufe kwa sababu tumetumia pesa yetu yote!"

Akawalisha kwa mkate

Hapa "mkate" una maana ya chakula kwa ujumla. "Aliwapatia chakula" au "Aliwagawia chakula"

Genesis 47:18

wakaja kwake

"watu wakaja kwa Yusufu"

Hatutaficha kwa bwana wangu

Watu wanamtambua Yusufu kama "bwana wangu". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "Hatutajificha kwako, bwana wetu" au "Hatutajificka kutoka kwako"

Hakuna kilichobaki machoni pa bwana wangu

Hapa "machoni" ina maana ya Yusufu mwenyewe. "Hatuna kitu kilichobaki kukupa, bwana wetu"

Kwa nini tufe mbele za macho yake, sisi na nchi yetu?

Neno la "macho" lina maana ya macho ya Yusufu. Watu hutumia swali kuweka msisitizo jinsi walivyo na hamu ya kununua chakula. swali hili linaweza kutasfiriwa kama kauli. "Tafadhali usitazame tu tunavyokufa na nchi yetu inaharibika!"

Kwa nini tufe ... wote sisi na nchi yetu?

Nchi inakuwa haina faida na inaharibika kwa sababu hakuna mbegu ya kupanda; kwa hiyo inazungumziwa kana kwamba nchi itakufa.

Genesis 47:20

Kwa njia hii, nchi ikawa mali ya Farao

"Kwa hiyo nchi ikawa ya Farao"

Ilikuwa ni nchi ya makuhani pekee ambayo Yusufu hakuinunua

"Lakini hakununua nchi ya makuhani"

makuhani walikuwa wakipewa posho

"Posho" ni kiasi cha pesa au chakula ambacho mtu hutoa mara kwa mara mtu mwingine. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Farao aliwapa makuhani kiasi fulani cha chakula kila siku"

Walikula katika sehemu aliyowapa Farao

"Walikula kutoka kwa kile ambacho Farao aliwapatia"

Genesis 47:23

nanyi mtapanda

"ili muweze kupanda"

Wakati wa mavuno, mtampa Farao sehemu ya tano, na sehemu nne zitakuwa zenu

Neno la "tano" ni sehemu. "Wakati wa mavuno utagawanyisha mazao katika sehemu tano. Utatoa sehemu moja kwa Farao kwa ajili ya malipo na sehemu nne ni kwa ajili yenu"

wa chakula cha nyumba zenu na watoto wenu

Unaweza kuwekwa wazi taarifa inayoeleweka. "kwa chakula kwa ajili ya nyumba zenu na kwa chakula kwa ajili ya watoto wenu"

Genesis 47:25

Na tupate kibali machoni pako

Hapa "macho" ina maana ya fikra na mawazo. "Na ufurahishwe na sisi"

tupate kibali

Hii ina maana ya kwamba mtu anakubalika kwa mtu mwingine.

katika nchi ya Misri

"katika nchi ya Misri" au "katika nchi yote ya Misri"

hata leo

Hii ina maana katika kipindi ambacho mwandishi alikuwa akiandika haya.

moja ya tano

tano- Neno la "tano" ni sehemu. "Wakati wa mavuno utagawanyisha mazao katika sehemu tano. Utatoa sehemu moja kwa Farao kwa ajili ya malipo na sehemu nne ni kwa ajili yenu"

Genesis 47:27

Walikuwa wenye kuzaa na kuongezeka sana

Neno "kuongezeka" linaelezea jinsi walivyokuwa "wamezaana". "Walikuwa na watoto wengi sana"

Walikuwa wenye kuzaa

Hapa "kuzaa" ina maana ya kufanikiwa au kupata watoto.

miaka kumi na saba

"miaka 17"

kwa hiyo miaka ya maisha ya Yakobo ilikuwa miaka mia moja arobaini na saba

miaka saba - "kwa hiyo Yakobo aliishi hadi umri wa miaka 147"

Genesis 47:29

Wakati wa kufa kwake Yakobo ulipokaribia

Hii inazungumzia juu ya muda kana kwamba inasafiri na kutua mahali. "Muda wa Israeli kufariki ulipokaribia"

Ikiwa nimepata kibali machoni pako

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo. "Kama nimepata kibali na wewe" au "Kama nimekufurahisha"

sasa

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

nimepata kibali

Hii ina maana ya kwamba mtu amekubalika na mtu mwingine.

weka mkono wako chini ya paja langu

Tendo hili ni ishara ya kufanya ahadi ya dhati.

unionyeshe uaminifu na kweli

Nomino inayojitegemea ya "uaminifu"na "kweli" zinaweza kutafsiriwa kama vivumishi. "nitendee kwa namna ya uaminifu na kweli"

Tafadhari usinizike Misri

Neno "tafadhali" linaongeza msisitizo kwa ombi lake.

Nitakapolala na baba zangu

Hapa "kulala" ni njia ya upole ya kumaanisha kufa. "Nitakapokufa na kujiunga na wa familia yangu waliokufa kabla yangu"

Niapie

"Niahidi" au "Fanya kiapo kwangu"

akamwapia

"allimuahidi" au "alifanya kiapo kwake"