Genesis 18

Genesis 18:1

Mamre

Hili lilikuwa jina la mwanamume aliyemiliki mialoni.

mlangoni pa hema

"katika uwazi wa hema" au "katika kuingilia kwa hema"

joto la mchana

"wakati wa jua kali la mchana"

Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama.

"Alitazama juu na kuona, tazama, wanamume watatu walikuwa wamesimama"

tazama

"ghafla". Neno "tazama" hapa linatuonyesha kitakachofuata ni cha kushangaza kwa Abrahamu.

mbele yake

"karibu" au "pale". Walikuwa karibu na yeye, lakini umbali wa kutosha kwa yeye kuwakimbilia.

kuinama

Hii ina maana kuinama chini na kuonyesha unyenyekevu na heshima kwa mtu.

Genesis 18:3

Bwana

Hili ni jina la heshima. Maana zaweza kuwa 1) Abrahamu alijua ya kuwa mmoja wa wanamume hawa alikuwa Mungu au 2) Abrahamu alijua ya kwamba wanamume hawa walikuja kwa niaba ya Mungu.

machoni pako

Abrahamu anazungumza na mmoja wa wanamume.

usinipite

"tafadhali msiendelee kupita"

mtumishi wako

"mimi". Abrahamu ana maanisha yeye mwenyewe katika njia hii kuonyesha heshima kwa mgeni wake.

Naomba maji kidogo yaletwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Niruhusu nikuletee maji" au "Mtumishi wangu atakuletea maji"

maji kidogo ... chakula kidogo

"maji kidogo ... chakula kidogo." Kusema "kidogo" ilikuwa lugha ya upole ya kuonyesha ukarimu. Abrahamu angewapatia maji na chakula cha kutosha zaidi.

mnawe miguu yenu

Utamaduni huu uliwasaidia wasafiri waliochoka kujiburudisha baada ya kutembea umbali mrefu.

wenu ... mji...

Abrahamu anazungumza na wanamume wote watatu, kwa hiyo "wenu" na "mji..." ni katika hali ya wingi.

Genesis 18:6

vipimo vitatu

kama lita 22

mkate

Mkate huu yawezekana ulikuwa umepikwa haraka katika jiko la moto. Inawezekana ulikuwa tambarare au duara kama mikate midogo midogo ya duara.

kwa haraka

"mtumishi aliharakisha"

akaiandaa

"kuukata na kuubanika"

siagi

Hii ina maana ya sehemu ngumu ya maziwa yaliogandishwa. Inawezekana ilikuwa mtindi au jibini.

ndama aliye kwisha andaliwa

"ndama aliyebanikwa"

mbele yao

"mbele ya wageni watatu"

Genesis 18:9

Wakamwambia

"Kisha wakamwambia Abrahamu"

akasema, "Hakika nitarejea kwako

Neno "akasema" lina maana ya mwanamume ambaye Abrahamu alimwita "Bwana" katika 18:3.

majira ya machipuko

"pale ambapo majira kama haya yatakapowadia mwaka kesho" au "muda kama huu mwaka kesho"

na tazama

Neno "tazama" hapa linatutahadharisha kuwa makini kwa taarifa ya kushangaza inayofuata.

mlangoni pa hema

"katika uwazi wa hema" au "katika kiingilio cha hema"

Genesis 18:11

baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?

nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je nitapata furaha hii ya kupata mtoto? Sarai alitumia swali hili la balagha kwa sababu hakuamini angeweza kupata mtoto. "Siamini ya kuwa nitapitia furaha ya kupata mtoto. Bwana wangu ni mzee sana"

bwana wangu ni mzee

Hii ina maana ya "kwa kuwa mume wangu ni mzee pia".

bwana wangu

Hili ni jina la heshima ambalo Sarai alimpa mumewe Abrahamu.

Genesis 18:13

Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?

Mungu alitumia swali la balagha kuonyesha ya kwamba alifahamu alichokuwa akikifikiria Sarai na ya kwamba hakufurahishwa nacho. Anarudia swali la balagha la Sarai (18:11) kutumia maneno tofauti. "Sarai hakuwa sahihi kucheka na kusema, "Sitazaa mtoto kwa sababu mimi ni mzee sana!"

Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe?

"Je kuna jambo lolote ambalo Yahwe hawezi kufanya?" Yahwe anazungumzia juu yake mwenyewe kana kwamba anazungumzia mtu mwingine kumkumbusha Abrahamu ya kwamba yeye, Yahwe, ni mkuu na anaweza lolote. "Hakuna jambo ambalo mimi, Yahwe, siwezi kufanya!"

katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko

"Katikamuda huo niliouweka, ambao ni wakati wa machipuko"

Kisha Sarai akakataa na kusema

"Kisha Sarai aliukana kwa kusema"

akajibu

"Yahwe alijibu"

hapana ulicheka

"Ndio, ulicheka." Hii ina maana ya "Hapana, hiyo sio kweli; kweli umecheka."

Genesis 18:16

kuwaaga

"kuwaaga kwenda njia yao" au "kusema 'Kwaheri' kwao". Ilikuwa ni jambo la upole kuwasindikiza wageni umbali fulani wakati wanapoondoka.

Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya ...yeye?

Mungu alitumia swali hili la balagha kusema ya kwamba alikuwa akizungumza na Abrahamu kuhusu jambo muhimu sana na kwamba ilimpasa yeye kufanya hivyo. "Sipaswi na sitamficha Abrahamu kile ninachotaka kufanya .... yeye." au "Ninatakiwa na nitamwambia Abrahamu kile ninachotaka kufanya ... yeye"

Je ni ... kufanya, kwa kuwa ... yeye?

"Sitakiwi ... kufanya. Hii ni kwa sababu .. yeye"

katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitawabariki mataifa yote ya duniani kupitia Abrahamu.

katika yeye watabarikiwa

"watabarikiwa kwa sababu ya Abrahamu" au "watabarikiwa kwa sababu nimembariki Abrahamu".

ili awaelekeze

"ya kwamba atawaongoza" au "ili kwamba awaamuru"

waishike njia ya Yahwe ... Yahwe ampatie ... aliyo yasema

Yahwe anazungumza juu yake mwenyewe kana kwamba alikuwa mtu mwingine. "kutii kile ambacho mimi, Yahwe nahitaji....mimi, Yahwe, nitaleta ... nimesema"

waishike njia ya Yahwe

"kutii amri za Yahwe"

watende utakatifu na haki

"kwa kufanya utakatifu na haki" Hii inaelezea namna ya kushikilia njia ya Yahwe.

ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake

"ili kwamba Yahwe aweze kumbariki Abrahamu kama alivyosema angefanya" Hii ina maana ya ahadi ya agano ya kumbariki Abrahamu na kumfanya kuwa taifa kubwa.

Genesis 18:20

kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu

Hii inaweza kuelezwa kwa maneno mengine ili maana halisi ya "kilio" linaloelezwa kama kitenzi cha "kushtaki". "watu wengi sana walikuwa wakishtaki watu wa Sodoma na Gomora kufanya uovu mwingi"

dhambi yao ni kubwa

"wamefanya dhambi sana"

sasa nitashuka pale

"Nitashuka pale sasa hadi Sodoma na Gomora"

nitashuka pale na kuona

"nitashuka pale kujua" au "nitashuka pale kuamua"

kuona kilio ... kilicho nifikia

Yahwe anazungumzia kana kwamba alijua kuhusu jambo hili kwa sababu alisikia kilio na mashtaka yakija kutoka kwa watu waliokuwa wameteseka. Hii inaweza kuwekwa kwa maneno mengine ili kitenzi cha "kilio" kiweze kuelezwa kama kitenzi cha "kushtaki". "waovu kama wale wanaowashtaki wanasema kuwa wako vile"

ikiwa kweli

"kama sio waovu kama kilio kinavyoashiria"

Genesis 18:22

wakageuka toka pale

"aliondoka kutoka katika hema la Abrahamu"

Abrahamu akabaki amesimama mbele ya Yahwe

"Abrahamu na Yahwe walibaki pamoja"

alikaribia

"alimkaribia Yahwe" au "alisogea karibu na Yahwe"

utawafutilia mbali

Abrahamu anazungumzia kuwaangamiza watu kana kwamba alikuwa akifagia takataka kwa ufagio. "kuangamiza"

watakatifu pamoja na waovu

"watu watakatifu na watu waovu"

Genesis 18:24

Taarifa ya Jumla:

Abrahamu anaendelea kuzungumza na Yahwe

Huenda wakawepo

"Chukulia wakawepo"

Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?

Abrahamu alikuwa na tumaini ya kwamba Yahwe angesema, "Sitaikatalia mbali". "Nadhani hautaikatalia mbali. Badala yake, utaiacha kuiharibu sehemu kwa sababu ya watakatifu hamsini ambao wapo pale"

utawakatilia mbali

"kuingamiza". Abrahamu anazungumzia kuwaangamiza watu kana kwamba alifagia uchafu na ufagio. "kuangamiza watu waliokuwa wakiishi pale"

na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?

Abrahamu alikuwa akitumaini ya kwamba Mungu angesema, "Nitaacha kuangamiza sehemu kwa niaba ya watu watakatifu hamsini walioishi pale"

usiuache mji

"ruhusu watu waishi"

kwa ajili ya hao

"kwa sababu ya"

Hasha usifanye hivyo

"Sitapenda ufanye jambo kama hilo" au "Haupaswi kutaka kufanya jambo kama hilo"

hivyo, kuwauwa

"jambo kama hili kama kuwaua" au "jambo kama hilo, yaani, kuwaua"

watakatifu watendewe sawa na waovu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "unatakiwa kuwatendea watakatifu sawa sawa na waovu"

Je Mhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?

Abrahamu alitumia swali hili la balagha kusema kile alichotarajia Mungu kukifanya. "Mhukumu wa ulimwengu wote hakika atafanya kilicho haki" au "Kwa kuwa wewe ni Mhukumu wa ulimwengu wote, hakika utafanya lililo sahihi!"

Mhukumu

Mungu anasemwa kama mhukumu kwa sababu yeye ni mhukumu aliye kamilika ambaye hufanya maamuzi ya mwisho kuhusu mema na mabaya.

Genesis 18:27

Tazama

Msemo wa "tazama" hapa unavuta nadhari juu ya taarifa ya kushangaza inayofuata.

Nimeshika kusema

"Niwie radhi kwa kuwa wazi na kuzungumza na wewe" au "Samahani kwa kudiriki kuzungumza"

kwa Bwana wangu

Abrahamu anaonyesha heshima kwa Yahwe kwa kuzungumza na Yahwe kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mwingine. "kwako wewe, Bwana wangu"

mavumbi na majivu

Sitiari hii inamuelezea Abrahamu kama binadamu, ambaye atakufa na mwili wake kugeuka kuwa vumbi na majivu. "ni binadamu pekee" au "kama vile vumbi na majivu yasivyokuwa na umuhimu"

watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini

"watu arobaini na tano tu watakatifu"

kwa upungufu wa hao watano

"iwapo kuna watu watano pungufu watakatifu"

Sitaangamiza

"Sitaangamiza Sodoma"

Genesis 18:29

Akaongea naye

"Abrahamu akazungumza na Yahwe"

ikiwa arobaini watapatikana pale

Hii ina maana ya "ikiwa ukapata watu watakatifu arobaini Sodoma na Gomora"

Akajibu

"Yahwe akajibu"

Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini

"Sitaangamiza miji iwapo nitakuta watu watakatifu arobaini pale"

thelathini

"watu thelathini watakatifu" au "watu thelathini wazuri"

Tazama

Msemo wa "tazama" hapa unavuta nadhari juu ya taarifa ya kushangaza inayofuata.

Nimeshika kusema

"Niwie radhi kwa kuwa wazi na kuzungumza na wewe" au "Samahani kwa kudiriki kuzungumza"

ishirini

"watu ishirini watakatifu" au "watu ishirini wazuri"

Genesis 18:32

Huenda kumi wakaonekana kule

"Huenda utakuta watu kumi watakatifu pale"

kumi

"watu kumi watakatifu" au " watu kumi wazuri"

Kisha akasema

"Na Yahwe akajibu"

kwa ajili ya hao kumi

"ikiwa nikipata watu kumi watakatifu pale"

Yahwe akaendelea na njia yake

"Yahwe aliondoka" au "Yahwe alienda"