Genesis 17

Genesis 17:1

Abram alipokuwa na umri wa miaka tisini na tisa

miaka mia tisa na tisa - Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Mungu wa uwezo

"Mungu mwenye uweza wote" au "Mungu ambaye ana uwezo wote"

Uende mbele yangu

Kuenda ni sitiari kwa ajili ya kuishi, na "mbele yangu" au "katika uwepo wangu" hapa ni sitiari kwa ajili ya kutii. "Ishi kwa namna nayotaka uishi" au "Kunitii"

Kisha nitalithibitisha

"Iwapo utafanya hivi, basi nitathibitisha"

nitalithibitisha agano langu

"Nitatoa agano langu" au "Nitafanya agano langu"

agano

Katika agano hili Mungu anamuahidi kumbariki Abramu lakini pia anataka Abramu amutii.

nitakuzidisha sana

"nitazidisha kwa wingi idadi ya vizazi vyako" au "nitakupatia vizazi wengi sana"

Genesis 17:3

Abramu akainama uso wake hadi chini ardhini

"Abramu alijirusha uso chini ya ardhi" au "Abrahamu aliinama chini mara moja uso ukiwa ardhini." Alifanya hivi kuonyesha ya kuwa alimheshimu Mungu na angemtii.

Mimi

Mungu alitumia msemo huu kutambulisha kile alichoenda kukifanya kwa Abramu kama sehemu ya agano lake na Abramu.

tazama, agano langu liko nawe

Neno "tazama" hapa linasema ya kwamba kinachofuata ni cha uhakika: "agano langu na wewe ni la uhakika"

baba wa mataifa mengi

"baba wa idadi kubwa ya mataifa" au "yule ambaye mataifa mengi yatajiita"

Abrahamu

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi yafuatayo: Jina "Abramu" lina maana ya "baba aliyeinuliwa" na jina "Abrahamu" linafanana na "baba wa kundi"

Nitakufanya uwe na uzao mwingi

"Nitakusababisha uwe na vizazi vingi sana"

nitakufanya mataifa

"Nitasababisha vizazi vyako kuwa mataifa"

wafalme watatoka kwako

"miongoni mwa vizazi vyako kutakuwa na wafalme" au "baadhi ya vizazi vyako kutakuwa na wafalme"

Genesis 17:7

Taarifa ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Abrahamu.

katika vizazi vyao

"katika kila kizazi"

kwa agano la milele

"kama agano ambalo litadumu milele"

Mungu kwako na kwa wazao wako baada yako

"kuwa Mungu wako na vizazi vyako" au "agano"

Kanaani, kuwa miliki ya milele

"Kanaani, kama miliki ya milele" au"Kanaani, kuimiliki milele"

Genesis 17:9

nawe

Mungu anatumia msemo huu kutambulisha kile Abramu alichokuwa akielekea kufanya kama sehemu ya agano la Mungu na yeye.

ulishike agano langu

"fuata agano langu" au "heshimu agano langu" au "tii agano langu"

Hili ndilo agano langu

"Hili ni hitaji la agano langu" au "Hii ni sehemu ya agano langu". Sentensi hii inatambulisha sehemu ya agano ambayo Abramu ilimpasa afanye.

Kila mwanaume wa kwenu lazima atahiriwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Unapaswa kutahiri kila mwanamume miongoni mwako"

Kila mwanaume

Hii ina maana ya wanadamu wa kiume

Lazima mtatahiriwa katika nyama ya govi la ngozi ya mbele

Baadhi ya jamii inaweza kutumia lugha nyepesi zaidi kama "Unatakiwa kutairiwa." Iwapo tafsiri yako ya "fanya tohara" inajumlisha neno la govi la ngozi ya mbele, hauhitaji kurudia.Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Unatakiwa kuwatahiri wanamume wote miongoni mwenu"

ishara ya agano

"ishara inayoonyesha ya kwamba agano lipo"

ishara

Maana zaweza kuwa 1) "ishara" au 2) "ishara". Maana ya kwanza inaonyesha kulikuwa na ishara moja, na maana ya pili inaonyesha kulikuwa na ishara zaidi ya moja. Hapa neno "ishara" ina maana ya ukumbusho kuhusu jambo ambalo Mungu aliahidi.

Genesis 17:12

Taarifaya Jumla

Mungu anaendelea kuzungumza na Abrahamu.

Kila mwanaume

"Hii ina maana ya wanadamu wa kiume"

katika vizazi ya watu wenu

"katika kila kizazi"

yeye ambaye amenunuliwa kwa fedha

Hii ina maana ya watumwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mwanamume yeyote utakayemnunua"

agano langu litakuwa katika mwili wenu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utaweka alama ya agano langu juu ya mwili wako"

kuwa agano la milele

"kama agano la kudumu". Kwa sababu iliwekwa juu ya mwili, hakuna aliyeweza kuifuta.

Mwanaume yeyote asiye tahiriwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda, na unaweza kuacha maneno ambayo yanaweza kuleta maana mbaya katika lugha yako. "mwanamume ambaye haujamtahiri"

Mwanaume yeyote asiye tahiriwa ... govi la ngozi yake ya mbele atatengwa na watu wake

Maana zaweza kuwa 1) "nitamtenga mwanamume yeyote asiyetahiriwa ... govi la mbele kutoka kwa watu wake" au 2)"Ninataka umtenge mwanamume yeyote asiyetahiriwa ... govi la mbele kutoka kwa watu wake"

atatengwa na watu wake

Maana zaweza kuwa 1) "aliuawa" au 2) "kufukuzwa kutoka kwenye jamii".

Amevunja agano langu

"Hajatii amri za agano langu." Hii ni sababu itakayomfanya atengwe kutoka kwa watu wake.

Genesis 17:15

kwa habari ya Sarai

Maneno "kwa habari ya" zinatambulisha mtu anayefuata ambaye Mungu anamzungumzia.

nitakupatia mtoto wa kiume kwake

"Nitamfanya azae mtoto kupitia kwake"

atakuwa mama wa mataifa

"atakuwa mama wa mataifa mengi" au "uzao wake watakuwa mataifa"

Wafalme wa watu wa mataifa watapatikana kutokana na yeye

"Wafalme wa watu watatokana kwake" au "Baadhi ya uzao wake watakuwa wafalme wa watu"

Genesis 17:17

akasema moyoni mwake

"akawaza mwenyewe" au "akasema mwenyewe kimya kimya"

Je yawezekana mtoto azaliwe kwa mwanaume ambaye ana umri wa miaka mia moja?

Abrahamu alitumia swali hili la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. "Hakika mwanamume mwenye umri wa miaka mia moja hawezi kuwa baba wa mtoto!"

Je Sara, ambaye ana umri wa miaka tisini anaweza kuzaa mwana?

Tena Abrahamu alitumia swali la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. msemo "ambaye ana umri wa miaka tisini" unasema kwa nini Abrahamu hakuamini ya kwamba Sarai hataweza kuzaa mtoto. "Sarai ana umri wa miaka tisini. Hakika hawezi kuzaa mtoto wa kiume!"

Lau Ishmaeli angeweza kuishi kabla yako!

"Tafadhali muache Ishmaeli arithi agano ulilofanya pamoja na mimi" au "Huenda Ishmaeli anaweza kupokea baraka ya agano lako" Abrahamu alipendekeza jambo ambalo aliamini lingeweza kutokea"

Genesis 17:19

Hapana, Sarai mkeo atakuzalia

Mungu alisema hili kusahisha imani ya Abrahamu juu ya Sarai kupata mtoto.

utamwita jina lake

Neno "utamwita" linamlenga Abrahamu.

Na kwa habari ya Ishmaeli

Maneno "na kwa habari" yanaonyesha ya kwamba Mungu anabadilisha maongezi kuhusu mtoto ambaye angezaliwa na kumuongelea Ishmaeli.

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini kwa kile nachotaka kukuambia"

nitamfanya kuwa na uzao

Hii ni lahaja inayokuwa na maana ya "nitamsababisha awe na watoto wengi"

na kumzidisha maradufu

"na nitamsababisha awe na uzao mwingi"

viongozi wa makabila

"machifu" au "watawala". Hawa viongozi sio wana kumi na mbili na wajukuu wa Yakobo ambao wataongoza makabila kumi na mbili ya Israeli.

Lakini agano langu nitalifanya imara na Isaka

Mungu anarudi kuongelea juu ya agano lako na Abrahamu na kusisitiza ya kwamba atatimiza ahadi yake na Isaka, na sio Ishmaeli.

Genesis 17:22

Alipo kuwa amemaliza kuzungumza naye

"Mungu alipomaliza kuzungumza na Abrahamu"

Mungu akaondoka kwa Abraham

"Mungu akamuacha Abrahamu"

kila mwanaume miongoni mwa watu wa nyumba ya Abraham

"kila binadamu wa kiume katika nyumba ya Abrahamu" au "kila mtu wa kiume katika nyumba ya Abrahamu". Ina maana ya wanadamu wa kiume wa umri wote: watoto wachanga, wavulana na wanamume.

Genesis 17:24

ni pamoja na wale waliozaliwa katika nyumba ile na wale walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni

"Hii inajumlisha wale waliozaliwa katika nyumba yake na wale walionunuliwa kutoka kwa wageni"

wale walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni

Hii ina maana ya watumishi au watumwa

wale walionunuliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wale ambao amekwisha wanunua"