Genesis 13

Genesis 13:1

akaondoka kutoka

"kwenda" au "kuondoka kutoka"

akaenda Negebu

Negebu ilikuwa ni eneo la jangwa kusini mwa Kanaani, magharibi mwa Misri. Hii inaweza kufanywa kwa uwazi. "akarudi katika jangwa la Negebu"

Abram alikuwa tajiri wa wanyama, fedha na dhahabu

"Abramu alikuwa na wanyama wengi, fedha nyingi na dhahabu nyingi"

wanyama

"mifugo" au "ng'ombe"

Genesis 13:3

Aliendelea na safari yake

Abramu na familia yake walisafiri kwa hatua, kwenda kutoka sehemu hadi sehemu. Hii inaweza kufanywa wazi. "Waliendelea na safari yao"

mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo

Watafsiri wanaweza kuweka maandishi machache yanayosema "Tazama Mwanzo 12:8." Muda wa safari yake unaweza kuwekwa wazi. "katika eneo alipotenga hema lake kabla hajakwenda Misri"

akaliitia jina la Yahwe

"aliomba katika jina la Yahwe" au"alimuabudu Yahwe"

Genesis 13:5

Sasa

Neno hili linatumika kuonyesha kitakachofuatia ni taarifa ya nyuma kumsaidia msomaji kuelewa matukio yatakayofuata.

Nchi haikuwatosha wote

Hapakuwa na ardhi ya kutosha ya malisho na maji kwa ajili ya wanyama wao.

mali zao

Hii inajumuisha mifugo, ambayo inahitaji malisho na maji.

hawakuweza kukaa pamoja

"hawakuweza kuishi pamoja"

Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo

Hii ni sababu nyingine ya nchi kutoweza kuwahimili wote.

Genesis 13:8

Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi,

"Tusigombane"

ugomvi

"chuki" au "ugomvi" au "malumbano"

na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu

"na tuwazuie wanaume wanaochunga wanyama wetu kulumbana"

licha ya hayo sisi ni familia

"kwa sababu sisi ni familia"

familia

"ndugu" au "jamaa". Lutu alikuwa mpwa wa Abramu.

Je nchi hii yote haiko mbele yako?

Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa katika hali ya chanya. "nchi nzima ipo wazi kwa matumizi yako"

Nenda na ujitenge na mimi

Abrahamu alizungumza kwa huruma na Lutu na kumtia moyo afanye jambo litakalowasaidia wote. "Tugawanyike".

Ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto

Maana zaweza kuwa 1) "ukienda njia moja, basi na mimi nitaenda njia nyingine" au 2) "ukienda kaskazini, nitaenda kusini." Abramu alimruhusu Lutu kuchagua sehemu ya nchi aliyoitaka, na Abramu angechukua kile kilichobaki.

Genesis 13:10

nchi yote tambarare ya Yorodani

Hii ina maana ya eneo la jumla la mto Yordani.

ilikuwa na maji kila mahali

"ilikuwa na maji mengi"

kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri

"kama bustani ya Yahwe au kama nchi ya Misri". Haya yalikuwa maeneo mawili tofauti.

bustani ya Yahwe

Hili ni jina lingine kwa bustani ya Edeni.

bustani

Hii yaweza kuwa shamba la miti ya matunda au eneo lenye kila aina ya miti.

Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora

Hii inatazamia jambo litakalotokea baadae. Hapa ni muhimu kwa sababu inaeleza kwa nini Lutu alikaa katika eneo ambalo baadae halikuwa na mbolea.

ndugu

"ndugu wa karibu" au "familia". Hii ina maana ya Lutu na Abramu pamoja na nyumba zao.

Genesis 13:12

akaishi

"akatulia" au "akakaa"

nchi ya Kanaani

"nchi ya watu wa Kanaani"

Akatandaza hema zake hadi Sodoma

Maana zaweza kuwa 1) "alitandaza mahema yake karibu na Sodoma" au 2) "Alisogeza mahema yake kuzunguka eneo lililofika hadi Sodoma".

Genesis 13:14

baada ya Lutu kuondoka kwake

"baada ya Lutu kumuacha Abrahamu"

Genesis 13:16

tembea katika urefu na upana wa nchi hii,

"kutembea tembea juu ya ardhi nzima"

Mamre

Hii ilikuwa jina la mwanamume aliyemiliki miti ya mwaloni.

Hebroni

jina la sehemu

madhabahu ya Yahwe

"dhabahu la kumuabudu Yahwe"