Genesis 12

Genesis 12:1

Sasa

Neno hili linatumika kuweka alama sehemu mpya ya simulizi.

Nenda utoke katika nchi yako, na toka kwa ndugu zako

"Nenda kutoka nchini kwako, kutoka katika familia yako"

Nitakufanya uwe taifa kubwa

Hapa "nitakufanya" ni umoja na ina maana ya Abramu, lakini Abramu anawakilisha vizazi vyake. "Nitaanzisha taifa kubwa kupitia kwako" au "Nitawafanya vizazi vyako kuwa taifa kubwa"

na kulifanya jina lako kuwa kubwa

Neno "jina" linawakilisha sifa ya mtu. "na kukufanya uwe maarufu"

na utafanyika baraka

neno "jina" linawakilisha sifa ya mtu. "na kukufanya uwe maarufu"

asiye kuheshimu nita mlaani

"Nitamlaani yeyote atakayekutendea jambo kwa njia ya aibu" au "iwapo kuna mtu atakayekutendea jambo lisilofaa, nitamlaani"

Kupitia kwako familia zote za nchi zitabarikiwa

Hii inaweza kufanywa katika hali ya kutenda. "Nitabariki familia za nchi kupitia kwako"

Kupitia kwako

"Kwa sababu yako" au "Kwa sababu nimekubariki"

Genesis 12:4

walivyomiliki

Hii inajumlisha wanyama na mali isiyokuwa na uhai

Watu ambao wamewapata

Maana yaweza kuwa 1) "watumwa ambao wamewakusanya" au 2) "watu ambao wamewakusanya kuwa pamoja nao"

Genesis 12:6

Abramu akapitia katikati ya nchi

Ni jina la Abramu pekee linatajwa kwa sababu alikuwa kichwa cha familia. Mungu alimpatia amri ya kuchukua familia yake na kwenda kule. "Kwa hiyo Abramu na familia yake walikwenda katikati ya nchi"

nchi

"nchi ya Kanaani"

mwaloni wa More

Yawezekana More ilikuwa jina ya sehemu

Yahwe aliyemtokea Abramu

"Yahwe, kwa sababu alimtokea"

Genesis 12:8

alipiga hema yake

Abramu alikuwa na watu wengi pamoja naye alipokuwa akisafiri. Watu waliokuwa wakihama kutoka sehemu moja hadi nyingine waliishi ndani ya mahema. "walitengeneza mahema yao"

kuliitia jina la Yahwe

"waliomba kwa jina la Yahwe" au "kumuabudu Yahwe"

Kisha Abram akaendelea kusafiri

"Kisha Abramu alichukua hema lake na kuendelea na safari"

upande wa Negebu

"kuelekea eneo la Negebu" au "kuelekea kusini" au "kusini ya jangwa la Negebu"

Genesis 12:10

Kulikuwa na njaa

Mazao hayakuota vizuri msimu huo.

katika nchi

"katika eneo" au "katika nchi ambapo Abramu alikuwa akiishi"

akaenda chini kuingia

Maana zaweza kuwa 1) "alikwenda kusini zaidi" au 2) "aliondoka mbali na Kaanani kuingia". Ingependeza kutafsiri kwa kutumia maneno ya kawaida ya kutoka eneo la juu kuelekea eneo la chini.

wataniua mimi ... wewe hai

Sababu watakayomuua Abramu inaweza kufanywa wazi. "wataniua ili kwamba wakuoe"

ili kwamba niwe salama kwa sababu yako

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba, kwa sababu yako, hawataniua mimi"

Genesis 12:14

Ikawa kwamba

Maana zaweza kuwa 1) Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya wapi tukio linaanza, na kama lugha yako ina namna ya kufanya hivi basi tumia njia hiyo, au 2) "Na hivyo ndivyo kilichotokea"

Wakuu wa Farao wakamuona

"Wakuu wa Farao walimwona Sarai" au "wakuu wa Farao walimwona"

mwanamke akachukuliwa kupelekwa nyumbani mwa Farao

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Farao akamchukua mpaka nyumbani kwake" au "Farao aliwaamuru askari wake kumpeleka nyumbani kwake"

mwanamke

Sarai

nyumbani mwa Farao

Maana zaweza kuwa 1)"Familia ya Farao", yaani kama mke au 2) "Nyumba ya Farao" au "Hekalu la Farao" ni tasifida ya Farao kumfanya awe mmoja wa wake zake.

kwa ajili yake

"kwa ajili ya Sarai" au "kwa sababu yake"

Genesis 12:17

kwa sababau ya Sarai, mke wa Abramu

Hii inaweza kufanywa kwa uwazi zaidi. "Kwa kuwa Farao alitaka kumchua Sarai , mke wa Abramu, aweze kuwa mke wake mwenyewe"

Farao akamwita Abramu

"Farao akamuita Abramu" au "Farao akamuamuru Abramu kuja kwake"

Nini hiki ambacho umenifanyia?

Farao alitumia lugha hii ya balagha kuonyesha jinsi gani alivyokasirika juu ya kile Abramu alichomfanyia. Inaweza kuelezeka kwa namna ya mshangao. "Umedanya jambo baya kwangu!"

Kisha Farao akatoa amri kwa watu wake kuhusiana naye

"Kisha Farao akawaongoza wakuu wake kuhusu Abramu"

na wakamuondoa, yeye pamoja na mke wake na vyote alivyokuwa navyo

"na wakuu wakamfukuza Abramu kutoka kwa Farao, pamoja na mke wake na alivyokuwa navyo"