Genesis 11

Genesis 11:1

Sasa

Neno hili linaonyesha kuwa mwandishi anaanza sehemu mpya ya simulizi.

nchi yote

watu wote juu ya nchi

inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba watu wote walizungumza lugha moja.

waliposafiri

"walihama" au "sogea pande zote"

upande wa mashariki

Yawezekana maana ni 1) "mashariki" au 2) "kutoka mashariki" au 3) "kuelekea mashariki". Chaguo linalofaa ni "mashariki" kwa sababu Shinari ipo upande wa mashariki ambapo wasomi wanaamini safina ilikuja kutulia.

wakakaa

waliacha kusogea kutoka sehemu moja hadi nyingine na wakaanza kuishi sehemu moja.

Genesis 11:3

haya njooni

"haya njooni"

tuyachome kikamilifu

Watu hutengeneza matofali kwa udongo na kuyachoma ndani ya joko la moto sana ili yawe magumu na imara.

lami

kimiminiko kinene, kinachonata, cheusi kinachotoka ardhini.

chokaa

hiki ni kiini kinene kinachoundwa kwa unga wa ndimu, udongo, mchanga, na maji inayotumika kufanya mawe au matofali kugandamana.

tujifanyie jina

"tujifanyie sifa yetu kuwa kubwa"

jina

"sifa"

tutatawanyika

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "tutajigawanya baina yetu na kuishi sehemu tofauti"

Genesis 11:5

wazao wa Ibrahimu

"watu"

akashuka

Habari kuhusu mahali aliposhuka inaweza kuwekwa wazi. "akashuka kutoka mbinguni". Hii haielezi jinsi gani alishuka kutoka mbinguni.

kuona

"angalia kwa makini" au "kutazama kwa makini zaidi"

watu hawa ni taifa moja na lugha moja

Watu wote walikuwa katika kundi moja kubwa na wote walizungumza lugha moja.

wanaanza kufanya hivi

Yawezekana maana kuwa 1) "wameaanza kufanya hivi" ikimaanisha ya kwamba wameanza kujenga mnara lakini haijakamilika au 2)"hili ni jambo la kwanza walilofanya", ikimaanisha ya kwamba katika siku za usoni watafanya mambo makubwa zaidi.

halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kila jambo wanalikusudia kufanya litawezekana kwao"

Haya! Njooni

"haya! njooni"

tushuke

Neno "tushuke" ni wingi ingawa ina maana ya Mungu. Tafsiri zingine husema "na nishuke" au "nitashuka"

tuvuruge lugha yao

Hii ina maana ya kwamba Yahwe angesababisha watu wote wa nchi kukoma kuzungumza lugha moja. "kuchanganya lugha yao"

ili kwamba wasielewane

Hii ilikuwa lengo la kuchanganya lugha yao. "ili kwamba wasiweze kuelewa kile mwingine anachokisema"

Genesis 11:8

kutoka pale

"kutoka katika mji"

jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga

Jina la "Babeli" linaonekana kama neno lenye maana ya "kuchanganyikiwa"

alivuruga lugha ya nchi yote

Ina maana ya kwamba Yahwe alisababisha watu wote katika nchi kutozungumza lugha moja. "alichanganya lugha ya nchi yote"

Genesis 11:10

Taarifa ya jumla

Sura iliyosalia inaorodhesha mtiririko wa vizazi vya Shemu mpaka vya Abramu.

Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu

Sentensi hii inaanza orodha ya vizazi vya Shemu.

gharika

Hii ilikuwa gharika kutoka kipindi cha Nuhu ambapo watu walikuwa waovu sana mpaka Mungu akatuma gharika nchi yote kufunika nchi.

akawa baba wa Alfaksadi

"akapata mwana wake wa kiume Alfaksadi" au "mwana wake wa kiume Alfaksadi alizaliwa"

Alfaksadi

jina la mwanamume

mia moja ... miwili ... mia tano

Watafsiri wanaweza kuandika maneno au namba "100", "2", and "500".

Genesis 11:12

akawa baba wa Shela

"mwana wa kiume wake Shela alizaliwa"

Shela

jina la mwanamume

Genesis 11:14

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:16

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:18

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:20

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:22

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:24

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Abramu, Nahori, na Harani

Hatujui mpangilio wa kuzaliwa kwa watoto wake.

Genesis 11:27

Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera

Sentensi hii inatambulisha habari ya vizazi vya Tera. Mwanzo 11:27-25:11 unazungumzia kuhusu vizazi vya Tera, mahsusi mwanae Abrahamu. "Hii ni habari ya vizazi vya Tera"

Harani akafa machoni pa baba yake Tera

Hii ina maana ya kwamba Harani alikufa wakati baba yake akiwa hai. "Harani alikufa wakati baba yake, Tera, alipokuwa naye"

Genesis 11:29

wakajitwalia wake

"akaoa wake"

Iska

hili ni jina la kike

Sasa

Neno hili linatumiwa kutambulisha habari mpya kuhusu Sarai ambayo itakuwa muhimu baadae katika sura.

tasa

Lugha hii inaelezea mwanamke ambaye kimwili hawezi kutunga mimba au kuzaa mtoto.

Genesis 11:31

akamtwaa

Hapa neno "mwana wa" lina maana ya Tera.

Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abramu

mkwewe, mwanawe mke wa Abramu - "mkwe wa Sarai, ambaye alikuwa mke wa mwanawe Abramu.

Harani ... Harani

Haya ni majina mawili tofauti na yanaandikwa tofauti Kihebrania. Moja lina maana ya mtu na lingine lina maana ya mji.